Si ajabu tunawazika kwa heshima wale walio machukizo mbele za Mungu

Si ajabu tunawazika kwa heshima wale walio machukizo mbele za Mungu

Course Coordinator

JF-Expert Member
Joined
Jul 27, 2019
Posts
1,742
Reaction score
3,224
Wasalaam,

Nilipokuwa kidato cha tatu, mwanafunzi mwenzetu alijiua kwa kunywa vidonge 16 vya chloroquine.

Binti huyo aliyekuwa akiitwa Rebeka, alikuwa mzuri wa sura, umbo, na tabia na kwa kweli hakuna hata mtu mmoja aliyewaza kuwa mrembo huyo angeweza Kujitoa roho kikatili hivyo. Kifo chake kilizua mtafaruku mkubwa mno katika familia, lakini kubwa zaidi ni kuwa kanisa lake lilimsusa. Rebeka alikuwa Mkatoliki (RC) na kwa taratibu za kanisa hilo mtu akijiua anakuwa ameikana imani, hivyo hawezi kuzikwa Kikristo.

Ndugu zake walizunguka makanisa kadhaa kutafuta Padre wa kumzika, lakini wote walikataa. Padre mmoja mzee kwa jina la Werawera alipoambiwa tu habari za msiba huo mara moja akakubali kuongoza mazishi bila kipingamizi.

Ajabu baadhi ya waumini wakageuka kumlaumu Padre huyo kwa kukiuka taratibu za kanisa. Wakati wa ibada ya mazishi, ndipo padre huyo akatueleza sababu zilizomsukuma kuja kumzika binti huyo aliyejiua. Akasema “Mama mmoja alikuwa na mume mlevi sana. Kila siku mwanaume huyo alienda kilabuni kunywa pombe na kurudi nyumbani usiku. Kwa vile mama huyo alikuwa Mcha Mungu, hakuweza kumkimbia mumewe; bali kila siku alimuombea kwa Mungu ili abadilike na kuwa mcha Mungu kama yeye.

Lakini siku moja mumewe alipokuwa akivuka daraja kuelekea kilabuni aliteleza na kudumbukia mtoni, akafa maji. Kifo hicho kilimuumiza sana yule mama Kila siku alimlilia Mungu kwa kutosikia maombi yake, na kumuacha mumewe kufa akiwa mlevi, jambo linalothibitisha kuwa amekwenda jehanam.

Lakini siku moja wakati huyo mama amekaa peke yake akisononeka, mpita njia mmoja akamwambia, mama bado unasonononeka kwa ajili ya mumeo? Yule mama akasema ndiyo, na sisononeki kwa sababu amekufa, bali kwa sababu amekwenda jehanam, maana amekufa akiwa mlevi. Yule mtu akamwambia “Mama jiombee nafsi yako wewe, mumeo amemaliza safari yake na yuko peponi” Mama akasema HAIWEZEKANI alikuwa mlevi sana, na alikufa akienda Kutafuta pombe. Yule mtu akamwambia “ mama, alipokuwa akianguka mtoni, katikati ya daraja na maji ALITUBU dhambi zake” halafu yule mtu akatoweka. Kumbe alikuwa ni malaika mjumbe wa Mungu.

Padre akasema mara nyingine tunajipa nafasi ya Mungu na kupora haki ya kuhukumu ambayo ni Kazi ya Mungu tu. Si ajabu tunawazika kwa heshima wale walio machukizo kwa Mungu kwa sababu walifanikiwa kutuhadaa, na tunawadhihaki wale ambao mwenyezi Mungu amewapokea kwa sababu mioyo yao haikuwa na hila, au Walijaliwa KUTUBU kabla mauti haijawachukua. Ni Mungu tu ajuae KWA HIYO Kabla hujasema maneno mabaya kwa mtu aliyekufa, jiulize kama kweli una macho yanayoweza kuona SIRINI kama Mungu.

