Si kila anayetoka Kagera ni Mhaya

Si kila anayetoka Kagera ni Mhaya

Mkuu, ninatamani sana kufika Wilaya moja inaitwa Kyerwa. Ninasikia katika Wilaya hiyo moja kuna mipaka ya nchi mbili za Uganda na Rwanda?
Nadhani ilikuwa hiyo kabla ya Karagwe haijagawanywa wilaya mbili.

Kwa upande wa Uganda ni Wilaya ya Kyerwa kata ya Murongo. Huko kuna pombe inaitwa Uganda walaji hiyo usipime.

Kwa upande wa Rwanda sina kumbukumbu nzuri lakini ni wilaya ya Karagwe kata za Bweranyange, Nyaishozi etc. Nakumbuka miaka ya 2004-2006 walienda kijiji kimoja mpakani wakakuta 90% ya wakazi ni Wanyarwanda. Tatizo wanahamia na mifugo yao yaani ni shida kabisa.
 
Missenyi imepakana na kyerwa na bukoba, ukitoka Missenyi utaenda kyerwa halafu Karagwe.

Mkuu hujui chochote kuhusu Kagera, Missenyi imepakana na Bukoba na Karagwe then ndo Kyerwa. Hii wilaya ya Kyerwa ipo mpakani huko mwa Rwanda na juu Uganda
 
Mkuu hujui chochote kuhusu Kagera, Missenyi imepakana na Bukoba na Karagwe then ndo Kyerwa. Hii wilaya ya Kyerwa ipo mpakani huko mwa Rwanda na juu Uganda
Mkuu, Missenyi na kyerwa si zote mwanzo zilihesabika Karagwe?
 
Mkuu hujui chochote kuhusu Kagera, Missenyi imepakana na Bukoba na Karagwe then ndo Kyerwa. Hii wilaya ya Kyerwa ipo mpakani huko mwa Rwanda na juu Uganda
Mi sijapinga kuhusu kupakana, labda kwa kuwa sijasema inapakana na Karagwe, na aliyetoka Missenyi akapita Karagwe akaenda Kyerwa ndio akafika rusumo labda ndio umueleweshe vizuri mkuu.
 
Mkuu hujui chochote kuhusu Kagera, Missenyi imepakana na Bukoba na Karagwe then ndo Kyerwa. Hii wilaya ya Kyerwa ipo mpakani huko mwa Rwanda na juu Uganda
Mkuu nisamehe bure[emoji16][emoji16] nimepitia komenti yangu sikumaanisha kutoka Misenyi unaingia kyerwa maana huko ni kuzunguka, lakini pia inategemea unatokea Missenyi sehemu gani, japo Misenyi huko ndani sipafahamu
 
Ukitoka Karagwe Wakati Unakwenda Rusomo Ndiyo Utapita
Kyerwa
We jamaa acha uongo,Rusumo ipo karibu na biharamulo,ni njia ya kwenda N'gara,Kama unataka kahama,unapita nyakanazi(,njia panda ya kigoma,)
Kufika kyerwa,unaweza kupitia karagwe,au Kama unataka bukoba mjini,unaweza ukapita kagera sugar,ukaingia Uganda,then unaibukia kyerwa,karibu na Mulongo border
 
Ulifika Hadi pande za Ngara
Kiongozi Mimi Nilipita Sijaishi Huko
Sijajua Kama Kuna Mipaka Hiyo

Ila Nilipita Pori La Burigi Chato National Park
Siyo Rahisi Kuwa Na Mipaka Hiyo
Bila Shaka Lazima Itakuwa Nchi Ya Uganda, Rwanda, Burundi. Ukweli Nimetembea Wilaya Zote Za Mkoa Wa Kagera Tena Nilitokea Biharamulo, Muleba, Mpaka Misenyi
Ndiyo Unakwenda Karagwe
🤔
 
We jamaa acha uongo,Rusumo ipo karibu na biharamulo,ni njia ya kwenda N'gara,Kama unataka kahama,unapita nyakanazi(,njia panda ya kigoma,)
Kufika kyerwa,unaweza kupitia karagwe,au Kama unataka bukoba mjini,unaweza ukapita kagera sugar,ukaingia Uganda,then unaibukia kyerwa,karibu na Mulongo border
Unapajua Kyanyamisa?
yupo sahihi ukitoka Rusumo unakuja Benaco then unaingia pori la Kimisi hapo Kyanyamisa ndio barrier ya mwisho ya polisi na ipo wilaya ya kyerwa ukitoka hapo unaitafuta omurushaka Karagwe.
 
