mwanamwana
JF-Expert Member
- Aug 1, 2011
- 1,309
- 4,798
Nadhani ilikuwa hiyo kabla ya Karagwe haijagawanywa wilaya mbili.Mkuu, ninatamani sana kufika Wilaya moja inaitwa Kyerwa. Ninasikia katika Wilaya hiyo moja kuna mipaka ya nchi mbili za Uganda na Rwanda?
Acha dhambi majira ya Majilio hayaUkitoka Karagwe Wakati Unakwenda Rusomo Ndiyo Utapita
Kyerwa
Missenyi imepakana na kyerwa na bukoba, ukitoka Missenyi utaenda kyerwa halafu Karagwe.
Mkuu, Missenyi na kyerwa si zote mwanzo zilihesabika Karagwe?Mkuu hujui chochote kuhusu Kagera, Missenyi imepakana na Bukoba na Karagwe then ndo Kyerwa. Hii wilaya ya Kyerwa ipo mpakani huko mwa Rwanda na juu Uganda
Mi sijapinga kuhusu kupakana, labda kwa kuwa sijasema inapakana na Karagwe, na aliyetoka Missenyi akapita Karagwe akaenda Kyerwa ndio akafika rusumo labda ndio umueleweshe vizuri mkuu.Mkuu hujui chochote kuhusu Kagera, Missenyi imepakana na Bukoba na Karagwe then ndo Kyerwa. Hii wilaya ya Kyerwa ipo mpakani huko mwa Rwanda na juu Uganda
Mkuu nisamehe bure[emoji16][emoji16] nimepitia komenti yangu sikumaanisha kutoka Misenyi unaingia kyerwa maana huko ni kuzunguka, lakini pia inategemea unatokea Missenyi sehemu gani, japo Misenyi huko ndani sipafahamuMkuu hujui chochote kuhusu Kagera, Missenyi imepakana na Bukoba na Karagwe then ndo Kyerwa. Hii wilaya ya Kyerwa ipo mpakani huko mwa Rwanda na juu Uganda
Nimekaaa pale kama wiki wanyarwanda wengi sana aiseee.....vipi Western hotel imeboreshwa?Sisi wengine na Banyankole wa Kaisho
Asante kwa ufafanuzi. Alitaka kutupotosha.Mkuu ramani yako imekaa vibaya, baada ya kyerwa ni Karagwe, halafu Ngara rusumo.
Sio karagwe, kyerwa, Ngara rusumo.
Karagwe imepakana na Rwanda wakati kyerwa ni Rwanda na Uganda.
We jamaa acha uongo,Rusumo ipo karibu na biharamulo,ni njia ya kwenda N'gara,Kama unataka kahama,unapita nyakanazi(,njia panda ya kigoma,)Ukitoka Karagwe Wakati Unakwenda Rusomo Ndiyo Utapita
Kyerwa
Pembezoni mwa mto NgonoKaterero asili yake ni wapi?
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] kuna ile clip Mzee wa kihaya anawasilisha rambirambi msibaniWengine sisi ni Waingereza Ila kwetu Kanyigo
🤔Kiongozi Mimi Nilipita Sijaishi Huko
Sijajua Kama Kuna Mipaka Hiyo
Ila Nilipita Pori La Burigi Chato National Park
Siyo Rahisi Kuwa Na Mipaka Hiyo
Bila Shaka Lazima Itakuwa Nchi Ya Uganda, Rwanda, Burundi. Ukweli Nimetembea Wilaya Zote Za Mkoa Wa Kagera Tena Nilitokea Biharamulo, Muleba, Mpaka Misenyi
Ndiyo Unakwenda Karagwe
Unapajua Kyanyamisa?We jamaa acha uongo,Rusumo ipo karibu na biharamulo,ni njia ya kwenda N'gara,Kama unataka kahama,unapita nyakanazi(,njia panda ya kigoma,)
Kufika kyerwa,unaweza kupitia karagwe,au Kama unataka bukoba mjini,unaweza ukapita kagera sugar,ukaingia Uganda,then unaibukia kyerwa,karibu na Mulongo border
Katika wilaya zote za Kagera Ngara ipo good Sana landscape yakePia ufike na Ngara uone eneo maarufu kama mafiga matatu kwa wenyeji wa huko, ni mpaka unaotenganisha Tanzania, Burundi na Rwanda. Kwa jinsi palivyo ni kama mafiga japo mto kagera ndio umetenganisha Rwanda na Tanzania, huku Burundi na Tanzania zikitenganishwa na bonde.
