Si kwamba wanaojiua kutokana na matatizo ama changamoto za kimaisha hawawashirikishi watu

Si kwamba wanaojiua kutokana na matatizo ama changamoto za kimaisha hawawashirikishi watu

TheForgotten Genious

JF-Expert Member
Joined
Jan 18, 2014
Posts
2,087
Reaction score
3,156
Kumekuwa na wimbi kubwa la watu kujiua kwa namna tofautitofauti kutokana na changamoto za kimaisha, ndoa, kiuchumi nk.

Wengi tumekuwa tukisema "Ongeeni na watu" kuhusu matatizo ili pengine yatatuliwe, wanaamini kwamba wahanga hawawashirikishi watu wakati sivyo.

Watu wengi wanafanya maamuzi baada yakuwashirikisha watu wa karibu, ndugu, jamaa na marafiki pasipo msaada na yamkini katika hao wanaoshirikishwa wanakuwa ndio chanzo cha kuchochea maaumivu badala yakutatua.(Sio kwamba hawawashirikishi watu ila watu hawashirikishiki)

Mfano mtu ana matatizo ya kwenye ndoa yanayomtesa, anawashirikisha wazazi na ndugu wengine, badala ya kutatua tatizo wanaanza kuleta yakale ,"ohh tulikwambia hukusikia"na maneno mengine kama hayo.

Una rafiki unamshirikisha jambo ila anaishia kukwambia pole anaendelea na mishe zake na mkiachana wala hakufuatilii, na sio rafiki hata ndugu tu wanakaa kimya hata hawafuatilii,WATU WANASHIRIKISHWA ILA HAWATAKI KUSHIRIKISHIKA! Sasa unakuta mtu ni mwepesi,amekosa option,unafikiri atafanya nini kama sio kuchukua maamuzi magumu?.

Haya mtu anatatizo,ndugu badala yakujadili namna yakutatua tatizo wanaanza kujadili tatizo na maneno chungumzima hawajui namna gani lina muathiri kisaikolojia mhusika,litazame tatizo kwa ufupi kujua asili kisha tafuteni soultion yakulitatua na sio kuitisha vikao vyakukaa kujadili tatizo ni upungufu wa akili kichwani.

MAONI YANGU.

1). Watu wajifunze namna yakukabiliana na nyakati ngumu,wajifunze kitu inaitwa "EMOTION INTELLIGENCE ",usilipe nafasi tatizo liendeshe akili yako bali akili iwe na nafasi yakuliendesha tatizo lako.

2).Matatizo yako hususani yanayohusu madeni ni bora ukazungumza kinaga ubaga na wadeni wako na sio ndugu ama marafiki asilimia kubwa wanaishia kukuumiza tu, (japo si wote).

3).Usiumize kichwa sana kwa kitu ambacho umesha kielezea kwa mtu na hataki kuelewa muache afanye anachotaka maana yeye ndio mwenye maamuzi ya mwisho kwa wakati huo.

4).Usikubali kutoka kwenye focus ya kile unachokiamini na kukipambania kwa sababu ya changamoto unazokutana nazo,maana changamoto sio vitu bali ni watu wanaokuzunguka,wakabili.

5).Usiwe mtu wa rundo la watu wasio na msaada kwako hata kwa mawazo pevu,achana nao haraka.

6).Usipoteze muda kumfikiria mtu aliyegoma kukusaidia wakati anauwezo huo kwa asilimia nyingi,haitakusaidia maana kusaidiwa ni hiari ya mhusika na hailazimishwa.

7).Ifunze akili yako kuvumbua milinganyo mikubwa kwa utulivu.

8).Sio kila kitu chakuwashirikisha watu,maana wanaweza kukikuza wakati hakukuwa na ulazima huo,chuja.

9).Usimlazimishe mtu kukusaidia maana msaada ni hiari.

10).Usiwe mtumwa kwa mtu anayekudai au lah,,atakufanya mtumwa wa fikra.

Mimi nimechagua kuishi Kivyangu maana nitakufa kivyangu,na nina amini kama kuna mtu ataumia baada ya kifo changu ni Wanangu,Mama yangu na mke wangu kama atakuwa ananipenda kweli ,na baada ya kifo changu thamani yangu haitakuwa na utofauti na mzoga wa fisi hata kama nitazikwa kwenye jeneza la mamilioni,naisui kwa falsafa,mifumo na kanuni zangu.

Usipingane na nyakati utaathiri Hatima,zikubari nyakati

MTU AKISHINDWA KUNIELEWA HUWA NA ACHANA NAYE MAPEMA SANA.

MPASI N.A
 
Kuna kitu kikubwa nimekiona hapa JF na kinaumiza sana.. Pengine uongozi wa JamiiForums wakiweza wanaweza kuchukua hatua stahiki kwenye hili

JF imejijengea heshima na kuaminika na wengi mno, hivyo wale ambao wanakumbana na magumu na changamoto za maisha na hawana pa kusemea. Huchagua JF kama sehemu salama na ya kuaminika kwa ajili ya kutua mizigo yao! Si wote wanahitaji misaada ya kifedha la hasha, wengine wanahitaji tu msaada wa mawazo na kutiwa moyo
Hii inawapa faraja kubwa na kujiona kumbe hawajakosea kuja hapa! Neno moja la faraja linaweza kuiponya nafsi iliyokuwa inateketea!

