Si zaidi ya Miaka 20 Ijayo, Tanzania Bara tutaenda kujifunza Zanzibar namna ya kutumia akili kufanya maendeleo

Si zaidi ya Miaka 20 Ijayo, Tanzania Bara tutaenda kujifunza Zanzibar namna ya kutumia akili kufanya maendeleo

Lord denning

JF-Expert Member
Joined
Jun 3, 2015
Posts
15,819
Reaction score
33,255
Wakiwa na rasilimali chache sana, Zanzibar wamegundua ili waweze kuendelea haraka ni vizuri waachane na akili za ki Tanzania Bara.

Sisi tukiwa tunaendekeza ujinga eti uraia pacha utahatarisha usalama wao siku nyingi walishapitisha suala la Diaspora kushiriki kuwa sehemu ya uchumi wa nchi yao.

Tukiwa tunaendekeza ujinga sijui wageni wasiruhisiwe kumiliki ardhi wao siku nyingi walishapitisha suala la wageni kumiliki ardhi na matunda yameanza kuonekana kwenye uchumi wao.

Kwa sasa ukitazama kwa makini kwenye kila kitu Zanzibar wanafanya kwa viwango vya juu sana.

Sisi tukiwa tunapiga lopolopo kujenga miji ya kisasa na makazi bora kwa wananchi, Zanzibar wameanza kutumia fedha wanazopata kuboresha makazi ya wananchi wao kwa kuwajengea nyumba bora kwenye maeneo yaliyopangwa na kujengwa vizuri.

Kinachonifurahisha zaidi Zanzibar hawana madini, hawana gesi, hawana Mbuga za wanyama ila wameamua kutumia akili kufanya mambo ya maana ambayo yanawapa fedha na wanazitumia vizuri.

Kwa hali ilivyo haitazidi miaka 20 Zanzibar itaenda kuwa kama Singapore au Korea Kusini. Nina uhakika baada ya miaka 20 ijayo Tanzania bara tutaenda kujifunza Zanzibar kuhusu namna ya kutumia akili kuvutia mitaji na kufanya maendeleo sahihi na kwa haraka.

FB_IMG_1736344565441.jpg
FB_IMG_1736344534094.jpg
FB_IMG_1736344523845.jpg
Screenshot_20250108_170741_LinkedIn.jpg
 
Wakiwa na rasilimali chache sana, Zanzibar wamegundua ili waweze kuendelea haraka ni vizuri waachane na akili za ki Tanzania Bara.

Sisi tukiwa tunaendekeza ujinga eti uraia pacha utahatarisha usalama wao siku nyingi walishapitisha suala la Diaspora kushiriki kuwa sehemu ya uchumi wa nchi yao.

Tukiwa tunaendekeza ujinga sijui wageni wasiruhisiwe kumiliki ardhi wao siku nyingi walishapitisha suala la wageni kumiliki ardhi na matunda yameanza kuonekana kwenye uchumi wao.

Kwa sasa ukitazama kwa makini kwenye kila kitu Zanzibar wanafanya kwa viwango vya juu sana.

Sisi tukiwa tunapiga lopolopo kujenga miji ya kisasa na makazi bora kwa wananchi, Zanzibar wameanza kutumia fedha wanazopata kuboresha makazi ya wananchi wao kwa kuwajengea nyumba bora kwenye maeneo yaliyopangwa na kujengwa vizuri.

Kinachonifurahisha zaidi Zanzibar hawana madini, hawana gesi, hawana Mbuga za wanyama ila wameamua kutumia akili kufanya mambo ya maana ambayo yanawapa fedha na wanazitumia vizuri.

Kwa hali ilivyo haitazidi miaka 20 Zanzibar itaenda kuwa kama Singapore au Korea Kusini. Nina uhakika baada ya miaka 20 ijayo Tanzania bara tutaenda kujifunza Zanzibar kuhusu namna ya kutumia akili kuvutia mitaji na kufanya maendeleo sahihi na kwa haraka.

View attachment 3195947View attachment 3195948View attachment 3195949View attachment 3195950
Hata Sasa bila Samia huku Bara kuendelea kupauka chini ya yule mtu wao.

Wajamaa na maendeleo wapi na wapi?
 
Kweli wewe utakuwa masikini wa akili Sasa huto tujumba ndo umeona kitu Cha kijufunza
Wanasumbuliwa na wivu pamoja na fitina mbona bara kuna majengo makubwa zaidi ya hayo, angalia maduka na parking ya mlimanicity haipo kuingine roho mbaya ni hatari
 
Maneno ya maskini wa bara hayo. Hamna lolote la maana kazi kuwananga wenzenu wanaofanya vizuri
Sasa hapo kizuri kinachofanyika ni Nini au hizo shule mlikuwa hamna?

Kitu Cha maana alichofanya mwinyi hata Mimi nampongeza ni kuuza visiwa Kwa wazungu wajenge mahoteli
 
Wanasumbuliwa na wivu pamoja na fitina mbona bara kuna majengo makubwa zaidi ya hayo, angalia maduka na parking ya mlimanicity haipo kuingine roho mbaya ni hatari
Mimi Hawa jamaa huwa nawashangaa sana kwanini wanatuchukia badala ya kuwachukia CCM wanao force muungano
 
Kwani kitu gani kina wazuia how diaspora kufanya maendeleo huku makwao???
 
Tuache ushabiki na mihemko, kuiendeleza TzBara si kazi ndogo... Unahitaji nguvu kubwa ya kiuchumi na uwekezaji, TzBara ina eneo kubwa kulinganisha na huko unakosema, pesa nyingi itahitajika kwenye ujenzi wa miundombinu na miradi ya kimkakati
 
Tuache ushabiki na mihemko, kuiendeleza TzBara si kazi ndogo... Unahitaji nguvu kubwa ya kiuchumi na uwekezaji, TzBara ina eneo kubwa kulinganisha na huko unakosema, pesa nyingi itahitajika kwenye ujenzi wa miundombinu na miradi ya kimkakati
Maneno ya wakosaji
 
Back
Top Bottom