Pia ufike na Ngara uone eneo maarufu kama mafiga matatu kwa wenyeji wa huko, ni mpaka unaotenganisha Tanzania, Burundi na Rwanda. Kwa jinsi palivyo ni kama mafiga japo mto kagera ndio umetenganisha Rwanda na Tanzania, huku Burundi na Tanzania zikitenganishwa na bonde.
Katika wilaya zote za Kagera Ngara ipo good Sana landscape yake
 
Unapotoka Bukoba mjini mpka Kyaka pale kuna njia panda ya kwenda Mtukura yaani mpk wa Uganda na Tanzania alafu kushoto unaenda Karangwe ambapo unaenda mpk Ngara ambapo utapata mpaka wa Rwanda na Tanzania alafu Burundi na Tanzania ila mipaka hiyo ipo kwenye wilaya tatu tofauti lakini zipo kwenye ukanda moja... Sema ni raha sana kwa sababu kuna utamu wa vitu vya mpakani....
 
Unapajua Kyanyamisa?
yupo sahihi ukitoka Rusumo unakuja Benaco then unaingia pori la Kimisi hapo Kyanyamisa ndio barrier ya mwisho ya polisi na ipo wilaya ya kyerwa ukitoka hapo unaitafuta omurushaka Karagwe.
Hapana,hapo bado kabisa kufika wilaya ya Kyerwa hapo ni Karagwe ili kufika wilaya ya Kyerwa kwa barabara hiyo ni baada ya kupita Omurushaka uelekee Nkwenda siyo Kayanga
 
KAGERA NI MUHAYA Turejee Historia. Wahaya ni nani? Jina Wahaya lilianza kutumika lini? Jina Wahaya linatokana na nomino IHAYA. Huu ni mwambao wa Ziwa Lweru.

Hadi ujio wa Wazungu lilimaanisha mwambao wa ziwa hilo sehemu za sasa Kyamutwara na Maruku. Ihaya lilikuwa ni eneo la vijiji vya wavuvi. Kwahiyo neno Wahaya lilimaanisha wavuvi. Katika kitabu cha Historia ya Bukoba, Hans Cory anasema jina Muhaya lilikuwa ni tusi dogo maana wavuvi hawakuwa na mahali pa kudumu pa kuishi na hawakuwa na mali ya kudumu.

Neno Ihaya halikuishia Kyamutwara na Maruku. Ihangiro ya zamani, uligawanyika sehemu mbili: Migongo na Omwihaya.

Kwa hiyo matumizi ya jina Wahaya yalienea hadi Ihangiro. Rekodi za wapelelezi wa Kizungu zinataja jina Buhaya. Omukama Rumanyika Orugundu alimwambia Speke: Mashariki mwa Karagwe kando ya ziwa kunaitwa BUHAYA ni maarufu kwa kilimo cha mibuni na pembe za ndovu. Mwisho wa kunukuu.

Katika vitabu vingine kama vile Victoria Nyanza, Karagwe ina sura yake na eneo lote Mashariki ya Karagwe wanaliita Kiziba.

Athari hiyo bado ipo Baganda huita Wahaya wote Baziba Jina Wahaya linaendana na jina jingine BUKOBA. Bukoba ni sehemu ya ukoo wa ABAKOBA. Ni pale kastamu.

Kwa kweli Bukoba kama eneo walikaa Wavuvi, Abahaya. Kuenea kwa matumizi ya majina Bukoba na Wahaya kuliambana na uvamizi wa wakoloni.

Wajermani walilipanua kujumuisha mji wa Bukoba, baadaye tawala zote za kando ya ziwa. Kwa wakati huo Karagwe haikujumuishwa. Na hata Omukama Ntare wa Karagwe walipomnyonga. Karagwe iliwekwa kwenye usimamizi wa Omukama Kahigi wa Kihanja ila ikabaki inajitegemea."
Nakushauri kasome tena historia vizuri ya mkoa wa Kagera. Wanahistoria wengine wanasema kuwa neno "haya" lilitokana na matatizo ya mawasiliano kati ya wageni/wakoloni wa mwanzo na wenyeji wa mkoa wa Kagera wa wakati huo. Kutokana na matatizo ya lugha ya mawasiliano miongoni mwa wenyeji wa Kagera na wakoloni, wazungu hawa walishangaa kila wakiongea na wenyeji neno "haya" linaloashiria kukubali au kusema "ndiyo" lilijitokeza sana kwa wenyeji wa Muleba, Bukoba Mjini na Vijijini na Karagwe.

Hata hivyo kwa wilaya ya Biharamulo na Ngara ilikuwa tofauti, hawakusikia hili neno "haya". Hawa hawako kwenye kundi la Wahaya kwa utafiti wa wakoloni.

Kwahiyo wazungu hao collectively wakawabatiza wenyeji hawa "Wahaya". Kwahiyo kiuhalisia Kagera hakuna kabila linaitwa wahaya. Wahaya ni mkusanyiko watu wanaojiita WanyaIhangiro (Muleba), Waziba, Wahyoza (Bukoba M/V), Wanyambo (Karagwe) nk. Acha niishie hapa kwa leo.
 
Back
Top Bottom