MjajaroKaterero
Member
- Sep 22, 2023
- 57
- 103
Kuzaliwa 2001Hello!
Tangu kale na kale vijana, wazee, watoto na watu wa Rika zote wanakufa lakini sasa hii trending ya vifo vya vijana ina walakini.
Nimetafakari kwanini vijana wanakufa sana, kijana anakufa anawaacha wazazi wake wakiwa na nguvu, kijana anakufa anawaacha bibi na babu zake wangali hai.
Mungu kanipa jibu kuwa dhambi ndizo zinawaua vijana mapema. Mimi sijui ni dhambi gani, nimeambiwa tu dhambi ndio sababu kubwa.
Acheni dhambi vijana mtakwisha na kuwaachia wazazi wenu makovu moyoni. Kijana anasoma anahangahikiwa kazi anaanza kazi tu anakufa.
Kijana mwingine anaoa tu anakufa. Kijana mwingine anamaliza ujenzi wa nyumba yake anataka ahamie umauti unamkuta.
Acheni dhambi vijana, naongea katika Roho.
Kufa 2023...