Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hii inabidi uweke thread watu wajifunze.Mimi Hadi Sasa nimechoma zaidi ya milioni mia tatu na sijatoboa hapa hata buku Sina.
Bora ningeziwekezea kwenye zipu.
Heri yako wewe uliyekuwa na uthubutu ukajaribu, kwa maana mpaka hapo kuna kitu umeshajifunza, ukianza tena utaanza vyema zaidi. Amka, anza tena, mtangulize Mungu, nawe utafanikiwa, amini nakwambia.2024 niliweka malengo ya biashara.. aisee nimepigwa na fataki
Mapema iwezekanavyo. Kuna wanaoanza biashara wakiwa bado wanasoma shule za primary. The earlier the better.Ni umri gani sahihi wa kuanza biashara mkuu.?
Biashara inahitaji watu wagumu na mabahili ,kuna mda inafika ata kula inabidi usile ili biashara iendelee
Raha ya biashara uijue kiundani wekeza muda wako mwingi pale ...datss waajiriwa wengi walio na biashara wanafail hapo wanatamani yale maokoto yanayopatikana bila kujua kuwa waliowaajiri wanafaidi sana nguvu zao bila wao kujua maana wanambinu zote za kuiba na aasikamatwe na mabosi zao..unakuta boss hajui chochote katika biashara yake anafungua hardware hajui kifaa hata kimoja ..anafungua saloon hajui kusuka..anafungua stationery hajui matumizi ya photocopy mashine wala computer.. msaidizi asipokuwepo shughuli zote zinasimama maana boss hana analololijua na hajawekeza muda wake katika biashara utaletewa hesabu za hovyo unajikuta mtaji umepukutika ..kwa hapo lazima upigwe na ulizweHapo kama Umeajiriii watesiii na huna uzoefuuu subirii upukutishweeee...[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787] Yani biashara kama huna muda binafsi wa kuifatilia kwa karibu na huna experience nayo mwaka wa kwanza ni wa kujifunza kubali hasaraa
Alafu kingine boss usipokuwa makini unajikuta huendani na bei za sokoni..eidha unauza bei chini zaidi au ya juu zaidi wateja wakakimbia msaidizi hana muda huo kufatilia anachojar ni maokoto...biashara ni kama mtoto inahitaji ukaribu ..uipende na uitumikie kwa kuwekza muda wako utajua muelekeo wake nn uboreshe zaidi ili kuhakikisha biashara inasimama na kukua,bado unayo nafasi simama jipange upya fanyia marekebisho hizo changamoto utatoboaMda,wasimamizi,kukosa uzoefu,washauri,umbali,timing,buy cheap ni baadhi TU ya factor zilizonikwamisha
Naamini saSa umekwiva mkuuMda,wasimamizi,kukosa uzoefu,washauri,umbali,timing,buy cheap ni baadhi TU ya factor zilizonikwamisha
Unaweza ukaanguka mara moja usiinuke tena, na ukafa.Usiogope, unaweza kuanguka hata mara Kumi na ukasimama tena mambo yakanyooka... Ila nyie🙌🙌
Wee jamaa😃😂😂.. Acha kumtisha kijanaUnaweza ukaanguka mara moja usiinuke tena, na ukafa.
Tuambie ni kwa namna gani uliweza kusimama tena mkuu... ili na sisi tujifunzeKudumu kwa biashara inategemea na factors nyingi Location, demand, mtaji, msimamizi, sera za kiuchumi n.k
Mfano mwaka 2014 nilianzisha biashara ile biashara ilianza vizuri sana na akachanganya sana, ilifanya vizuri kwa sababu ya mazingira biashara ilipokuwepo kulikuwa hakuna access ya barabara pana ya kupita malori, barabara pana ilikuwa inaishia kwangu kwahiyo wateja walikuwa wanatoka maeneo mbalimbali kuja kununua bidhaa kwangu kwa jumla halafu wanasomba na mikokoteni kuingia huko ndani ndani.
Mwaka 2017 ukaja mradi wa kukarabati barabara za mitaani, watu wakalipwa na barabara zikapanuliwa kwa kiwango cha lami.
Nikapoteza wateja wa jumla wote, biashara yangu mauzo yakadrop ile mbaya mwisho ikafa.
Biashara ya pili ilikuwa ya duka baada ya barabara kukarabatiwa zilijengwa frame nyingi sana, yakafunguliwa maduka mengi biashara zinazofanana, bidhaa nyingi wateja wachache. Duka likaangukia pua.
Kwahiyo kudumu kwa biashara muda mrefu kuna sababu nyingi sana. Ila nilichojifunza jitahidi kuwa mfanyabiashara wa kati wa Jumla/mtaji mkubwa na sio mfanyabiashara wa mwisho.
Oukay, maana yake ulikata tamaa kabisa kwa wakati ule??Niliachana na biashara nikaingia kwenye ajira, ndio najipanga tena kufungua biashara nikiwa kwenye ajira.
Shida ya kuanza biashara ukubwani!!!Wakuu
Wale mliofanikiwa kuanzisha biashara zenu na zimedumu mpaka sasa SHIKAMOONI WAKUBWA. Hili game sio la kitoto for beginners.
Duuh.. Unanitisha mkuu😃😃Ndugu pale matumizi ya kawaida ya familia yanapokuwa makubwa kuliko faida ni stress kubwa, huoni pakutokea tena kwenye biashara, halafu unatakiwa ulipe kodi za watu hujui unaipatia wapi, madeni ya mikopo kila siku hodiii dukani, huna backup, only option ilikuwa kujiondoa.
Nikatangaza kuuza biashara watu wengi wakajitokeza kuinunua kwa historia yake, nikaiuza bei nzuri sana.
Niliyemuuzia naye ameshaifunga [emoji3] sidhubutu hata kumsalimia ananiulaumu balaa.