Shirika la Bima la Taifa (NIC) kuna tatizo gani? Mbona hamlipi fedha za watu kwa wakati?

Shirika la Bima la Taifa (NIC) kuna tatizo gani? Mbona hamlipi fedha za watu kwa wakati?

The Palm Tree

JF-Expert Member
Joined
Apr 13, 2013
Posts
7,951
Reaction score
12,541
Mimi ni mfanyakazi wa taasisi X ya umma hapa Shinyanga...

Nilichukua bima ya elimu (Education Provider With Profit) kwa ajili ya ada ya watoto wangu hapa tawi la NIC - Shinyanga yenye thamani ya Tshs 7,500,000 kwa makato ya Tshs. 62,500 kila mwezi kwa miaka kumi (10) tangu mwaka 2010...

Bima yangu imeiva tangu mwezi Oktoba mwaka huu 2020 na nimeshafuata taratibu zote kwa kuomba na kujaza papers zote zinazotakiwa ili kulipwa fedha zangu...

Surprisingly, huu sasa unaenda mwezi wa tatu silipwi pesa yangu. Kila nikifika kwenye ofisi zenu (NIC - Shinyanga) ni maneno tu badala ya kupewa fedha...

Kila mara mnasema faili langu bado liko makao makuu ya NIC - DSM, halijarudi ili kutoa "go ahead" ya kuandaliwa kwa malipo yangu...

That doesn't concern me please...!!

Basically haya ni majibu yenye maelezo ya ubabaishaji tu na hayana ukweli wowote...

Hivi ktk zama hizi za maendeleo ya teknolojia ya mawasiliano na habari inawezekana vipi faili litembee lenyewe toka Shinyanga hadi DSM kwa miezi zaidi ya miwili pasipo kurudi....???

NIC - Shinyanga, tafadhali nikija safari hii naomba nikute fedha zangu na sitaki tuendelee kudanganyana kama watoto waliozaliwa Jana...

Ama la tuambieni mna matatizo gani?. Je, fedha zetu mliwapa CCM kufanyia kampeni za uchaguzi za mwaka huu kama mifuko ya hifadhi yq jamii (Provident Funds) walivyofanya na sasa wanawasumbua wazee wetu wastaafu kwa kutolipa mafao yao...?

NIC mnajichafua sana na kuharibu biashara yenu kwa sababu ya urasimu huu usio kuwa na ulazima wowote wa kushindwa kulipa fedha za wateja wenu wanaostahili kwa wakati...

Nilikuwa na mpango nikipata fedha hii, nikate bima nyingine lakini kwa usumbufu huu, bora niwekeze kihela changu ktk biashara nyingine....
 
Wapeleke mahakamani na udai haki yako pamoja na fidia ya kuvunja makubaliano baina yako na wao (Breach Of Contract).

Ukishinda case yako na wakizingua tena kukulipa omba "ATTACHMENT" ya kukamata jengo lao au gari la mkurugenzi uuze.
Akifanya hivyo chap chap anafanyiwa mpango wa uhujumu uchumi.
 
Akifanya hivyo chap chap anafanyiwa mpango wa uhujumu uchumi.

Na hata kutekwa juu. Hiyo hela imeingizwa kwenye project vita vya kiuchumi. Vita hii hela yoyote inachukuliwa ili kujenga nchi na sifa atapata mtu mwingine.
 
Wapeleke mahakamani na udai haki yako pamoja na fidia ya kuvunja makubaliano baina yako na wao (Breach Of Contract).

Ukishinda case yako na wakizingua tena kukulipa omba "ATTACHMENT" ya kukamata jengo lao au gari la mkurugenzi uuze.
I think the law does not allow to attach a government property. I stand to be collected.
 
Inaonekana bado upo ktk historia ndugu yetu ...kwanza kabisa NIC Haina product ya Elimu Kama hiyo uliyoitaja.....umesemamiaka 10

Kwa utaratibu bima ya elimu huwa kwa kipindi cha miaka mitano yaani miezi 60.
ambapo kwa kipindi cha kuanzia Januari mpaka Disemba hakuna bima ya elimu iliyofikia mwisho yenye kima cha milioni 7 zote ambazo tumeanda zinaishia milioni 5 kushuka chini kwa kumbukumbu bima ya kiwango cha juu ilikuwa ya milioni 6 ambayo mteja alikuwa akichangia shilingi laki 105,338 ambaye tayari amekwishalipwa.

