Course Coordinator
JF-Expert Member
- Jul 27, 2019
- 1,742
- 3,224
Wasalaam,
Nilipokuwa kidato cha tatu, mwanafunzi mwenzetu alijiua kwa kunywa vidonge 16 vya chloroquine.
Binti huyo aliyekuwa akiitwa Rebeka, alikuwa mzuri wa sura, umbo, na tabia na kwa kweli hakuna hata mtu mmoja aliyewaza kuwa mrembo huyo angeweza Kujitoa roho kikatili hivyo. Kifo chake kilizua mtafaruku mkubwa mno katika familia, lakini kubwa zaidi ni kuwa kanisa lake lilimsusa. Rebeka alikuwa Mkatoliki (RC) na kwa taratibu za kanisa hilo mtu akijiua anakuwa ameikana imani, hivyo hawezi kuzikwa Kikristo.
Ndugu zake walizunguka makanisa kadhaa kutafuta Padre wa kumzika, lakini wote walikataa. Padre mmoja mzee kwa jina la Werawera alipoambiwa tu habari za msiba huo mara moja akakubali kuongoza mazishi bila kipingamizi.
Ajabu baadhi ya waumini wakageuka kumlaumu Padre huyo kwa kukiuka taratibu za kanisa. Wakati wa ibada ya mazishi, ndipo padre huyo akatueleza sababu zilizomsukuma kuja kumzika binti huyo aliyejiua. Akasema “Mama mmoja alikuwa na mume mlevi sana. Kila siku mwanaume huyo alienda kilabuni kunywa pombe na kurudi nyumbani usiku. Kwa vile mama huyo alikuwa Mcha Mungu, hakuweza kumkimbia mumewe; bali kila siku alimuombea kwa Mungu ili abadilike na kuwa mcha Mungu kama yeye.
Lakini siku moja mumewe alipokuwa akivuka daraja kuelekea kilabuni aliteleza na kudumbukia mtoni, akafa maji. Kifo hicho kilimuumiza sana yule mama Kila siku alimlilia Mungu kwa kutosikia maombi yake, na kumuacha mumewe kufa akiwa mlevi, jambo linalothibitisha kuwa amekwenda jehanam.
Lakini siku moja wakati huyo mama amekaa peke yake akisononeka, mpita njia mmoja akamwambia, mama bado unasonononeka kwa ajili ya mumeo? Yule mama akasema ndiyo, na sisononeki kwa sababu amekufa, bali kwa sababu amekwenda jehanam, maana amekufa akiwa mlevi. Yule mtu akamwambia “Mama jiombee nafsi yako wewe, mumeo amemaliza safari yake na yuko peponi” Mama akasema HAIWEZEKANI alikuwa mlevi sana, na alikufa akienda Kutafuta pombe. Yule mtu akamwambia “ mama, alipokuwa akianguka mtoni, katikati ya daraja na maji ALITUBU dhambi zake” halafu yule mtu akatoweka. Kumbe alikuwa ni malaika mjumbe wa Mungu.
Padre akasema mara nyingine tunajipa nafasi ya Mungu na kupora haki ya kuhukumu ambayo ni Kazi ya Mungu tu. Si ajabu tunawazika kwa heshima wale walio machukizo kwa Mungu kwa sababu walifanikiwa kutuhadaa, na tunawadhihaki wale ambao mwenyezi Mungu amewapokea kwa sababu mioyo yao haikuwa na hila, au Walijaliwa KUTUBU kabla mauti haijawachukua. Ni Mungu tu ajuae KWA HIYO Kabla hujasema maneno mabaya kwa mtu aliyekufa, jiulize kama kweli una macho yanayoweza kuona SIRINI kama Mungu.
Inafaa sana KUMKEMEA VIKALI mtu yeyote anayetenda uovu wakati AKIWA HAI ili aziache njia zake mbaya. Lakini akishakufa hawezi kusikia wala kujirekebisha Hivyo hakuna haja ya kumtukana. Matusi kwa marehemu hayamuumizi yeye, bali wana familia yake ambao kimsingi hawana hatia yoyote. Mkaidi achapwe viboko akiwa hai, kwani maiti haijali hata ukali wa moto.
