Uchaguzi 2020 Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) limesikitishwa na kitendo uongozi wa CHADEMA kuwakemea na kuwafukuza watangazaji wake

Uchaguzi 2020 Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) limesikitishwa na kitendo uongozi wa CHADEMA kuwakemea na kuwafukuza watangazaji wake

TBC hiyo ndo adhabu mlistahili kwa kweli na sivinginevyo, mmekaa kinafiki sana
 
Hatuna haja nao kabisa hao wanafiki wakubwa sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
Watu wa ajabu sana. Lisu amezunguka mikoa zaidi ya 16 kupata wadhamini, TBC haikuona haja ya kurusha LIVE matukio, leo katika mazingira ya kusuasua imefukuzwa, watu wanahangaika. Watu wanaangalia wanachokipenda.
 
TBC imeanza lini mahaba na CHADEMA. Unafiq mbaya aana alichofanya Mbowe ni stahili kwa TBC.
 
TBC inapenda kutimiza wajibu wake wa kisheria na imekuwa tayari, siku zote, kufanya kazi na vyama vyote vya siasa bila ubaguzi...haaa haaa
 


Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) Limesikitishwa na kitendo uongozi wa CHADEMA kuwakemea na kuwafukuza watangazaji wake katika mkutano wao wa kuzindua Kampeni za Mgombea wao wa Urais katika viwanja vya Zakheim, Mbagala Jijini Dar es Salaam, jioni hii.

TBC1 na TBC Taifa kama chaneli za umma zilikuwa zinarusha matangazo ya moja kwa moja kwenye uzinduzi huo kwa mujibu wa sheria na miongozo ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi.

Hata hivyo, kwa mujibu wa mwongozo wa Tume wa mwaka 2020, (kifungu e na j), kanuni za maadili ya tasnia ya habari; vyombo vya utangazaji vya umma pia vinao wajibu wa kuhakikisha maudhui yanayorushwa hewani yanazingatia maadili ya taaluma na ya jamii.

Kitendo cha uongozi wa CHADEMA kutangaza kuwafukuza watangazaji wa TBC si cha kiungwana na kinahatarisha usalama wa watendaji hao na vifaa vyao.

Pamoja na kwamba TBC inapanga kutoa taarifa rasmi Polisi na kwenye Tume ya Taifa ya Uchaguzi, kwa sasa inasitisha rasmi kurusha matangazo ya CHADEMA hadi hapo watendaji wake watakapohakikishiwa usalama.

TBC inapenda kutimiza wajibu wake wa kisheria na imekuwa tayari, siku zote, kufanya kazi na vyama vyote vya siasa bila ubaguzi.

Kwa mara ya kwanza TBCCM inasikia uchungu na maumivu mpaka imelia😭😭😭👷👷👷💩💩
 
Naona mbowe safari hii kaja kivingine, wakati wanafunga kampeni pale jangwani 2015 TBC walipokata matangazo, mbowe akasema nimesikia TBC wamekata matangazo hatuongei mpaka warudi hewani, kalitawala kaukimya kwa muda TBC waliporudi hewani watu walishangilia na nyundo zikaendelea kama kawaida,
Hii ya kuwafukuza kabisa hatari.
 
Mngekuwa na morali hii ya kutaka mabadiliko kwenye mfumo wa elimu ingekuwa ni uzalendo uliotukuka.
Ficha upumbavu wako na ionyeshe hekima yako.....

Mifumo yote ya kishenzi ikiwemo elimu inayosimamiwa na fisiemu itabadilika kwa kuwaondoa ccm kwa sanduku la kura na si vinginevyo

Ila kwasababu kuna masikini wa akili wengi kama wewe bado mnaunga juhudi za ccm yenye mfumo huo mbovu unaousemea wa elimu acha tuendelee kuisoma namba
 
We endelea kujiongopea hivi unafahamu bila ya hayo madaraja safari ya nusu 30 saa huku kijiji inaweza kuchukua masaa 3 kwa usafiri wetu; kama mtu an akimbizwa hospitali uwepo wa daraja linakuwa swala kufa na kupona. Halafu we unaona daraja halina tija, akili zenu zinawatosha wenyewe.
Mwambie uyo Mkuu naona anajisaulisha


Sent from my TECNO-C8 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom