Shirika la Reli Tanzania wamepata wapi pesa za kununua Magari ya kifahari ilhali hawaliingizii taifa faida yoyote zaidi ya kutoa huduma?

Shirika la Reli Tanzania wamepata wapi pesa za kununua Magari ya kifahari ilhali hawaliingizii taifa faida yoyote zaidi ya kutoa huduma?

Mkuu ngoja nikuambie neno, ili usilete kuchongea watu bila sababu. NI kwamba katika sheria ya manunuzi ya serikali inasema kabisa magari gani yanapaswa kununuliwa, na huwa ni hizo Landcruiser na Pick up double cabin. Wakati fulani ilikuwa ni Land Rover Defender 110. Kwa hiyo hawa watu hawajiamulii, bali ni sheria inawapeleka kununua hayo magari. Bila hiyo sheria ungekuta wananunua Range Rover, Lexus, Jeep, BMW X5, Mercedes GLS nk.

Kuna wakati mradi wa EU hapa nchini walipata matatizo kwa kuwa wao walitaka kuagiza magari ya Ulaya, lakini sheria ikawa inawabana kununua magari ya Japan kulingana na sheria ya manunuzi ya Tanzania. EU wakaona kama wanalazimishwa kuwa promote Wajapan wakati fedha ni za Ulaya.

Kwa hiyo usimlaumu mtu wa serikalini au shirika la umma kununua hizo V8
Kwa kuwa ni Sheria basi wanunue tu magari ya kifahali? Hii ni alarm ya kuwa watanzania hatutaki Sheria za kipumbavu wakati nchi Haina uchumi.
 
Kwa kuwa ni Sheria basi wanunue tu magari ya kifahali? Hii ni alarm ya kuwa watanzania hatutaki Sheria za kipumbavu wakati nchi Haina uchumi.
Labda sheria ndio ina matatizo. Lakini lengo la sheria ni kwamba hizo Landcuiser, Nissan Patrol ndio zilionekana zinafaa kwa barabara za Tanzania, na kuweza kufikisha viongozi hadi vijijini.

Kwa mfano, sidhani kama sheria inasema ununue V6 au V8, hivyo unakuta mkurugenzi anajipiga kwenye V8, kwa kuwa V8 ni ngoma nzito zaidi ya V6.
 
Labda sheria ndio ina matatizo. Lakini lengo la sheria ni kwamba hizo Landcuiser, Nissan Patrol ndio zilionekana zinafaa kwa barabara za Tanzania, na kuweza kufikisha viongozi hadi vijijini.

Kwa mfano, sidhani kama sheria inasema ununue V6 au V8, hivyo unakuta mkurugenzi anajipiga kwenye V8, kwa kuwa V8 ni ngoma nzito zaidi ya V6.
Haya magari ukiyaona Kwa sasa nafikiri hakuna shirika Wala taasisi ya umma inayafikia Kwa idadi.
 
Kumbuka TRC nayo ni kubwa ina vitengo vingi na maofisa wanaostahili hizo gari kulingana na Tume ya Utumishi. Hawanunui ovyo kwa kupenda
Sasa tukifanya hivyo basi shirika la umeme TANESCO lingeongoza Kwa magari. Hawa TRC hawana ofisi wilayani na baadhi ya mikoa hawana vitengo inakuwaje wamemonopolize transport Kwa wingi hivi?
 
Mkuu hawa watu siyo Dar pekee Bali hata mikoani huko wametapakaa.
TRC hawawezi kuwa mikoani kama Iringa, Mbeya ambako hakuna reli na huduma zao za barabara walisimamisha. Lakini Dodoma, Morogoro, Tabora nk lazima utakuta Land Cruiser V8 za TRC na namba zao RAC
 
TRC hawawezi kuwa mikoani kama Iringa, Mbeya ambako hakuna reli na huduma zao za barabara walisimamisha. Lakini Dodoma, Morogoro, Tabora nk lazima utakuta Land Cruiser V8 za TRC na namba zao RAC
Mkuu tuendelee kulipa TOZO?
 
  • TOZO!
  • Kwenye kitabu The Animal Farm kuku wanahimizwa kutaga ili nguruwe wale na kumenepeana
 
Back
Top Bottom