Ila mara nyingi mimi naona pia inategemea na utayari wa wewe mwanafunzi, maana waweza kwenda katika shule nzuri ila kama huna nia ya dhati ya kusoma unatoka na matokeo mabovu japo pia kwa kiasi fulani shule nazo zinachangia.
Ninasema hivi kutokana na experience ambayo nina rafiki yangu alichaguliwa shule moja hivi ya serikali na hiyo shule kiukweli sio nzuri yani haina walimu wa kutosha na mambo mengine kama ujuavyo hizi shule za serikali tena shule yenyewe ipo mkoa lakini kwa juhudi binafsi za huyu bwana alitoka na Div 1 nzuri tu na sasa hivi yupo chuo.
Hivyo ni sawa pia yani (shule+juhudi binafsi= matokeo mazuri)