Shuhuda aliyeshiriki kuokoa watu Kariakoo asema "Kule chini hali ni mbaya, nimeshuhudia Watu wamefukiwa na vifusi"

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Your browser is not able to display this video.
Nassor Athuman akizungumza kile alichokishuhudia baada ya kutoka eneo ambalo jengo limeanguka Kariakoo, Dar es Salaam.

Nassor amesema ameshuhudia watu 10 hadi 15 akiwa chini bila ya kuweza kuwasaidia kutokana na hali jinsi ilivyokuwa.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila anasema kufikia leo mpaka Saa 1 asubuhi na usiku mzima ni watu 5 pekee waliookolewa.

Shughuli za uokoaji bado zinaendelea huku jeshi la polisi likiimarisha ulinzi mkali katika eneo wakiongozwa na Kamanda wa Polisi kanda Maalum ya Dar es Salaam, Muliro Jumanne Muliro.

Chanzo: Crown FM
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…