Nishajibu, kama nishakujibu na hujaweza kujua jibu nina hakika gani kua kurudia kwangu mara nyingi zaidi kutakupa access ya kujua jibu?
Kama ungejibu unadhani ningeuliza kwanini hujajibu?
Unaweza kuuliza kwanini sijajibu kutokana na uwezo mdogo wa kupambanua hoja zenye majibu ukahisi hujajibiwa
Kwani wewe umejibu mara ngapi?
Mara nyingi
Ulisema yupo? Au hayupo?
Una uhakika gani upeo wangu wa kuelewa majibu ni mdogo kama hata kujibu umeshindwa kujibu?
Kwa kuuliza tu hili swali pia ni uthibitisho juu ya kile unachokiuliza
Sasa umejuaje hakipo kama
hakipo?
Kwasababu hakipo. We ulitaka nikupe ushahidi wa picha kuonesha hakipo?
Good now umekiri umeshindwa kuonesha hakipo na sio kwamba kipo au hakipo.
Sijaandika hivyo wala sijakusudia hivyo usipotoshe kauli yangu
Kushindwa kwangu kuonesha uthibitisho wa kisichokuwepo hakipo ni uthibitisho wa kuonesha kua hakipo
[Quote{Wapi niliandika hivyo sio unanilisha maneno.[/quote]
Humu humu
Nilishajibu kwamba nimeshindwa kuthibitisha.
Hatua gani uliyofikia hadi ukashindwa?
Jibu kwanini isiwezekane?
Yani nijibu swali ambalo we hujaliweka wazi bila kulifafanua?
We umedai kua inawezekana, umeruka step ya kuthibitisha kutilia uzito kwenye hoja yako kuonesha kivipi inawezekana now unaniuliza mimi eti "kwanini isiwezekane"
Thibitisha kauli yako kivipi inawezekana
Una uhakika gani swali langu halijatosha kuwa uthibitisho?
Kwasababu halithibitishi chochote. Swali lako nalifananisha na kivuli cha fimbo kisicho kua na msaada wowote
Ulishasema umeshindwa kuonesha uthibitisho.
Sikuishia hapo tu, vile vile nilisema kwasababu kisichopo hakipo hivyo hata uthibitisho wake haupaswi kuwepo, ukiwepo basi kitu kipo
Hakuna sehemu umethibitisha kama hakipo kama ipo weka hiyo sehemu.
Kwani nimesema hayo mawazo ni ya nani?
Kwani mpaka useme ndio ieleweke ya nani?
Weka uthibitisho mpaka ukafikia hitimisho kua hayupo
Nimeshajibu kwamba huyo mama hayupo duniani ila Inawezekana yeye kuwepo.
Ina maana huna uhakika kwamba yupo ama hayupo?
Kwenye hilo jibu nililojibu kuna linasema nimeshindwa kuthibitisha.
Pia hapo juu umedai kua umefanya research kwenye dunia ukamkosa, hapa unakanusha ulichokijibu huko juu umekua sigara kali hueleweiki kote unawaka.
Kulingana na rejea yako huko juu ebu tuambie kivipi huyo mama hayupo kwenye hii dunia baada ya kufanya research mpaka ukafikia hitimisho kua hayupo?
Nilishajibu inawezekana akawepo na sio kwamba nimeshindwa kuthibitisha kuwa yupo au hayupo basi hayupo.
Assumption sio jibu nalo taka mimi katika hoja zangu, mi nataka facts.
Usipende kuwa kijivu, kama mweusi baki mweusi na kama mweupe uwe mweupe kuliko kujificha kwenye kijivu kukwepa maswali magumu
Sasa Wewe sio mwalimu wangu.
na sijaweka madai kua we ni mwanafunzi wangu, hiyo ni kanuni tu ambayo iko applied sehemu nyingi nimekupa mfano u-relate na mfumo wa hoja nazo kupa, naweza kukupa hoja kwa mtindo wa swali na hilo halimaanishi kwamba nacho kuuliza sikijui
Sababu umeshindwa kujibu swali.
Unajuaje hujajibiwa na sio kwamba umejibiwa umeshindwa kulijua jibu?
Vitaje hivyo viwango vya kuelewa uthibitisho kama vipo.
Kama nimekupa majibu hujayaelewa na umebaki kusisitiza kwamba hujajibiwa Unanihakimishia vipi kwamba nikivitaja utaweza kuvielewa?
Now unatafuta excuses za kutokujibu sababu huwezi kujibu.
Niko makini na unacho kinandika na ndio maana natilia mkazo hoja zangu kulingana na kauli zako. Ukishaniambia kua hujali kujua au kutokujua halafu at the same time ukanuliza swali mimi sio mjinga wa kukurupuka kujibu bila kuzingatia naye mjibu ni kweli anastahili kujibiwa
Onesha
Hilo nilikuuliza mimi wewe ndo unatakiwa kujibu.
Mimi sikukuwekea tafsiri ila nilikupa chanzo chake, ila wewe umeweka maneno tata ambayo ulidai umeyatoa kwenye tafsiri ya hicho chanzo, nimekuuliza unipe link au screenshot inayoonesha tafsiri ya lile neno kwenye hiyo kamusi uliyoinukuu unakimbia
Hiyo inaonesha wazi kua hiyo tafsiri yako ni ya uwongo
Mimi naelewa katika mifumo yote ya uelewa sababu hata hiyo mifumo ya uelewa unayoiongelea sidhani kama ipo.
Sasa mbona hueleweki umesimamia wapi?
Kama huielewi mifumo hiyo kama ipo utaemaje kwamba unaelewa katika mifumo yote?
Huoni ulichokijibu tu hapa kinaipa nguvu hoja yangu kua wewe huelewi?
Mambo makubwa ni yapi hayo?
Yote yaliyo kinyume na madogi
Labda hayo makubwa ni makubwa in your perspective na sio kwangu.
Ushahidi wa hiki kwamba haya mambo ni makubwa huyawezi ebu soma ulichokiandika hapo juu
Sababu nilisema haiwezekani kuthibitisha kisicho uthibitisho sio uthibitisho
Kwanini haiwezekani?
Na sijasema haiwezekani kuthibitisha uthibitisho sio uthibitisho.
Kivipi iwezekane? Thibitisha
Ulichoandika sio uthibitisho.
We mwenyewe ulichokiandika sio uthibitisho kuonesha nilichokiandika awali sio uthibitisho. Unafikiri kuna sababu yeyote ya msingi kufikia hitimisho kwa hoja yako isiyokua na uthibitisho kwamba siko sahihi?
Hakuna sehemu umethibitisha kwamba sijajibu