Young Warlock
JF-Expert Member
- Dec 29, 2013
- 328
- 111
ebu edit hapo.....tabora boys ndo special kongwe asee
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kwa uwelewa wangu mdogo niliofundishwa ni kwamba mjadala huwa unafundisha endapo wanaojadili hilo jambo wanaelewa nini maana ya optimal ignorance .Ila nilichogundua ni kwamba wewe uwelewa wako ni mkubwa zaidi yetu wote tunaojadili na hakuna anayejua zaidi yako . Hoja unaikimbia unaanza kukosoa makosa madogo madogo ya kiuandishi (kwa mtazamo wangu). Unanikumbusha kipindi kile tupo o-level kwenye debate (anaweza akasimama mtu na kumwambia mwongeaji/mtoa hoja kwa idhini ya mwenyekiti "hujachomekea shati lako vizuri")"Coming president wa tz" maana yake ndo nini?
shule za wenye vipaji maalumu zipo hata nchi zingne kama usa.
HADI university zipo kwa mfano qualification za kuingia stanford univ.havard,m.i.t ni za juu zaidi ya vyuo vingine.lakini nao bado wana consider academic qualification
Kwa hiyo ni "vipaji maalum" kwenye masomo tu?
Is this fair?
Nimebahatika kusoma miaka 6 huko, MZUMBE o level,then Kibaha A Level,nilipo htm miaka kadhaa ilopita.
Wanafunzi wanaachwa kama kuku wa kienyeji,sylabi haziwi covered,then wanasoma kupita kiasi [hata wengine huchizika]
Walimu wenye vipaji wapo aisee!
Namkumbuka Wibonele Mz [RIP] na Sir Mgina KBH,LOL!
Mkuu,T.Boys imepewa hadhi ya u special miaka ya 2000's!
Duu...kweli we lengo lako ni kupotosha Kwa makusudi..mwl Nyerere kasoma pale na ilikua tayari ni special
Wale ni shule ambazo zilibahatika kuwapata wasomaji na kukesha na wazee wa kuklemu wa wa shule za msingi so haimanishi ni bright kiivyo ndio maana kuna mazezeta tulioenda jangwani na zanaki na shule zingine tunakula maisha kushinda wa😵VER
Hata we nadhani ungetamani kua na cv yenye tabora girls ama kilakara bt mafuta yalikata So unaumia
Mkuu kabla ya kujibu maswali yako labda naomba tuwekane sawa kwenye msamiati huu wa "Vipaji Maalumu" au "Vipaji Maalumu Kiakili".
Elimu ya sekondari ya Tanzania kwa nyakati nilizokuwa nasoma ilikuwa na shule za aina nne zenye kutoa mafunzo ya elimu hiyo.
1. Shule za Vipaji Maalumu
2. Shule za Mafunzo ya Ufundi
3. Shule za Bweni zisizo na Umaalumu au Mafunzo ya Ufundi
4. Shule za Kutwa
Namna ya kudahiliwa au kujiunga na shule hizi ilitegemea na viwango vya ufaulu wa wanafunzi, iwe kutoka elimu ya msingi kwenda sekondari au kutoka "ordinary level" kwenda "advanced level".
Binafsi nimefanikiwa kusoma kwa miaka sita katika shule hizi za vipaji maalumu, na wakati ule namaliza darasa la saba tulikuwa tunatahiniwa masomo matatu tu nayo ni Hisabati, Maarifa na Lugha ambapo kila somo lilikuwa linapewa alama hamsini.
Ili uweze kujiunga na shule za vipaji ilikuwa unatakiwa upate jumla ya alama kati ya 145 hadi 150.
Kwa baadhi ya mikoa ambayo viwango vya elimu ya msingi vilikuwa duni, wanafunzi kutoka mikoa hiyo walipunguziwa alama kiasi wenye ufaulu wa alama 138 waliweza kupata nafasi pia.
Kwa wale waliotakiwa kujiunga na shule za ufundi ufaulu wa somo la Hisabati ulizingatiwa zaidi, wanafunzi wa shule hizo wengi wao walikuwa na uwezo mkubwa sana wa kukokotoa hisabati.
Wale ni shule ambazo zilibahatika kuwapata wasomaji na kukesha na wazee wa kuklemu wa wa shule za msingi so haimanishi ni bright kiivyo ndio maana kuna mazezeta tulioenda jangwani na zanaki na shule zingine tunakula maisha kushinda wa😵VER
Kwa hiyo wewe unabisha au?
Sibishi mkuu,nimehoji tubadilishane mawazo!