Si ajabu wangekuwa washadai yeye si Mtanzania!

Si ajabu wangekuwa washadai yeye si Mtanzania!

Yanayoendelea huko Kenya kuhusu suala la uraia wa Miguna Miguna yanasikitisha.

Lakini mwisho wa siku naamini Miguna atawabwaga tu mahakamani.

Na yote haya yamemfika kwa sababu tu alianza kumkosoa sana Uhuru Kenyatta.

Nakumbuka kwenye ule uchaguzi wa 2013 alivyokuwa anapendwa na watu wa Jubilee kwa sababu alikuwa akimnanga Odinga.

Alialikwa hadi kwenye hafla ya kusherehekea uapisho wa Kenyata.

Muda wote huu, hata kipindi akiwa mshauri wa Raila Odinga kipindi ni waziri mkuu, suala la uraia wake halikuwa na utata!

Kagombea mpaka ugavana wa Nairobi na uraia wake ulithibitishwa na tume yao ya uchaguzi.

Hata kitambulisho cha uraia wa Kenya anacho. Achilia mbali kuwa kazaliwa Kenya.

Sasa ghafla baada ya kuanza kumkosoa sana Uhuru eti ndo suala la uraia wake limeibuka.

Sasa huyu Miguna huwa namfananisha na Tundu Lisu kwa umachachari wao wa kuweza kuongea bila hofu.

Kwa mtaji huo, naamini kuwa kama Lisu angekuwa ni mzaliwa wa mikoa iliyo mipakani mwa Tanzania na nchi inayopakana nazo, kudhani au kuhisi kuwa uraia wake ungekuwa ushahojiwa si jambo la ajabu.

Baadhi ya kesi alizofunguliwa Lisu zinachekesha mno kiasi cha kuweza kumfanya mtu adhanie kuwa hao waliotoa maagizo ya yeye kukamatwa na kufunguliwa kesi ni wanafanya hivyo ili kumsumbua tu na si kwa nia ya kwamba wanamfungulia kesi ili hatimaye wampate na makosa na wamfunge jela.

Nadhani huwa wanajua kabisa kuwa kesi zao hazina mashiko.

Hata kwa Miguna Miguna nako ni vivyo hivyo tu.

Watawala wengi wa Afrika wanafanana kwa mengi. Hawapendi kukosolewa na hawana uvumilivu mwingi wa watu wanaotofautiana nao kimtazamo.

Na hulka hii haijalishi kama mtu yupo upinzani au la. Ni kwamba, mtu huyo akishapata madaraka na mamlaka makubwa anabadilika na kutaka kuwa mungu mtu!

Tuna safari ndefu sana na sidhani kama hata njia ya kutufikisha huko twaijua.
Nimeona waliberia wameanza kutimuliwa nyie kina Mange mtapona kweli?!!!
 
Boss idawa Hauogopi Watu Wasiojulikana???!!! Haujui kukosoa ni Kosa la Jinai???!!! Umeongea vizuri na ukweli. Boss Mkuu alianza vizuri sana. Ila sasa sijui kalewa sifa au wanaomshauri na kujishauri wanamdanganya na kujidanganya.
Mkuu haijalishi unaogopa ama jasiri mwisho wa siku utaumizwa na maamuzi ya hii serikali.....
 
Nawe wajipendekeza kwangu?
Amesoma,Leseni yake ni Kubwa....
Ni Dereva mzoefu tatizo lake ni Mkuda....
Magari ya Wagonjwa Hayapishi...
Waenda kwa miguu,Ambao amewagonga Hawahesabiki....
Hili basi analiendesha Vibaya... matuta Anafukia....
Najuta kulidandia........
Kauzu....... Anatupeleka Puta Abiria..
Wengine Sauti zimewakauka Kwa Kulia..
 
Yanayoendelea huko Kenya kuhusu suala la uraia wa Miguna Miguna yanasikitisha.

Lakini mwisho wa siku naamini Miguna atawabwaga tu mahakamani.

Na yote haya yamemfika kwa sababu tu alianza kumkosoa sana Uhuru Kenyatta.

Nakumbuka kwenye ule uchaguzi wa 2013 alivyokuwa anapendwa na watu wa Jubilee kwa sababu alikuwa akimnanga Odinga.

Alialikwa hadi kwenye hafla ya kusherehekea uapisho wa Kenyata.

Muda wote huu, hata kipindi akiwa mshauri wa Raila Odinga kipindi ni waziri mkuu, suala la uraia wake halikuwa na utata!