Hapana,hapo bado kabisa kufika wilaya ya Kyerwa hapo ni Karagwe ili kufika wilaya ya Kyerwa kwa barabara hiyo ni baada ya kupita Omurushaka uelekee Nkwenda siyo KayangaUnapajua Kyanyamisa?
yupo sahihi ukitoka Rusumo unakuja Benaco then unaingia pori la Kimisi hapo Kyanyamisa ndio barrier ya mwisho ya polisi na ipo wilaya ya kyerwa ukitoka hapo unaitafuta omurushaka Karagwe.
Nakushauri kasome tena historia vizuri ya mkoa wa Kagera. Wanahistoria wengine wanasema kuwa neno "haya" lilitokana na matatizo ya mawasiliano kati ya wageni/wakoloni wa mwanzo na wenyeji wa mkoa wa Kagera wa wakati huo. Kutokana na matatizo ya lugha ya mawasiliano miongoni mwa wenyeji wa Kagera na wakoloni, wazungu hawa walishangaa kila wakiongea na wenyeji neno "haya" linaloashiria kukubali au kusema "ndiyo" lilijitokeza sana kwa wenyeji wa Muleba, Bukoba Mjini na Vijijini na Karagwe.KAGERA NI MUHAYA Turejee Historia. Wahaya ni nani? Jina Wahaya lilianza kutumika lini? Jina Wahaya linatokana na nomino IHAYA. Huu ni mwambao wa Ziwa Lweru.
Hadi ujio wa Wazungu lilimaanisha mwambao wa ziwa hilo sehemu za sasa Kyamutwara na Maruku. Ihaya lilikuwa ni eneo la vijiji vya wavuvi. Kwahiyo neno Wahaya lilimaanisha wavuvi. Katika kitabu cha Historia ya Bukoba, Hans Cory anasema jina Muhaya lilikuwa ni tusi dogo maana wavuvi hawakuwa na mahali pa kudumu pa kuishi na hawakuwa na mali ya kudumu.
Neno Ihaya halikuishia Kyamutwara na Maruku. Ihangiro ya zamani, uligawanyika sehemu mbili: Migongo na Omwihaya.
Kwa hiyo matumizi ya jina Wahaya yalienea hadi Ihangiro. Rekodi za wapelelezi wa Kizungu zinataja jina Buhaya. Omukama Rumanyika Orugundu alimwambia Speke: Mashariki mwa Karagwe kando ya ziwa kunaitwa BUHAYA ni maarufu kwa kilimo cha mibuni na pembe za ndovu. Mwisho wa kunukuu.
Katika vitabu vingine kama vile Victoria Nyanza, Karagwe ina sura yake na eneo lote Mashariki ya Karagwe wanaliita Kiziba.
Athari hiyo bado ipo Baganda huita Wahaya wote Baziba Jina Wahaya linaendana na jina jingine BUKOBA. Bukoba ni sehemu ya ukoo wa ABAKOBA. Ni pale kastamu.
Kwa kweli Bukoba kama eneo walikaa Wavuvi, Abahaya. Kuenea kwa matumizi ya majina Bukoba na Wahaya kuliambana na uvamizi wa wakoloni.
Wajermani walilipanua kujumuisha mji wa Bukoba, baadaye tawala zote za kando ya ziwa. Kwa wakati huo Karagwe haikujumuishwa. Na hata Omukama Ntare wa Karagwe walipomnyonga. Karagwe iliwekwa kwenye usimamizi wa Omukama Kahigi wa Kihanja ila ikabaki inajitegemea."
hii mpya,wahaya wengine wanatokea wapiNa si kila mhaya anatoka Kagera!