Shirikisho la mpira Afrika (CAF) limekaa kizamani sana

Shirikisho la mpira Afrika (CAF) limekaa kizamani sana

Right eye

JF-Expert Member
Joined
Sep 6, 2022
Posts
1,149
Reaction score
1,994
Habari,

Hili shirikisho letu la mpira Africa limekaa kizamani sana kwa kuendelea kutukuza na kukumbatia kanuni zisizo na faida Wala manufaa kwa mpira wetu.

Hili la fainali kuchezwa nyumbani na ugenini ni jambo la hovyo lisilokua na faida chanya kwa mpira wetu.

Sioni mantiki ya kanuni hii ya kuchezwa kwa fainali nyumbani na ugenini zaidi ya kuona kuzipa timu flani za mataifa ya kiarabu kutumia mbinu chafu katika kutafuta ushindi kwa wapinzani wao.

Swala jingine ni hili la goli la ugenini nalo naona kama ni upuuzi tu kwa mpira wetu hizi ni kanuni zilizopitwa na wakati na hazifai kwa mpira wa kisasa.

Ushauri wangu kwa CAF waondoe hizi kanuni mbili za fainali kuchezwa nyumbani na ugenini na hii ya goli la ugenini,Badala yake fainali iwe moja na ichezwe kwenye uwanja ambao ni mgeni kwa timu zote mbili. Na hili la goli la ugenini lisiwepo badala yake fainali ichezwe kwa dakika tisini kama hakuna matokeo ziongezwe dakika thelathini na endapo kutakua hakuna matokea pia basi mchezo uamuliwe kwa mikwaju ya penati.
 
Swala jingine ni hili la goli la ugenini nalo naona kama ni upuuzi tu kwa mpira wetu hizi ni kanuni zilizopitwa na wakati na hazifai kwa mpira wa kisasa.
Goli la ugenini ndilo lililoiondoa Simba mara mbili katika michuano; dhidi ya Jwaneng Galaxy na dhidi ya UD Songo. Mimi naona hizi kanuni zinafaa maana zilikuwako tangu zamani na zilishatumika sana. Hakuna haja ya kuiga Ulaya
 
Habari.
Hili shirikisho letu la mpira Africa limekaa kizamani sana kwa kuendelea kutukuza na kukumbatia kanuni zisizo na faida Wala manufaa kwa mpira wetu...
Naheshimu Msimamo wako mkuu,

Lakini nafikiri mwaka jana walifanya hiko kitu wakabadilisha tena.

Sababu ni kuwa nchi zetu Africa ni Maskini. Imagine hata fainal ingechezewa Africa Kusini ama Ghana, je ni watanzania wangapi wangeenda Ghana? Huoni kama nchi iliyo Tajiri kidogo itapata advantage ya kuwa na mashabiki wengi kuliko wenzao?

Na hiyo itasababisha mchezo ukae upande mmoja.

Kuhusu goli la ugenini,

Uko sahihi pia tukiangalia modern football, lakini pia Mpira wa Africa yetu bado una unyumbani na ugenini sana kwahyo kutoa credit kwa Timu ilopata ushindi mnono au magoli mengi ikiwa ugenini ni jambo zuri.

Hayo ni mawazo ya walioamua kurudisha system ya zamani.

Embu tafakari na hzo point then uzione zimekaaje mkuu.
 
Yani jana wydad kapata goli moja tu mashabiki wake walikuwa wanashangilia hatari halafu timu inayoongoza mashabiki wake wamepoa. Shida ni goli la ugenini walilopata wapinzani wao wydad anawezabeba kombe hata kwa ushindi wa bao moja kwa sifuri.
 
Umeongea vizuri mkuu lakini wakiwa wote ugenini haiwezi kutengeneza mianya mikubwa ya kutafuta matokeo nje wa uwanja kama inavyofanyika hivi Sasa.

Kwasasa kwa kanuni hizi naona faida zaidi kwa nchi ambazo tayari zimeshajikita zaidi kwenye mbinu chafu.
 