Bima ya elimu ya kima cha milioni 7 makato yake kwa mwezi ni 121,800 kwa miezi 60 yaani miaka 5

Nimekupa data hizi ili kubainisha uongo wa mwandishi ambae anaonekana dhahiri Ana Nia ovu na Shirika.
 
Mimi ninae bima na NIC ya 13900 kwa 10yrs itakuwa matured 2023
Naendelea kusubiri niende nkawaashie moto
LA sivyo ntakunya of is in wajue watu ni vichaa
 
Inaonekana bado upo ktk historia ndugu yetu ...kwanza kabisa NIC Haina product ya Elimu Kama hiyo uliyoitaja.....umesemamiaka 10

Kwa utaratibu bima ya elimu huwa kwa kipindi cha mitano yaani miezi 60.
ambapo kwa kipindi cha kuanzia Januari mpaka Disemba hakuna bima ya elimu iliyofikia mwisho yenye kima cha milioni 7 zote ambazo tumeanda zinaishia milioni 5 kushuka chini kwa kumbukumbu bima ya kiwango cha juu ilikuwa ya milioni 6 ambayo mteja alikuwa akichangia shilingi laki 105,338 ambaye tayari amekwishalipwa.

Bima ya elimu ya kima cha milioni 7 makato yake kwa mwezi ni 121,800 kwa miezi 60 yaani miaka 5

Nimekupa data hizi ili kubainisha uongo wa mwandishi ambae anaonekana dhahiri Ana Nia ovu na Shirika.
 
Mimi ni mfanyakazi wa taasisi X ya umma hapa Shinyanga...

Nilichukua bima ya elimu (Education Provider With Profit) kwa ajili ya ada ya watoto wangu hapa tawi la NIC - Shinyanga yenye thamani ya Tshs 7,500,000 kwa makato ya Tshs. 62,500 kila mwezi kwa miaka kumi (10) tangu mwaka 2010...

Bima yangu imeiva tangu mwezi Oktoba mwaka huu 2020 na nimeshafuata taratibu zote kwa kuomba na kujaza papers zote zinazotakiwa ili kulipwa fedha zangu...

Surprisingly, huu sasa unaenda mwezi wa tatu silipwi pesa yangu. Kila nikifika kwenye ofisi zenu (NIC - Shinyanga) ni maneno tu badala ya kupewa fedha...

Kila mara mnasema faili langu bado liko makao makuu ya NIC - DSM, halijarudi ili kutoa "go ahead" ya kuandaliwa kwa malipo yangu...

That doesn't concern me please...!!

Basically haya ni majibu yenye maelezo ya ubabaishaji tu na hayana ukweli wowote...

Hivi ktk zama hizi za maendeleo ya teknolojia ya mawasiliano na habari inawezekana vipi faili litembee lenyewe toka Shinyanga hadi DSM kwa miezi zaidi ya miwili pasipo kurudi....???

NIC - Shinyanga, tafadhali nikija safari hii naomba nikute fedha zangu na sitaki tuendelee kudanganyana kama watoto waliozaliwa Jana...

Ama la tuambieni mna matatizo gani?. Je, fedha zetu mliwapa CCM kufanyia kampeni za uchaguzi za mwaka huu kama mifuko ya hifadhi yq jamii (Provident Funds) walivyofanya na sasa wanawasumbua wazee wetu wastaafu kwa kutolipa mafao yao...?

NIC mnajichafua sana na kuharibu biashara yenu kwa sababu ya urasimu huu usio kuwa na ulazima wowote wa kushindwa kulipa fedha za wateja wenu wanaostahili kwa wakati...

Nilikuwa na mpango nikipata fedha hii, nikate bima nyingine lakini kwa usumbufu huu, bora niwekeze kihela changu ktk biashara nyingine....
Kuna sheria za bima ilitungwa kwa ajili hizo hizo za watu kucheleweshewa malipo.

Tafuta wakili mzuri mpige hela unazodai na za usumbufu na za gharana za kesi.
Fanya kama wazungu wanavyotufanyia ICSID.

Tuwache kulalamika mitandaoni wakati nchi ina sheria.
 
Ingia nao makubaliqno ya kuwapatia 30% faster utalipwa. Vinginevyo sahau
 
Back
Top Bottom