John Haramba
JF-Expert Member
- Feb 4, 2022
- 365
- 1,374
Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu amezungumzia mafanikio ya mwaka mmoja wa Serikali ya Awamu ya Sita, amezungumza akiwa katika Ofisi za Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), leo Machi 4, 2022.
Haya hapa ni baadhi ya mambo muhimu ambayo ameyazungumza ambayo yamekuwa na faida kubwa kwa raia wa kawaida.
#Serikali imeendelea kutoa kipaumbele kikubwa katika Sekta ya Afya kipindi cha mwaka mmoja tangu kuingia madarakani ambapo jumla ya shilingi Bilioni 891.5 zimetolewa kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo chini ya usimamizi wa moja kwa moja wa Wizara ya Afya.
# Miradi ya maendeleo ya kipaumbele iliyotekelezwa moja kwa moja na Wizara ya Afya ni pamoja na;
# Ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya kutolea huduma za afya katika Hospitali za Rufaa za Mikoa, Hospitali za Rufaa za Kanda, Hospitali Maalumu na Hospitali ya Taifa Muhimbili ambapo kiasi cha shilingi bilioni 90.4 zilitolewa.
# Ukarabati wa majengo ya kufundishia katika Vituo vya Afya ambapo kiasi cha shilingi bilioni 6.3 kimetolewa. Ununuzi na usambazaji wa dawa, vifaa, vifaa tiba na vitendanishi, ambapo jumla ya shilingi Bil. 333 zimetolewa.
# Kununua Vifaa Tiba vya Uchunguzi, kuimarisha huduma za upatikanaji wa damu salama.
# Kugharamia posho za wanafunzi watarajali (Intens) wa Udaktari, Udaktari wa Meno na wataalam wa Afya Shirikishi kiasi cha shilingi Bil. 49.9 zimetolewa.
# Kulipia gharama za masomo kwa ajili ya Madaktari bingwa (specialists) na Madaktari bingwa Bobezi (Super Specialists) ndani na nje ya nchi ambapo jumla ya shilingi Bil. 4.4 zimetolewa.
# Kuimarisha mapambano dhidi ya UKIMWI, Kifua Kikuu na Malaria (ikiwemo ununuzi wa dawa ARVs, Dawa za Malaria na Vitendanishi) ambapo kiasi cha shilingi bilioni 117 kimetolewa.
MATOKEO YALIYOPATIKANA
# Kuboreshwa kwa miundombinu ya kutolea Huduma za Afya.
# Kuimarika kwa Upatikanaji wa Huduma za Matibabu ya Ubingwa Bobezi (Super specialized) nchini.
#Kuimarika upatikanaji wa dawa, vifaa, vifaa Tiba, vitendanishi katika vituo vya umma vya kutolea huduma za afya.
#Kuimarika kwa Huduma za Afya ya Uzazi, Mama na Mtoto.
#Kuendelea kupunguza Idadi ya Wagonjwa na Vifo vinavyotokana na UKIMWI, Malaria na Kifua Kikuu (TB)...
Haya hapa ni baadhi ya mambo muhimu ambayo ameyazungumza ambayo yamekuwa na faida kubwa kwa raia wa kawaida.
#Serikali imeendelea kutoa kipaumbele kikubwa katika Sekta ya Afya kipindi cha mwaka mmoja tangu kuingia madarakani ambapo jumla ya shilingi Bilioni 891.5 zimetolewa kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo chini ya usimamizi wa moja kwa moja wa Wizara ya Afya.
# Miradi ya maendeleo ya kipaumbele iliyotekelezwa moja kwa moja na Wizara ya Afya ni pamoja na;
# Ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya kutolea huduma za afya katika Hospitali za Rufaa za Mikoa, Hospitali za Rufaa za Kanda, Hospitali Maalumu na Hospitali ya Taifa Muhimbili ambapo kiasi cha shilingi bilioni 90.4 zilitolewa.
# Ukarabati wa majengo ya kufundishia katika Vituo vya Afya ambapo kiasi cha shilingi bilioni 6.3 kimetolewa. Ununuzi na usambazaji wa dawa, vifaa, vifaa tiba na vitendanishi, ambapo jumla ya shilingi Bil. 333 zimetolewa.
# Kununua Vifaa Tiba vya Uchunguzi, kuimarisha huduma za upatikanaji wa damu salama.
# Kugharamia posho za wanafunzi watarajali (Intens) wa Udaktari, Udaktari wa Meno na wataalam wa Afya Shirikishi kiasi cha shilingi Bil. 49.9 zimetolewa.
# Kulipia gharama za masomo kwa ajili ya Madaktari bingwa (specialists) na Madaktari bingwa Bobezi (Super Specialists) ndani na nje ya nchi ambapo jumla ya shilingi Bil. 4.4 zimetolewa.
# Kuimarisha mapambano dhidi ya UKIMWI, Kifua Kikuu na Malaria (ikiwemo ununuzi wa dawa ARVs, Dawa za Malaria na Vitendanishi) ambapo kiasi cha shilingi bilioni 117 kimetolewa.
MATOKEO YALIYOPATIKANA
# Kuboreshwa kwa miundombinu ya kutolea Huduma za Afya.
# Kuimarika kwa Upatikanaji wa Huduma za Matibabu ya Ubingwa Bobezi (Super specialized) nchini.
#Kuimarika upatikanaji wa dawa, vifaa, vifaa Tiba, vitendanishi katika vituo vya umma vya kutolea huduma za afya.
#Kuimarika kwa Huduma za Afya ya Uzazi, Mama na Mtoto.
#Kuendelea kupunguza Idadi ya Wagonjwa na Vifo vinavyotokana na UKIMWI, Malaria na Kifua Kikuu (TB)...