Inafaa sana KUMKEMEA VIKALI mtu yeyote anayetenda uovu wakati AKIWA HAI ili aziache njia zake mbaya. Lakini akishakufa hawezi kusikia wala kujirekebisha Hivyo hakuna haja ya kumtukana. Matusi kwa marehemu hayamuumizi yeye, bali wana familia yake ambao kimsingi hawana hatia yoyote. Mkaidi achapwe viboko akiwa hai, kwani maiti haijali hata ukali wa moto.

Kujiua sio suluhisho la kutatua matatizo yako.

UWE NA AMANI
 
Mkuu mwanzo wa habari yako nimeupenda sana kwasababu unaakisi uhalisia wa changamoto zinazojitokeza huku mitaani. Ila tangu ulipoingiza dhana ya "malaika" hapo nimeanza kupata mashaka dhidi ya mkasa wako kua ni finction.
 
Mkuu mwanzo wa habari yako nimeupenda sana kwasababu unaakisi uhalisia wa changamoto zinazojitokeza huku mitaani. Ila tangu ulipoingiza dhana ya "malaika" hapo nimeanza kupata mashaka dhidi ya mkasa wako kua ni finction
Kwaiyo wewe huamini kama malaika wap0?
 
Sheria za Kanisa zipo wazi kabisa.

Kujiua ni dhambi ya kumkufuru Roho Mtakatifu. Hakuna sababu inayoweza kuhalalisha dhambi ya kujinyonga/kujiua. Huyo Padre wako anapaswa kushtakiwa kwa Baba Askofu Liberatus (wa Jimbo lake).

Kuhusu mtu kumzika kama anastahili au hastahili tunaangalia maisha yake kama yaliakisi utayari wake wa kuuishi Ukristo. Ukizikwa Kikristu siyo ishara ya kwenda mbinguni kama ambavyo usipozikwa Kikristu siyo uthibitisho wa kwenda motoni.

Tunawazika Kikristu wale ambao walionesha kwa matendo yao kuuishi Ukristu: suala la kwamba wadhambi au siyo wadhambi siyo letu, ni la Mungu.

Kwahiyo usipotoshe hapa. Kujiua ni dhambi ya mauaji, ni dhambi ya mauti. Kujinyonga ni kumkufuru Roho Mtakatifu na ni dhambi ambayo haisameheki Mbinguni na Duniani.
 
RC ni dini ya ajabu Sana, kupokea michango wanapenda sana lakini pata tatizo ndio utajua kuwa wanafiki wakubwa, Kuna shemeji yangu wa kike alijichinja akafariki na walikuwa hawafunga ndoa aisee waligoma kumzika kwa misa kabisa wakati jamaa aliombwa kanisani kutaja mchango wake alitoa zaidi ya laki tano, shenzi kabisa
 
Sheria za Kanisa zipo wazi kabisa.

Kujiua ni dhambi ya kumkufuru Roho Mtakatifu. Hakuna sababu inayoweza kuhalalisha dhambi ya kujinyonga/kujiua. Huyo Padre wako anapaswa kushtakiwa kwa Baba Askofu Liberatus (wa Jimbo lake).

Kuhusu mtu kumzika kama anastahili au hastahili tunaangalia maisha yake kama yaliakisi utayari wake wa kuuishi Ukristo. Ukizikwa Kikristu siyo ishara ya kwenda mbinguni kama ambavyo usipozikwa Kikristu siyo uthibitisho wa kwenda motoni.

Tunawazika Kikristu wale ambao walionesha kwa matendo yao kuuishi Ukristu: suala la kwamba wadhambi au siyo wadhambi siyo letu, ni la Mungu.

Kwahiyo usipotoshe hapa. Kujiua ni dhambi ya mauaji, ni dhambi ya mauti. Kujinyonga ni kumkufuru Roho Mtakatifu na ni dhambi ambayo haisameheki Mbinguni na Duniani.
Wangapi wanajiuwa na kuzikwa?,asilimia kubwa watu wengi wanajiuwa taratibu bila kujua je Nayo ni dhambi,?mfano wanaokimbiza pikipiki/magari/walevi n.k nao wasizikwe?,je na yule anayekunywa /sumu au kujinyonga na kuokolewa awekwe kundi gani?
 