Kujiua sio suluhisho la kutatua matatizo yako.
UWE NA AMANI
Nilipokuwa kidato cha tatu, mwanafunzi mwenzetu alijiua kwa kunywa vidonge 16 vya chloroquine.
Binti huyo aliyekuwa akiitwa Rebeka, alikuwa mzuri wa sura, umbo, na tabia na kwa kweli hakuna hata mtu mmoja aliyewaza kuwa mrembo huyo angeweza Kujitoa roho kikatili hivyo. Kifo chake kilizua mtafaruku mkubwa mno katika familia, lakini kubwa zaidi ni kuwa kanisa lake lilimsusa. Rebeka alikuwa Mkatoliki (RC) na kwa taratibu za kanisa hilo mtu akijiua anakuwa ameikana imani, hivyo hawezi kuzikwa Kikristo.
Ndugu zake walizunguka makanisa kadhaa kutafuta Padre wa kumzika, lakini wote walikataa. Padre mmoja mzee kwa jina la Werawera alipoambiwa tu habari za msiba huo mara moja akakubali kuongoza mazishi bila kipingamizi.
Ajabu baadhi ya waumini wakageuka kumlaumu Padre huyo kwa kukiuka taratibu za kanisa. Wakati wa ibada ya mazishi, ndipo padre huyo akatueleza sababu zilizomsukuma kuja kumzika binti huyo aliyejiua. Akasema “Mama mmoja alikuwa na mume mlevi sana. Kila siku mwanaume huyo alienda kilabuni kunywa pombe na kurudi nyumbani usiku. Kwa vile mama huyo alikuwa Mcha Mungu, hakuweza kumkimbia mumewe; bali kila siku alimuombea kwa Mungu ili abadilike na kuwa mcha Mungu kama yeye.
Lakini siku moja mumewe alipokuwa akivuka daraja kuelekea kilabuni aliteleza na kudumbukia mtoni, akafa maji. Kifo hicho kilimuumiza sana yule mama Kila siku alimlilia Mungu kwa kutosikia maombi yake, na kumuacha mumewe kufa akiwa mlevi, jambo linalothibitisha kuwa amekwenda jehanam.
Lakini siku moja wakati huyo mama amekaa peke yake akisononeka, mpita njia mmoja akamwambia, mama bado unasonononeka kwa ajili ya mumeo? Yule mama akasema ndiyo, na sisononeki kwa sababu amekufa, bali kwa sababu amekwenda jehanam, maana amekufa akiwa mlevi. Yule mtu akamwambia “Mama jiombee nafsi yako wewe, mumeo amemaliza safari yake na yuko peponi” Mama akasema HAIWEZEKANI alikuwa mlevi sana, na alikufa akienda Kutafuta pombe. Yule mtu akamwambia “ mama, alipokuwa akianguka mtoni, katikati ya daraja na maji ALITUBU dhambi zake” halafu yule mtu akatoweka. Kumbe alikuwa ni malaika mjumbe wa Mungu.
Padre akasema mara nyingine tunajipa nafasi ya Mungu na kupora haki ya kuhukumu ambayo ni Kazi ya Mungu tu. Si ajabu tunawazika kwa heshima wale walio machukizo kwa Mungu kwa sababu walifanikiwa kutuhadaa, na tunawadhihaki wale ambao mwenyezi Mungu amewapokea kwa sababu mioyo yao haikuwa na hila, au Walijaliwa KUTUBU kabla mauti haijawachukua. Ni Mungu tu ajuae KWA HIYO Kabla hujasema maneno mabaya kwa mtu aliyekufa, jiulize kama kweli una macho yanayoweza kuona SIRINI kama Mungu.
Inafaa sana KUMKEMEA VIKALI mtu yeyote anayetenda uovu wakati AKIWA HAI ili aziache njia zake mbaya. Lakini akishakufa hawezi kusikia wala kujirekebisha Hivyo hakuna haja ya kumtukana. Matusi kwa marehemu hayamuumizi yeye, bali wana familia yake ambao kimsingi hawana hatia yoyote. Mkaidi achapwe viboko akiwa hai, kwani maiti haijali hata ukali wa moto.
Kujiua sio suluhisho la kutatua matatizo yako.
UWE NA AMANI