Si hata Rais Mstaafu Mwinyi walisema anauza nchi? Kiko wapi?

Si hata Rais Mstaafu Mwinyi walisema anauza nchi? Kiko wapi?

The Boss

JF-Expert Member
Joined
Aug 18, 2009
Posts
49,282
Reaction score
117,244
mwinyi-pic.jpg


Huu wimbo wa kila Rais kuambiwa anauza nchi ulianza kwa Rais Mwinyi, unajua sababu ilikuwaje?

Baada ya Nyerere kwenda China mwaka 1966 akasema akakuta kule China kila kitu kinafanywa na serikali kuanzia maduka ya mchele na sigara hadi magari ya taxi na bakery za kuuza mikate.U communist ulikuwa umepamba Moto sana sana, ingawa leo wachina washaufuta kabisa huo ucommunits. Lakini kipindi Nyerere anaenda huko hadi Suti zile tunaita Kaunda Suit Nyerere alitoa huko kwa wachina. Waziri mkuu wao anaitwa Choun Enlai kama sikosei, Kaunda nae alizitoa huko huko kwa wachina.

Nyerere aliporudi mwaka 1967 akapitisha Azimio la Arusha na kuanza rasmi "siasa za Ujama na kujitegemea" na kutaiifisha biashara zote za watu binafsi na majumba yao na kampuni za Serikali za kuuza mchele na sigara zikaanzishwa kukaja RTC ikaja Co Cabs kampuni ya taxi ya serikali. RTC na maduka ya kijiji na mtaa na shirika la kusaga na kukoboa unga na Makampuni Tele Tele ya serikali.

Ikawa marufuku kwa mwananchi kumiliki taxi yako binafsi hata kununua gari tu Kwa kibali maalum kwanza. Ikawa marufuku kuwa hata na kiduka cha kuuza mchele na unga na sigara, ukifanya hivyo wewe ni mhujumu wa uchumi na bepari na mkabaila. Siasa hizo pia zilifanya kila shirika kuwe na ofisi ya CCM wananchi wanafundishwa utii na itikadi za siasa ya Ujamaa na kujitegemea.

Pamoja na mazuri mengi sana ya Nyerere na siasa ya Ujamaa na kujitegemea lakini ukweli usemwe ku copy kila kitu Kwa wachina bila kuangalia mazingira yetu alikosea sana hasa pale alipojaribu kuanzisha vijiji vya ujamaa. Watu wakaondolewa kwa nguvu kwenye mashamba yao wakalazimishwa kulima shamba la kijiji.

Wengine waliogoma wakachomewa nyumba zao moto waende wahamie kwenye vijiji vya ujamaa, wapo walioliwa na Simba na wengi walipohamia huko wakawa masikini zaidi. Hadi zoezi la vijiji vya ujamaa likapigwa stop, nchi ikaingia na njaa, uzalishaji ukapungua.

Kupata bidhaa kama sigara na mchele au unga ikawa Kwa kupanga foleni na kupigana vikumbo kwenye maduka ya vijiji na mitaa. Hali ikawa mbaya zaidi vita ya Uganda ilipofika.

Wakati Mwinyi anachukua nchi hali ilikuwa mbaya sana ikabidi aanze na kuruhusu watu binafsi wafanye biashara hizo ndogo ndogo kama kuuza mikate, mchele na sigara ili serikali itoke huko. Kampuni kama co cabs ya Taxi ikabidi iaachwe ife kifo cha kawaida, maduka ya RTC ikabidi nayo yafe, watu wenye exposure kidogo na biashara.

Wahindi, waarabu since Wana mitaji ya ndugu zao nje uzoefu wakawa wa kwanza kushika biashara hizo kabla ya waswahili, wachaga, wakinga n.k kuja later kuzishika na kuwa replace kabisa baadae. Wakati haya yote yanayokea alichoambulia Mwinyi ni matusi tu ya "kuuza nchi "na "kuwapa wahindi na waraabu" njia za uchumi as if kuna mswahili aliezuiwa kumiliki duka la kuuza mchele na sigara.

Leo hiii Kariakoo yote imejaa watu wa makabila tofauti, watu wamejiongeza now wanaenda wenyewe popote pale iwe China au Uturuki, haijalishi we mkinga au mchaga unafanya biashara popote Kwa uwezo wako wa akili na mtaji.

Popote leo ukianzisha mashine ya kusaga na kukoboa mchele au duka la jumla hakuna wa kukuita bepari wala kabaila, wala kukutisha.

Kilelele ilikuwa mwaka 1992 ambapo Mwinyi alifuta kabisa Azimio la Arusha na kuleta Azimio la Zanzibar ambalo lilipiga kabisa marufuku ya wananchi kunyayaswa Kwa aina yoyote kuhusu vibali vya biashara, wala kuuliza uliza watu kuhusu biashara wanazotaka kufanya na kuanza kuwaletea zengwe la "makabaila na mabepari"

Matusi aliyopata Mwinyi kuwa "anauza nchi" yalikuwa makubwa sana na mambo ya kumuita Mzanzibari tunataka Tanganyika yalikuwa mengi Sana kama sasa tu au pengine zaidi lakini alipokuja Rais Mtanganyika watu walikuwa tayari washazoea "matunda ya Rais Mwinyi' kiasi washasahau kuwa walikuwa wanataka turudi nyuma tena kwenye maduka ya serikali na taxi za Serikali na maduka ya vijiji na serikali kuuza mikate na sigara.

