Shida zilipokubana uliwahi kuuza kitu gani kwa bei ya hasara ili ujinasue?

gearbox

JF-Expert Member
Joined
Apr 20, 2024
Posts
563
Reaction score
1,768
Gari niliyonunua milioni 5 nikiwa nimeitumia miezi miwili tu niliiuza kwa milioni 1 na laki 3 kumaliza kesi flani isifike mbali tumalizane kimya kimya, pesa ilikuwa inahitajika fasta hivyo mteja ilibidi awe wa fasta, kuna watu wengi wameishia jela kwa kuchukulia vitu poa kwa jicho la mtaani kwamba ni kawaida, unapopata nafasi ya ku negotiate itumie!

Laptop nilinunua laki 8, niliuza kwa laki 2 na nusu ili nikamilishe ada.
 
Kesi gani ya kulawiti?
Kulawiti mbali sana huko.

Huku mitaani watu wanachukulia mambo kirahisi rahisi wanaenda jela kama masihara, hata kumkonyeza mtu ni shambulio la aibu jela miaka mitano ama utoboke mifuko. Kununua simu kwa mtu inaweza kuwa ya wizi waweza kwenda jela miaka 10 au kutoboka mifuko mpaka milioni 3 maana alieibiwa nae ataongeza uongo mlimuibia na pesa, unavuta sigara yako tayari kesi kwamba unavuta hadharani, n.k. sasa ukutana na mwenye usongo wa kesi, utajuta!
 
Hiyo hali ikikufikia ina maumivu sana, hadi unapokutana na mabandiko haya ya kukumbusha huo wakati unapata hisia za maumivu ya wakati ule.

Mimi nilipoteza biashara kubwa, shida mshirika wangu alikanyaga nyaya za moto mahali. Sasa hivi, sitaki hata kupita kwenye mtaa Magore, Upanga.

Ova
 
Figo
 
Mmmh ilikuaje mkuu
 
πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚ mnacheza na usalama kizembe?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…