Kagombea mpaka ugavana wa Nairobi na uraia wake ulithibitishwa na tume yao ya uchaguzi.

Hata kitambulisho cha uraia wa Kenya anacho. Achilia mbali kuwa kazaliwa Kenya.

Sasa ghafla baada ya kuanza kumkosoa sana Uhuru eti ndo suala la uraia wake limeibuka.

Sasa huyu Miguna huwa namfananisha na Tundu Lisu kwa umachachari wao wa kuweza kuongea bila hofu.

Kwa mtaji huo, naamini kuwa kama Lisu angekuwa ni mzaliwa wa mikoa iliyo mipakani mwa Tanzania na nchi inayopakana nazo, kudhani au kuhisi kuwa uraia wake ungekuwa ushahojiwa si jambo la ajabu.

Baadhi ya kesi alizofunguliwa Lisu zinachekesha mno kiasi cha kuweza kumfanya mtu adhanie kuwa hao waliotoa maagizo ya yeye kukamatwa na kufunguliwa kesi ni wanafanya hivyo ili kumsumbua tu na si kwa nia ya kwamba wanamfungulia kesi ili hatimaye wampate na makosa na wamfunge jela.

Nadhani huwa wanajua kabisa kuwa kesi zao hazina mashiko.

Hata kwa Miguna Miguna nako ni vivyo hivyo tu.

Watawala wengi wa Afrika wanafanana kwa mengi. Hawapendi kukosolewa na hawana uvumilivu mwingi wa watu wanaotofautiana nao kimtazamo.

Na hulka hii haijalishi kama mtu yupo upinzani au la. Ni kwamba, mtu huyo akishapata madaraka na mamlaka makubwa anabadilika na kutaka kuwa mungu mtu!

Tuna safari ndefu sana na sidhani kama hata njia ya kutufikisha huko twaijua.
Africa ingefaa itawaliwe tena?
 
Umeiweka vizuri mwanzo lakini kuna maeneo umepindisha na kucheza siasa badala kuzingatia ukweli ili hoja ijadiliwe ipasavyo, Miguna amekua akikosoa serikali na kuropokwa yote, kwanza kipindi alikua anagombea ugavana alitapika maneno ya kila aina, na akaachiwa bila ya kufuatwa. Tatizo limekuja pale alipitiliza kwa kumlisha kiapo cha urais Raila Odinga, hapo Jubilee walihisi kama ametoboa jicho, ikabidi wamkumbushie kale kadhambi kake ka kuukana uraia na kutafuta uraia wa nchi nyingine.

Kumbuka kipindi hicho Kenya hatukua na uraia pacha, ilikua kwamba ukiupata uraia wa nchi nyingine unapoteza wa Kenya. Kwa kifupi awamu ya Kibaki/Raila walifanya figisu na kuvunja shria na kumpa pasipoti ya Kenya bila ya kufuata taratibu za kisheria. Hiyo dhambi ameishi nayo na imekua ikifumbiwa macho hadi alipoichokonoa serikali kwenye macho.
 
Umeiweka vizuri mwanzo lakini kuna maeneo umepindisha na kucheza siasa badala kuzingatia ukweli ili hoja ijadiliwe ipasavyo, Miguna amekua akikosoa serikali na kuropokwa yote, kwanza kipindi alikua anagombea ugavana alitapika maneno ya kila aina, na akaachiwa bila ya kufuatwa. Tatizo limekuja pale alipitiliza kwa kumlisha kiapo cha urais Raila Odinga, hapo Jubilee walihisi kama ametoboa jicho, ikabidi wamkumbushie kale kadhambi kake ka kuukana uraia na kutafuta uraia wa nchi nyingine.

Kumbuka kipindi hicho Kenya hatukua na uraia pacha, ilikua kwamba ukiupata uraia wa nchi nyingine unapoteza wa Kenya. Kwa kifupi awamu ya Kibaki/Raila walifanya figisu na kuvunja shria na kumpa pasipoti ya Kenya bila ya kufuata taratibu za kisheria. Hiyo dhambi ameishi nayo na imekua ikifumbiwa macho hadi alipoichokonoa serikali kwenye macho.

Aliidhinishwaje na IEBC kugombea ugavana wa Nairobi 2017????