Umeongea vizuri mkuu lakini wakiwa wote ugenini haiwezi kutengeneza mianya mikubwa ya kutafuta matokeo nje wa uwanja kama inavyofanyika hivi Sasa.

Kwasasa kwa kanuni hizi naona faida zaidi kwa nchi ambazo tayari zimeshajikita zaidi kwenye mbinu chafu.
Hii inaukweli wake, tumeona hata mechi ya watani juzi (Yanga)

Jukumu la kubadilisha ni letu, kwahyo wenye authority hiyo wanahitaji kupata mawazo mengi kama haya
 
Caf wakae chini kwenye kigoda waanze kifikiri upya malalamiko yamekuwa mengi..wanakaa kwenye viti vya kunesa na kuzunguruka kama boss wa kampuni hawawezi kuona hayo.
 
Caf wakae chini kwenye kigoda waanze kifikiri upya malalamiko yamekuwa mengi..wanakaa kwenye viti vya kunesa na kuzunguruka kama boss wa kampuni hawawezi kuona hayo.
Kwa mwendo huu mashindano haya yatakosa msisimko kwa mashabiki wa mpira kwa sababu siku zote tutaendelea kuona nchi za kiarabu kuendelea kuchukua makombe wakati uwezo wao ni wa kawaida,Kinachowabeba ni mbinu chafu kutokana na udhaifu wa kanuni za caf.
 
mmedekezwa sana na TFF kila mkitaka kitu mnapewa tulieni dawa iwaingie hizi kanuni zilikuwepo muda mrefu na hakuna aliyewahi kulalamika.

Wenzenu wanacheza kwa malengo kwani walishamaliza fainali Dar
 
Goli la ugenini ndilo lililoiondoa Simba mara mbili katika michuano; dhidi ya Jwaneng Galaxy na dhidi ya UD Songo. Mimi naona hizi kanuni zinafaa maana zilikuwako tangu zamani na zilishatumika sana. Hakuna haja ya kuiga Ulaya
Baada ya kukosa, kwanini Walikubali kufungwa nyumbani.tuanzie hapa.
 
Kwa mwendo huu mashindano haya yatakosa msisimko kwa mashabiki wa mpira kwa sababu siku zote tutaendelea kuona nchi za kiarabu kuendelea kuchukua makombe wakati uwezo wao ni wa kawaida,Kinachowabeba ni mbinu chafu kutokana na udhaifu wa kanuni za caf.

wetu weusi kwenye ubora wenu, MALALAMIKO
 
Habari,

Hili shirikisho letu la mpira Africa limekaa kizamani sana kwa kuendelea kutukuza na kukumbatia kanuni zisizo na faida Wala manufaa kwa mpira wetu.

Hili la fainali kuchezwa nyumbani na ugenini ni jambo la hovyo lisilokua na faida chanya kwa mpira wetu.

Sioni mantiki ya kanuni hii ya kuchezwa kwa fainali nyumbani na ugenini zaidi ya kuona kuzipa timu flani za mataifa ya kiarabu kutumia mbinu chafu katika kutafuta ushindi kwa wapinzani wao.

Swala jingine ni hili la goli la ugenini nalo naona kama ni upuuzi tu kwa mpira wetu hizi ni kanuni zilizopitwa na wakati na hazifai kwa mpira wa kisasa.

Ushauri wangu kwa CAF waondoe hizi kanuni mbili za fainali kuchezwa nyumbani na ugenini na hii ya goli la ugenini,Badala yake fainali iwe moja na ichezwe kwenye uwanja ambao ni mgeni kwa timu zote mbili. Na hili la goli la ugenini lisiwepo badala yake fainali ichezwe kwa dakika tisini kama hakuna matokeo ziongezwe dakika thelathini na endapo kutakua hakuna matokea pia basi mchezo uamuliwe kwa mikwaju ya penati.
Ulaya hawana huo upuuzi,unapewaje goli na haujafanya chochote,sawa na kupokea mshahara na haujafanya kazi,
 
Back
Top Bottom