Siasa imetumika kwenye vifurushi

Siasa imetumika kwenye vifurushi

kiduni

JF-Expert Member
Joined
Jun 26, 2015
Posts
348
Reaction score
341
Nafikiri sote tunakumbuka kilichofanyika baada ya kupanda kwa gharama za mawasiliano, tulilalamika waziri akijitokeza na kutulaghai yuko pamoja na sisi gharama zitashushwa ifikapo mwezi April cha kushangaza vilibaki vilevile na sisi tukaridhika.

Mwezi April ndo huu gharama zimeongezwa mara dufu, wamekuja kwa style tofauti kidogo ila dhumuni ni lilelile walitangaza ndani ya masaa 24 vifurushi visitishwe jambo ambalo halitatekelezwa tukikaa kimya.

Hakuna ubishi kwa sasa simu ina nafasi kubwa kwenye jamii tunapoongezewa gharama maana yake wanatuongezea ugumu wa maisha binafsi kwa sasa nimelazimika kutumia freebasic ili nisijiumize.

Wito tusiache kuwapigia kelele na tujitahidi kupunguza mapato yao mpaka gharama zishushwe hata vifurushi vilivyopita navyo ghali mno hawayaoni maumivu yetu wenyewe mishahara yao mikubwa na bado wanajilipa posho kwa zao, hawapati maumivu.
 
Dawa ni kususua hivyo vifurushi vyao

Tuone sasa hizo trillion 2 walizoweka kama target kwa kodi ya mlalahoi kama zitafikiwa
 
Huwezi kupandisha gharama za huduma ya mawasiliano kama simu eti ndio uongeze mapato ya serikali, simu ni huduma tena muhimu sana katika maendeleo ya nchi.

Trilioni mbili kwa mwezi hawawezi kuipata kwa njia hiyo wakati hata mzunguko wa pesa ni mdogo.

Wao waachane na upotoshaji wa Magufuli, warudi kwa wafadhili ili watu tupate unafuu wa maisha, wataruhusiwa kukopa kwa riba ndogo na misaada watapewa tena ndio kodi zitapungua kwetu.
 
Dawa ni kususua hivyo vifurushi vyao

Tuone sasa hizo trillion 2 walizoweka kama target kwa kodi ya mlalahoi kama zitafikiwa
Wanapotukamua sana tutaishiwa mwisho wa siku hata 1T haitafika
 
Huwezi kupandisha gharama za huduma ya mawasiliano kama simu eti ndio uongeze mapato ya serikali, simu ni huduma tena muhimu sana katika maendeleo ya nchi.

Trilioni mbili kwa mwezi hawawezi kuipata kwa njia hiyo wakati hata mzunguko wa pesa ni mdogo.

Wao waachane na upotoshaji wa Magufuli, warudi kwa wafadhili ili watu tupate unafuu wa maisha, wataruhusiwa kukopa kwa riba ndogo na misaada watapewa tena ndio kodi zitapungua kwetu.
Hotuba zao zinaonyesha wanataka waendeleze ya Magufuli ina maana wao hawana mawazo mapya
 
Ndungulile ukileta utani utasababisha mambo ya vifurushi kuwa kama bei ya sukari.

Hayati alileta utani kwenye sukari, ona mpaka leo sukari ni mtihani licha ya kuwepo viwanda, sijui miwa ya kutosha n.k
 
Kutoka Gb 3 mpaka Gb 1 kwa bei ile ile ya ya Gb 3 hili ongezeko limekaa kipigaji sana

Hata sijui uzi unahusu nini nimechangia tu.
 
Back
Top Bottom