Shule ziwe na "madarasa kando" kwa ajili ya Wanafunzi Wabunifu

Shule ziwe na "madarasa kando" kwa ajili ya Wanafunzi Wabunifu

May Day

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2018
Posts
6,311
Reaction score
9,027
Dunia inaenda kasi sana na hakuna wa kumsubiri mwingine eti ndio tuende sawa.

Ni dhahiri kuwa Mataifa yaliyoshika hatamu za dunia hii wao wamewekeza sana kwenye sayansi na teknolojia, gunduzi mbalimbali zinazofanywa na Wananchi wao ndio zinazogeuzwa bidhaa na wengine tuliobaki tunakuwa Wateja.

Hakuna kinachokuja kama zawadi bila mikakati madhubuti, hivyo nasi Tanzania tujiulize ni nini mchango wetu kwenye hili? Ni nini tunafanya kukuza na kuwaendeleza Wabunifu wetu?

Nadhani ipo haja ya kuanza kuwatambua wale Wanafunzi wote wanaoonesha uwezo wa kubuni ili walau mara moja kwa wiki kuwa na muda nao maalumu kwa ajili ya wao kujinafasi ikiwa ni pamoja na kuwapatia vitendea kazi (vya kuchokonoa) wangali wadogo.

Nina wasiwasi kuwa tunawapoteza Wabunifu wengi sana kwa kuwaacha tu wakimezwa na mfumo wetu huu wa elimu tuliojiwekea, yaani Mtoto anatoka nyumbani asubuhi na kushinda Darasani na kisha baadae anarudi nyumbani akiwa amechoshwa na ma theory ya "Mali empire" wanayojazwa na Walimu wao.

Kuwe na mikakati ya kuhakikisha wale ambao wataonekana na muelekeo huo basi watakuwa na fursa ya kuunda kitu chochote kile, kuanzia mpira wa makaratasi mpaka Magari ya matairi ya visoda, walau kila siku Mtoto aunde kitu.

Bila ya hivyo tutabaki kuwa Wasindikizaji tu tena waliokata tamaa hapa Duniani.
 
Kaka mimi naweza kusema nina ubunifu, maana hadi nafika darasa la 5 nilikuwa nabuni vifaa mbalimbali hasa vya electronics na automation, ila mfumo wa elimu umenisumbua sana,kaa sababu ilinibidi nisome kwa ajili ya ubunifu wangu ila mitihani pia na hii iliathiri ufaulu wangu kwa kiasi fulani japo mambo yalienda sawa;

nashukuru kwa sasa niko moja ya taasisi ya elimu ya juu nchini ila bado naona mfumo wetu ni uleule wa kukariri vitabu bila uelewa na hii ipo hadi chuo kikuu;

nategemea ndani ya miaka mitano nitakuja na kiwanda changu na shule ya ubunifu itatoka hapo,naamini nitafika pazuri;

asante kwa wazo zuri;
 
Au kama ni kurahisisha basi ofisi za Wilaya ziwe na madarasa yanayotembea (Mobile classes), au waandae hema (tent) ambapo Wanafunzi mbalimbali watakaokuwa wamependekezwa na shule zao wawe wanafika hapo ikiwezekana kila wikiend.

Tunaweza kufikiri ni gharama kufanya hivi lakini amini usiamini ni gharama zaidi kubaki kama tulivyo miaka mia moja ijayo.

Huko almashauri zetu kwenyewe kila mwaka tunapoteza mabilioni ya pesa lakini tunaona sawa, tuwekeze kwa ajili ya siku zijazo..
 
kaka mimi naweza kusema nina ubunifu,maana hadi nafika darasa la 5 nilikuwa nabuni vifaa mbalimbali hasa vya electronics na automation,ila mfumo wa elimu umenisumbua sana,kaa sababu ilinibidi nisome kwa ajili ya ubunifu wangu ila mitihani pia na hii iliathiri ufaulu wangu kwa kiasi fulani japo mambo yalienda sawa;

nashukuru kwa sasa niko moja ya taasisi ya elimu ya juu nchini ila bado naona mfumo wetu ni uleule wa kukariri vitabu bila uelewa na hii ipo hadi chuo kikuu;

nategemea ndani ya miaka mitano nitakuja na kiwanda changu na shule ya ubunifu itatoka hapo,naamini nitafika pazuri;

asante kwa wazo zuri;
Kila la kheri Mkuu.
 
Back
Top Bottom