Sometimes kuwatoa watu kwenye kiza unaweza ambulia matusi makubwa sana. Hadi watu hao wafike kwenye mwanga ndo wanakuja kugundua aaha kumbe tulikuwa tunakuja huku.
 
View attachment 2678190

Huu wimbo wa kila Rais kuambiwa anauza nchi ulianza kwa Rais Mwinyi, unajua sababu ilikuwaje?

Baada ya Nyerere kwenda China mwaka 1966 akasema akakuta kule China kila kitu kinafanywa na serikali kuanzia maduka ya mchele na sigara hadi magari ya taxi na bakery za kuuza mikate.U communist ulikuwa umepamba Moto sana sana, ingaw
Mkataba wa IOC uliendelezwa? Unajua maana ya kuvunja katiba? Unataka kuhalalisha haramu?
Kuna shida gani kusaini Mkataba wenye kuheshimu katiba tuliyonayo na uhuru wetu?
Usiwadanganye watu...bila Nyerere kuzima lile kundi la G55, wale jamaa wangeanzisha serikali ya Tanganyika. Shingo ilishaelekea kibra
 
View attachment 2678190

Huu wimbo wa kila Rais kuambiwa anauza nchi ulianza kwa Rais Mwinyi, unajua sababu ilikuwaje?

Baada ya Nyerere kwenda China mwaka 1966 akasema akakuta kule China kila kitu kinafanywa na serikali kuanzia maduka
Hivi hujui kama aliuza Loliondo hata kwenye kitabu chake amekiri? au unajitoa ufahamu?
 
Mkataba wa IOC uliendelezwa? Unajua maana ya kuvunja katiba? Unataka kuhalalisha haramu?
Kuna shida gani kusaini Mkataba wenye kuheshimu katiba tuliyonayo na uhuru wetu?
Usiwadanganye watu...bila Nyerere kuzima lile kundi la G55, wale jamaa wangeanzisha serikali ya Tanganyika. Shingo ilishaelekea kibra
To be honest bila Nyerere kuweka mguu kati Tanganyika ingekua ishapatikana kitambo...
 
Kwani Zanzibar wao ufanisi na uboreshaji wa bandari hawautaki? Mbona Samia haupeleki kwao Zanzibar nao wakafaidike na ufanisi wa bandari kuendeshwa na DP World?

Bamdari zinazofanya vibaya ni za Tanganyika tu za Zanzibar hazina matatizo?

Samia aachane na bandari zetu, akauze za kwao Zanzibar.
 
Tunavyosema nchi inauzwa maana yake rasilimali muhimu za nchi zinamilikishwa kwa hao wageni kwa kutumia mikataba mibovu kabisa.
Mfano ni gesi yetu hii SIO YA KWETU.
Rejea hii hapa
 
View attachment 2678190

Huu wimbo wa kila Rais kuambiwa anauza nchi ulianza kwa Rais Mwinyi, unajua sababu ilikuwaje?

Baada ya Nyerere kwenda China mwaka 1966 akasema akakuta kule China kila kitu kinafanywa na serikali kuanzia maduka y
Watu weng ni wajinga na ni ngumu sana kuwatoa kwenye ujinga maana tunaongozwa na hisia na mihemko na kuburuzwa na wengne
 
Mzee Mwinyi: Mambo yaliyotushinda sisi Marais Watatu kwa miaka 30 Shujaa Magufuli ameyafanya kwa miaka 3
Hii nchi ni ngumu sana. Kila mtu anatetea upande wake uliopakwa siagi.

angalizo tuu: No body saw Magufuli coming!!!!

wanasiasa wetu wawe makini na ujangili wao wa mali za walalahoi. Ipo siku kila mtu ataubeba msalaba wake mwenyewe.
 
Mzee Mwinyi: Mambo yaliyotushinda sisi Marais Watatu kwa miaka 30 Shujaa Magufuli ameyafanya kwa miaka 3
Huyo unaemwita shujaa aliirudisha gesi yetu mikononi mwetu?
Na je wakati mikataba ya gesi inasainiwa yeye alifanya nini kuzuia akiwa kama Mbunge na Waziri?
Upuuzi wote wamefanya CCM na hakuna ccm yoyote anaeitakia mema hii nchi zaidi ya matumbo yao pekee .
 
The Boss njoo ujibu hapa
yaani wakati tunajadili yoote haya, tusisahau kuwa kuna mkataba wa aina hii hii na kwa waarabu wa aina hii hii ulisainiwa na watanzania walilaamika sana. leo hii pale loliondo madege ya kijeshi toka uarabuni yanadondoka na kupaa tu na twiga wetu.

Hata mfalme wa uarabuni/dubai sijui alikuja Tanzania (loliondo) bila kupitia kusalimia Ikulu ya Rais, manake alikuwa anaenda kwenye ardhi yake ya kiarabu aliyoinunua. angefikiri pale loliondo ni tanzania angefika kwanza dsm halafu aende kutalii loliondo.
 
Back
Top Bottom