 
  • Thanks
Reactions: Oii
Michezo ya kisiasa kama hii siyo ipo Afrika tu. Hata nchi zilizoendelea kama USA ipo. Ni sawa tu na Billy Bush alivyoukalia mkanda wa video uliokuwa unamuonyesha Trump akiwazungumzia wanawake kwa matusi; siku za mwisho kuelekea uchaguzi uliompa Trump urais ndiyo Billy Bush akautoa huo mkanda, presumably in an attempt to help stop Trump from becoming president.
 
Aliidhinishwaje na IEBC kugombea ugavana wa Nairobi 2017????



Narudia tena, serikali ya awamu ya awali ilitenda kosa kumpa pasipoti bila ya kufuata taratibu za kisheria, serikali ya sasa ikafumbia macho hako 'kadhambi', ikamuacha akaidhinishwa kugombea ugavana tena kwa mlengo wa upinzani huku akikosoa serikali balaa.
Sasa serikali ilizidiwa uzalendo au uvumilivu pale aliichokonoa hadi kwenye jicho kwa kutenda kosa la 'uhaini' la kumuapisha Raila. Ndio ikabidi kufukua mifupa yake.
 
Narudia tena, serikali ya awamu ya awali ilitenda kosa kumpa pasipoti bila ya kufuata taratibu za kisheria, serikali ya sasa ikafumbia macho hako 'kadhambi', ikamuacha akaidhinishwa kugombea ugavana tena kwa mlengo wa upinzani huku akikosoa serikali balaa.
Sasa serikali ilizidiwa uzalendo au uvumilivu pale aliichokonoa hadi kwenye jicho kwa kutenda kosa la 'uhaini' la kumuapisha Raila. Ndio ikabidi kufukua mifupa yake.

Sasa mbona mpaka hivi sasa mahakamani anawabwaga hao watu wa serikali?

Na sheria ya uraia ya sasa inasemaje kuhusu Wakenya waliokuwa na uraia wa nchi nyingine kabla ya katiba ya sasa?

Nakwambia mahakamani Miguna atawagaragaza hao serikali.

Believe me [emoji16]
 
Sasa mbona mpaka hivi sasa mahakamani anawabwaga hao watu wa serikali?

Na sheria ya uraia ya sasa inasemaje kuhusu Wakenya waliokuwa na uraia wa nchi nyingine kabla ya katiba ya sasa?

Nakwambia mahakamani Miguna atawagaragaza hao serikali.

Believe me [emoji16]

Kesi iliyowasilishwa mahakamani haihusiani na mambo ya uraia, hivyo ana kila sababu za kuwabwaga maana kilicho mbele ya mahakama ni tofauti kabisa.
Kwa sasa kinachotendeka ni kuhakikisha haruhusiwi kuingia ndani maana hana stakabadhi za uraia wa Kenya.
Wakenya wote waliokua wameukana uraia enzi zile waliombwa waje wawasilishe maombi ya uraia pacha, yeye hakufanya hicho, alitumia mbinu za kifisadi na kupata pasipoti kinyume na sheria.

Kwa kifupi, kama nilivyojibu kwenye hoja zingine, unapoichokoa serikali, hakikisha huna mifupa ya kufukuliwa, leo hii hata Magufuli kuna makaburi ya awamu ya nee anafukua, na kunayo anaachia tu. Ndiovyo siasa za Afrika zilivyo.
 
Na CHADEMA walitangaza kumuunga mkono Uhuru [emoji16][emoji16][emoji16]
Sssssh usiseme sana.
Utawaudhi chadema.

Wanapenda sana style ya Kenyatta..na kwao Kenyatta hakosei..ila sasa Magu akifanya hata moja tu la Kenyatta ndo utaijua kelele ya Chadema.

Hawajalaani mauaji na mateso ya watu kibao huko Kisumu wakati wa uchaguzi, hawajalaani mauaji ya risasi ya waandamanaji watano waliokuwa wakimpokea raila airport, hawajalaani hata kidogo kiongozi mkubwa wa upinzani kunyanyaswa na kufutwa uraia wake wa kuzaliwa, hawajalaani mpendwa wao kukaidi amri za mahakama wazi wazi katika kesi ya Miguna..

Hapa ndio huwa nawashidwa hawa 'makamanda'.
 
Siasa ni biashara chafu, ukweli hugeuzwa uongo na uongo hugeuzwa ukweli kwa maslahi ya kisiasa.
Mara nyingine huwa najiona mjinga sana kushabikia biashara hizi chafu za watu.
Kwa kweli..
Wanasiasa ni watu hatari.
Wengi ni waongo, vigeugeu sana.
tapatalk_1469821199593.jpeg
 
  • Thanks
Reactions: Oii
Back
Top Bottom