Si Cecil Mwambe wala John Heche wanaotosha uenyekiti CHADEMA Taifa, Uenyekiti una mambo mengi

Si Cecil Mwambe wala John Heche wanaotosha uenyekiti CHADEMA Taifa, Uenyekiti una mambo mengi

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2012
Posts
10,307
Reaction score
25,932
Mwanzo mwanzoni niseme wazi kuwa mimi si na sijawahi kuwa mwanachama wa CHADEMA au chama kingine chochote cha siasa hapa Tanzania au kwingineko duniani. Hilo linatosha kutoa maoni yangu huru kuhusu siasa za nchi yangu kwakuwa nazifuatilia.

CHADEMA wanapaswa kufanya uchaguzi mkuu wa kichama kitaifa mwaka huu(kwa mujibu wa Msajili wa Vyama vya Siasa wameshachelewa/ na wao CHADEMA wanadai waliusogeza uchaguzi wao mbele kwa kikao hadi Disemba mwaka huu.

Katika uchaguzi huo, nafasi mbalimbali zitagombewa. Lakini, nafasi ya juu kabisa ya kichama ni ya Mwenyekiti wa Taifa. Nafasi hii ni nyeti kwenye chama chochote-isipokuwa ACT Wazalendo yenye Kiongozi Mkuu wa Chama. Sababu ni kuwa Mwenyekiti ni nembo na kielelezo cha chama.

Mwenyekiti anapaswa kujaa busara, hekima, utulivu, ubunifu, uimara, ukali na upole ambavyo vitatumika kwa nyakati tofauti kulingana na matakwa yaliyo mezani. Si kila wakati huhitajika moja au lingine, hutegemea na mazingira. Mwenyekiti ndiye mtu wa mbele.

Chama ni itikadi na imani. Chama ni nidhamu na utii kwa sheria,taratibu na kanuni zinazokiongoza. Chama ni kukubali au kukataa vikaoni; kupongeza au kukosoa vikaoni. Mwenyekiti hapaswi kuwa mkurupukaji au mfuata upepo au mpendasifa.

Kwa maoni yangu, na kwa sifa nilizozianisha hapo juu, si Cecil Mwambe wa Ndanda wala John Heche wa Tarime wanaofaa kuwa Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa. Wanapaswa kuwa darasani kiuongozi kwa muda kidogo kabla ya kukabidhiwa chama hicho.

Mapendekezo yangu yangekuwa John John Mnyika wa Kibamba au Joseph Selasini wa Rombo. Lakini, Mbowe anapaswa kupumzika na kuketi benchi la washauri wa chama.
 
Mwanzo mwanzoni niseme wazi kuwa mimi si na sijawahi kuwa mwanachama wa CHADEMA au chama kingine chochote cha siasa hapa Tanzania au kwingineko duniani. Hilo linatosha kutoa maoni yangu huru kuhusu siasa za nchi yangu kwakuwa nazifuatilia.

CHADEMA wanapaswa kufanya uchaguzi mkuu wa kichama kitaifa mwaka huu(kwa mujibu wa Msajili wa Vyama vya Siasa wameshachelewa/ na wao CHADEMA wanadai waliuosogeza uchaguzi wao mbele kwa kikao hadi Disemba mwaka huu.

Katika uchaguzi huo, nafasi mbalimbali zitagombewa. Lakini, nafasi ya juu kabisa ya kichama ni ya Mwenyekiti wa Taifa. Nafasi hii ni nyeti kwenye chama chochote-isipokuwa ACT Wazalendo yenye Kiongozi Mkuu wa Chama. Sababu ni kuwa Mwenyekiti ni nembo na kielelezo cha chama.

Mwenyekiti anapaswa kujaa busara, hekima, utulivu, ubunifu, uimara, ukali na upole ambavyo vitatumika kwa nyakati tofauti kulingana na matakwa yaliyo mezani. Si kila wakati huhitajika moja au lingine, hutegemea na mazingira. Mwenyekiti ndiye mtu wa mbele.

Chama ni itikadi na imani. Chama ni nidhamu na utii kwa sheria,taratibu na kanuni zinazokiongoza. Chama ni kukubali au kukataa vikaoni; kupongeza au kukosoa vikaoni. Mwenyekiti hapaswi kuwa mkurupukaji au mfuata upepo au mpendasifa.

Kwa maoni yangu, na kwa sifa nilizozianisha hapo juu, si Cecil Mwambe wa Ndanda wala John Heche wa Tarime wanaofaa kuwa Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa. Wanapaswa kuwa darasani kiuongozi kwa muda kidogo kabla ya kukabidhiwa chama hicho.

Mapendekezo yangu yangekuwa John John Mnyika wa Kibamba au Joseph Selasini wa Rombo. Lakini, Mbowe anapaswa kupumzika na kuketi benchinla washauri wa chama.
Nilitegemea utatuwekea sifa za watu uliowataja, kama ni kutaja majina tu hata mimi nilishapendekeza Membe anafaa sana uenyekiti wa CCM ila sijui kwanini hawanisikii.
 
Nilitegemea utatuwekea sifa za watu uliowataja, kama ni kutaja majina tu hata mimi nilishapendekeza Membe anafaa sana uenyekiti wa CCM ila sijui kwanini hawanisikii.
[/QUOTE}
Hahahaaaa...... Wewe sifa ya Selasini huijui ambayo Cecil Mwambe anaikosa?!

Acha utani bwashee
 
Mapendekezo yangu yangekuwa John John Mnyika wa Kibamba au Joseph Selasini wa Rombo. Lakini, Mbowe anapaswa kupumzika na kuketi benchinla washauri wa chama.
Unataka akae mtu wa "kuunga juhudi" CDM ife? Kwa mazingira ya sasa ya udikiteita wa Jiwe, MBOWE should remain! Kama kungelikuwa na hali shwali ya kisiasa, Mbowe nami nngelisema apumzike, lkn kwa mazingira ya sasa ambapo watu wanarubuniwa kwa mabilioni, nani wa kuzikataa katika safu ya CDM? Wapo lkn kwa sasa tumuache Mbowe apambane na Jiwe! Lisu anaweza kuzikataa billions za Jiwe! Lakini kwa sasa naye waache kwanza.
 
Kwa maoni yangu, na kwa sifa nilizozianisha hapo juu, si Cecil Mwambe wa Ndanda wala John Heche wa Tarime wanaofaa kuwa Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa. Wanapaswa kuwa darasani kiuongozi kwa muda kidogo kabla ya kukabidhiwa chama hicho.
La msingi kama wanaona wanafaa basi wawe huru kugombea na wapiga kura wata amua ni nani wanamtaka kuwa mwenye kiti wao. Watupe uchaguzi wa kistarabu unao endana na katiba yao(good governance ina anzia chamani).
Wasiwe kama wale wanaosema utaratibu wetu ni............hata kama utaratibu huo umepitwa na wakati.
 
Yote yafanyike mi natoa baraka zangu tunahitaji utulivu na amani kwa hili
 
Magufuli alipelekwa chuo cha uongozii kuiongoza ccm na Nchi?, anazijua itikadi za chama chake?. John Heche anafaa Sana, chadema inahitaji Mtu jasiri atakayepambana na hujuma za ccm!!!!, Muda wa busara ulikuwa awamu zilizopita awamu tunahitaji mwenyekiti mwenye kauli thabiti na aliyemstali wa mbele. mnyika na selathin waoga sana hawafai.
 
Back
Top Bottom