Sheria za Kanisa zipo wazi kabisa.

Kujiua ni dhambi ya kumkufuru Roho Mtakatifu. Hakuna sababu inayoweza kuhalalisha dhambi ya kujinyonga/kujiua. Huyo Padre wako anapaswa kushtakiwa kwa Baba Askofu Liberatus (wa Jimbo lake).

Kuhusu mtu kumzika kama anastahili au hastahili tunaangalia maisha yake kama yaliakisi utayari wake wa kuuishi Ukristo. Ukizikwa Kikristu siyo ishara ya kwenda mbinguni kama ambavyo usipozikwa Kikristu siyo uthibitisho wa kwenda motoni.

Tunawazika Kikristu wale ambao walionesha kwa matendo yao kuuishi Ukristu: suala la kwamba wadhambi au siyo wadhambi siyo letu, ni la Mungu.

Kwahiyo usipotoshe hapa. Kujiua ni dhambi ya mauaji, ni dhambi ya mauti. Kujinyonga ni kumkufuru Roho Mtakatifu na ni dhambi ambayo haisameheki Mbinguni na Duniani.
Mmmmh ni sawa lakin tambua toba ( kutubu dhambi) ndio kunako kokoa roho ya mtu.

Swali: Je unajua ni neno gani alilosema la mwisho kabla ya kukata roho?
 
Ni jambo rahisi sana, inabidi kutenganisha kazi ya kupima utakatifu wa aliyefariki na huduma ya kuzika.

Mtu akiwa na dhehebu lake akafariki, ile ibada na huduma ya kuzika sio kwa ajili yake pekee, inawahusu ndugu na jamaa zake pua, ni shughuli yao.

Sasa kukataa kumzika mtu kwamba kaenda motoni au mbinguni unatumia kipimo gani? Bora wangemfukuza kanisani asiwe muumini akiwa hai. Mwanafunzi hata akiwa anapata zero mitihani lakini anajulikana ni mwanafunzi wa shule flani.

Ingekua utakatifu unapimwa kibinadam tungekosa wa kuongoza ibada za maziko.
 
Maswali yalioulizwa kwenye huu uzi ni kuntu ingependeza angetokoa kontawa wa rc au madhehebu na dini zinazokuwa na sheria kali kama izi
 
Sheria za Kanisa zipo wazi kabisa.

Kujiua ni dhambi ya kumkufuru Roho Mtakatifu. Hakuna sababu inayoweza kuhalalisha dhambi ya kujinyonga/kujiua. Huyo Padre wako anapaswa kushtakiwa kwa Baba Askofu Liberatus (wa Jimbo lake).

Kuhusu mtu kumzika kama anastahili au hastahili tunaangalia maisha yake kama yaliakisi utayari wake wa kuuishi Ukristo. Ukizikwa Kikristu siyo ishara ya kwenda mbinguni kama ambavyo usipozikwa Kikristu siyo uthibitisho wa kwenda motoni.

Tunawazika Kikristu wale ambao walionesha kwa matendo yao kuuishi Ukristu: suala la kwamba wadhambi au siyo wadhambi siyo letu, ni la Mungu.

Kwahiyo usipotoshe hapa. Kujiua ni dhambi ya mauaji, ni dhambi ya mauti. Kujinyonga ni kumkufuru Roho Mtakatifu na ni dhambi ambayo haisameheki Mbinguni na Duniani.
Umeongea vizuri,ila neno la Mungu linasema ijapokuwa dhambi zenu ni nyekundu Kama bendera zitakuwa nyeupe Kama theluji...je kwenye biblia Kuna sehe mu pameonyeshwa mtu aliyetenda dhambi ya mauaji hasameheki?
 
Back
Top Bottom