Jumanne Mwita
JF-Expert Member
- Nov 18, 2014
- 530
- 1,446
Habari wanajamvi,
Natumaini mu wazima na mnaendelea vyema na shughuli zenu za kila siku. Nimekuja kwenu leo nikiwa na swali ambalo ningeomba msaada wenu kulijibu. Katika kutafuta bima ya afya ambayo itakuwa na gharama nafuu na huduma bora, nimepata majina ya mashirika kadhaa yanayotoa huduma za bima ya afya Tanzania. Haya ni baadhi ya mashirika:
Nipo kuchanganua Bima yenye gharama nafuu, hasa kwa haya mashirika ya Bima kwa mwaka kwa mtu mmoja au kwa mtoto bima zao zikoje najua NHIF imepandisha gharama kwa haya mashirika mengine nayo hakuna yenye nafuu kuzidi NHIF?
Ningeomba msaada wenu katika kufahamu ni shirika gani kati ya haya linaweza kuwa na gharama nafuu na kutoa huduma nzuri. Kama una uzoefu na mojawapo ya mashirika haya au unajua lolote kuhusu vifurushi vyao vya bima ya afya, tafadhali shiriki maoni yako.
Pia, ningependa kujua:
1. Je, kuna kifurushi chochote cha bima ya afya kutoka mojawapo ya mashirika haya ambacho kina gharama nafuu kwa mtu mmoja au wawili kwa mwaka?
2. Kati ya mashirika haya, ni lipi lina huduma bora zaidi kwa wateja wake?
3. Kuna shirika lingine lolote ambalo unalipendekeza kwa gharama na huduma bora?
Maoni yako ni muhimu yanaweza kusaidia hata ambae hakuwa na nia ya kuhitaji Bima akashawishika hapa baada ya kusoma maoni hapa.
Karibuni kwa majadiliano!
Natumaini mu wazima na mnaendelea vyema na shughuli zenu za kila siku. Nimekuja kwenu leo nikiwa na swali ambalo ningeomba msaada wenu kulijibu. Katika kutafuta bima ya afya ambayo itakuwa na gharama nafuu na huduma bora, nimepata majina ya mashirika kadhaa yanayotoa huduma za bima ya afya Tanzania. Haya ni baadhi ya mashirika:
- NHIF (National Health Insurance Fund)
- AAR Insurance Tanzania
- Jubilee Insurance
- Strategis Insurance Tanzania
- Britam Insurance Tanzania
- First Assurance Tanzania
- UAP Insurance Tanzania
- Sanlam Life Insurance Tanzania
- Alliance Insurance Corporation Ltd
- Phoenix of Tanzania Assurance Company Ltd
- Metropolitan Tanzania Insurance Company
Nipo kuchanganua Bima yenye gharama nafuu, hasa kwa haya mashirika ya Bima kwa mwaka kwa mtu mmoja au kwa mtoto bima zao zikoje najua NHIF imepandisha gharama kwa haya mashirika mengine nayo hakuna yenye nafuu kuzidi NHIF?
Ningeomba msaada wenu katika kufahamu ni shirika gani kati ya haya linaweza kuwa na gharama nafuu na kutoa huduma nzuri. Kama una uzoefu na mojawapo ya mashirika haya au unajua lolote kuhusu vifurushi vyao vya bima ya afya, tafadhali shiriki maoni yako.
Pia, ningependa kujua:
1. Je, kuna kifurushi chochote cha bima ya afya kutoka mojawapo ya mashirika haya ambacho kina gharama nafuu kwa mtu mmoja au wawili kwa mwaka?
2. Kati ya mashirika haya, ni lipi lina huduma bora zaidi kwa wateja wake?
3. Kuna shirika lingine lolote ambalo unalipendekeza kwa gharama na huduma bora?
Maoni yako ni muhimu yanaweza kusaidia hata ambae hakuwa na nia ya kuhitaji Bima akashawishika hapa baada ya kusoma maoni hapa.
Karibuni kwa majadiliano!