LAKINI sasa!
Wengi waliojaribu kutua mizigo yao hapa wakiamini ni sehemu sahihi na salama wamejikuta wakijuta kuyasema magumu yao maana wamekumbana na matusi, kashfa, kejeli, dhihaka, dharau na mambo mengine ya ajabu kabisa toka kwa baadhi ya member wasiojitambua
 
Ndio watanzania walivyo hasa kina mama,

Wamama wengi wa kitanzania unapo msimulia tatizo lako hukimbilia kusema nilikwambia, ungenisikiliza ingekuwa hivi mara hivi,

Achana na hapo mtanzania mara nyingi akikutana na mwezake mada zao mara nyingi ni matatizo ya wezao, na shida za wezao hiyo haijengi.

Wamama wa kibongo badilikeni
 
Kamwe usikope kama hakuna ulazima, na kama hutaweza kulipa

Usizae kama huwezi kulea

Acha tamaa ya vitu vya watu, wake za watu

Matumizi yasizidi kipato

Usicheze vikoba, vikoba na kifo ni ndugu
Kila mtu huwa na mipango mzuri tu anapoamua kitu iwe kukopa au vp kutokana uelewa wake. Ila kuna mambo huibuka mpaka unashangaa
 
Mimi nimechagua kuishi Kivyangu maana nitakufa kivyangu,na nina amini kama kuna mtu ataumia baada ya kifo changu ni Wanangu,Mama yangu na mke wangu kama atakuwa ananipenda kweli ,na baada ya kifo changu thamani yangu haitakuwa na utofauti na mzoga wa fisi hata kama nitazikwa kwenye jeneza la mamilioni,naisui kwa falsafa,mifumo na kanuni zangu.
Mimi pia mkuu,natazama naishije nitaishije...basss....watu hawaaminiki wala hawana utu.Tujifunze kusimama wenyewe
 
Mimi binafsi zijawahi kuogopa sijui nikifa nitazikwa Nan Nani ,huu naonaga ni ujinga na upumbavu ,ukisha kufaa umekufa uzikwe kama mfalume au uzikwe na manispaaa yote ni kwenda chini tu .....

So ,sinaaga mambo ya kunyenyekea watu ambao naona hawana msaada na Mimi ,sijui kuishi vzuri na watu ....chanzo cha matatizo yote hapa duniani chanzo ni binadamu wenyewe ,maneno ,majungu ,kusemana ,roho mbaya ,.....kiufupi binadamu wengi wanapenda kuona binadamu mwenzio anamatatizo ,ni nature kabisa ....
 
Na namshukuru Mungu kwa hivi nilivyo. Kama nilipoteza ardhi heka kumi na mbili Kigamboni, nikataka kudhulumiwa nyumba Salasala na sikufikiria hata kujidhuru, nini kingine kigeni? Mungu aliyenivusha atanivusha tena
Kidhulumiwa mali bila kugusa nafsi yangu mental sina shinda ntakuacha tu,
ila kuna chagamoto zaidi ya kudhulumiwa mali, Mtu iko tayari awuze mali zake ili wewe ufungwe wakati huna hatia, ndugu zako mama moja na baba moja wana kuzunguka ili wakuumize wewe, mwanao anabakwa na mbakaji anataka akuue wewe pia, police inakata kukusaidia mpaka uwape rushwa hapo mke anaomba talaka, we acha dunia hi kuna mengi
 
Kuna jamaa alikuwa anawacheka sana watu wanaopigiwa wachumba zao na wake zao kitu kama bandarini sikumbuki.
ila jamaa akaja naye kuoa akapigiwa.kilichofata kujiua maana aibu itawekwa wapi
 
Omba Mungu usipate Tatizo/chagamoto kubwa katika maisha yako una tamani uamke usigizini umekufa hamna cho imotional intelligence
Sizungumzi ama kuandika visa vya kufikirika mimi ni mhanga and i know how i survived,hivyo na share kitu nimeweza kufaulu
 
Kuna kitu kikubwa nimekiona hapa JF na kinaumiza sana.. Pengine uongozi wa JamiiForums wakiweza wanaweza kuchukua hatua stahiki kwenye hili

JF imejijengea heshima na kuaminika na wengi mno, hivyo wale ambao wanakumbana na magumu na changamoto za maisha na hawana pa kusemea. Huchagua JF kama sehemu salama na ya kuaminika kwa ajili ya kutua mizigo yao! Si wote wanahitaji misaada ya kifedha la hasha, wengine wanahitaji tu msaada wa mawazo na kutiwa moyo
Hii inawapa faraja kubwa na kujiona kumbe hawajakosea kuja hapa! Neno moja la faraja linaweza kuiponya nafsi iliyokuwa inateketea!

LAKINI sasa!
Wengi waliojaribu kutua mizigo yao hapa wakiamini ni sehemu sahihi na salama wamejikuta wakijuta kuyasema magumu yao maana wamekumbana na matusi, kashfa, kejeli, dhihaka, dharau na mambo mengine ya ajabu kabisa toka kwa baadhi ya member wasiojitambua
Chuja ndugu huwezi kupata positive engage toka kwa kila mtu,na nilazima ukubali kupingwa kuonesha utofauti wako
 
Back
Top Bottom