Zanzibar 2020 Shule zote Zanzibar kufungwa kuanzia Oktoba 24 Mpaka Novemba 2 ili kupisha Uchaguzi

Zanzibar 2020 Shule zote Zanzibar kufungwa kuanzia Oktoba 24 Mpaka Novemba 2 ili kupisha Uchaguzi

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
Katibu mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Dkt Idrissa Muslim anawatangazia Walimu, Wanafunzi na Wananchi kua, Wizara itazifunga Shule zote za Zanzibar kuanzia tarehe 24/10/2020 na kufunguliwa tarehe 2/11/2020 kwa ajili ya kupisha Uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba 28 mwaka huu.

Wizara inawaomba Wazazi na Walezi kuwasimamia watoto wao kubaki nyumbani na kuendelea kudurusu masomo yao kwa kipindi chote hicho.

Chanzo: Zanzibar24.com
 
Hawa nao wanawarudisha nyuma watoto kimasomo. Znz natumai uchaguzi ni zoezi la sikumoja na hadi saa 5 usiku majibu yako mezani sasa siku zote hizo za nini kuwKosesha watoto masomo. Au ndo mpango kazi wa kukwiba kuraa
 
Ujechalism unataka uapply hapa zenji.

Safari hii afe mtu afe mmasai hatutakubali !
 
Uvccm tulitegemea mda huu muwe mshafika kilimanjaro kukabiliana na moto, Sasa huo uzalendo pori wenu ni wa kuimba mapambio na kumsifu meko tu, linapokuja suala linalohitaji uzalendo mnajificha kama mnadaiwa kodi na faza house mzaramo [emoji3][emoji3]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
24 na 25 Oct ni weekend hakuna school
Watakosa 26.
27 wanapiga kura waangalizi
28 ndio siku yenyewe
29 na 30 kuhesabu
31 na 1 Oct ni weekend sasa shida iwapi?
 
24 na 25 Oct ni weekend hakuna school
Watakosa 26.
27 wanapiga kura waangalizi
28 ndio siku yenyewe
29 na 30 kuhesabu
31 na 1 Oct ni weekend sasa shida iwapi?
Inategemea na matokeo, vinginevyo muda wa kufunga shule utaongezeka tuu.
 
Back
Top Bottom