Si Cecil Mwambe wala John Heche wanaotosha uenyekiti CHADEMA Taifa, Uenyekiti una mambo mengi

Si Cecil Mwambe wala John Heche wanaotosha uenyekiti CHADEMA Taifa, Uenyekiti una mambo mengi

Hakuna wanawake? Wanaoweza kushika nafasi za makamo au katibu mkuu? Ccm watakisambaratisha kwa propaganda za ukanda!!!

Hii nafasi ingemfaa sana Dr Slaa....
Kwa sababu yeye wa kanda ipi? Mbona unajichanganya sana,kama ni mahaba kwa slaa kaungane na Josephine kuwa naye alipo
 
Asee huu uzi ukiusoma halafu ukavuta picha ya Mwenyekiti wa CCM loh 😂 umempiga vilivyo..

Kwa Chadema Heche ni moja ya Mtu ninayemkubal ni Mvumilivu na anasimama katika haki wakati wote.
 
Unataka akae mtu wa "kuunga juhudi" CDM ife? Kwa mazingira ya sasa ya udikiteita wa Jiwe, MBOWE should remain! Kama kungelikuwa na hali shwali ya kisiasa, Mbowe nami nngelisema apumzike, lkn kwa mazingira ya sasa ambapo watu wanarubuniwa kwa mabilioni, nani wa kuzikataa katika safu ya CDM? Wapo lkn kwa sasa tumuache Mbowe apambane na Jiwe! Lisu anaweza kuzikataa billions za Jiwe! Lakini kwa sasa naye waache kwanza.
Kabisa si heche, mnyika wala Mwambe binafsi hata Selasini wanaweza kuvaa viatu vya Mbowe katika kipindi hichi kigumu kuwahi kutokea tangu upinzani umeanzishwa Tanzania 1992.
Mbowe bado anafaa kulinga na kipindi kigumu wanachopitia wapinzani wa Tanzania
 
Kabisa si heche, mnyika wala Mwambe binafsi hata Selasini wanaweza kuvaa viatu vya Mbowe katika kipindi hichi kigumu kuwahi kutokea tangu upinzani umeanzishwa Tanzania 1992.
Mbowe bado anafaa kulinga na kipindi kigumu wanachopitia wapinzani wa Tanzania
That is my point!
 
La msingi kama wanaona wanafaa basi wawe huru kugombea na wapiga kura wata amua ni nani wanamtaka kuwa mwenye kiti wao. Watupe uchaguzi wa kistarabu unao endana na katiba yao(good governance ina anzia chamani).
Wasiwe kama wale wanaosema utaratibu wetu ni............hata kama utaratibu huo umepitwa na wakati.
Wazo zuri la ukomavu wa demokrasia
 
Naona unataka uturudishe kule kule! Kaskazini. Lakini ahueni umeunga mkono kamanda kukaa pembeni na kuwapisha wengine.
Wewe unataka je?
Chadema ikifa ni dhahiri upinzani wa Tanzania utakufa hata haya machache tunayoyasikia huenda itakuwa ni story na maendeleo itabakia kuwa dhana
 
Umemalizia kwa Mh Mbowe apumzike kwa lipi? Mbona umemalizia kirahisi sana kuliko ulivyoanza!! Ebu rudi tena utueleze apumzike kivipi, na awe mshahuri kivipi.
Pili ujue Chadema ni chama cha siasa, chenye lengo la kushika dola.
Kwahiyo hakijafikia hilo lengo bado, sasa unapokuwa na mwenyekiti ambae amekitoa chama kikiwa na wabunge wanne, mpaka kufika 70 hii leo, halafu unasema apumzike ili iweje?
Hauoni ni kurudisha chama nyuma?
Na kama chama tawala chenyewe, mwenyekiti wake ni yule anaekuwa Rais, hauoni hapo kuwa bado kinaogopa kumpa uenyekiti mtu tofauti ili asije mvuruga Rais?
Mh msomi mimi nakupinga kwa hoja zako, uongozi ni kalama na sio kila mtu anafaa kuongoza. Wengine lazima waandaliwe ili waongoze, kwa chama chetu Chadema mimi nasema tunamuhitaji Mh Mbowe kuliko yeye anavyokihitaji chama chetu.
Naunga mkono hoja ya Mh Mbowe kugombea tena uenyekiti wa chama, mpaka pale Tanzania itakapo pata Rais sahihi wa kuongoza nchi.
Na kipindi hiki ambacho demokrasia imesilibwa upinzani wahitaji kiongozi shupavu aina ya Mbowe la sivyo tutakuwa na upinzani wa kina mlema na cheyo
 
Back
Top Bottom