Siasa ya Afrika inaongozwa na njaa. Hata wapinzani wanatumwa na njaa

The Phylosopher

JF-Expert Member
Joined
Mar 11, 2015
Posts
1,968
Reaction score
2,957
Nimejaribu kufanya tathimini fupi ya namna siasa za bara letu zinavyofanyika, inasikitisha kwamba msukumo mkubwa wa watu kuingia kwenye siasa ni njaa tu.

Nimejaribu kuangalia mataifa yaliyojaribu kubadili vyama, ukweli ni kwamba hakukuwa na jipya malalamiko ya wananchi yalibaki pale pale kama si kuongezeka.

Mifano ya nchi zilizochagua upinzani:

Malawi, Zambia, Kenya, Uganda nk.
Kwenye mataifa yote hayo walichagua upinzani kwa matumaini makubwa sana lakini upinzani uliposhika hatamu wananchi wakagundua wamedanganywa

Wito wangu tuchape kazi siasa ni ajira kuwashabikia sana wanasiasa kujitoa ufahamu ni kujidhalilisha.
 
Hata TANU CCM ya Sasa kilikuwa chama Cha upinzani kipindi Cha mkoloni. Kwa Sasa wamebaki kutukana nonsense wao kwa wao na ufisadi miaka yote.
 
Naunga mkono.

Siasa ni sanaa na vyama vya siasa ni sawa na Kaole group!
 
Nimejaribu kufanya tathimini fupi ya namna siasa za bara letu zinavyofanyika, inasikitisha kwamba msukumo mkubwa wa watu kuingia kwenye siasa ni njaa tu...
hata kama hakuna mabadiliko tunalazimika kuing'oa ccm, hayo mengine yatajulikana mbeleni.
 
Nimejaribu kufanya tathimini fupi ya namna siasa za bara letu zinavyofanyika, inasikitisha kwamba msukumo mkubwa wa watu kuingia kwenye siasa ni njaa tu...
Hii Ni Africa, vita kubwa tulionayo Ni njaa naufukara kuanzia level ya mtu mmojamoja mpaka kitaifa. Nivzur maamuzi ya kila mmoja wetu yabase kwenye hio factor kua kuanzia ndugu madiwani wabunge Marais mawazir nakila tumjuaye Yuko kwenye vita ya njaa kwaajili ya yeye nakizazi chake sio habar yakumtegeme mtu apigane kwaajili yako.

Iwe Ni sayansi dini siasa au utapeli chochote kitatumika muhimu nimatokeo tuu sio njia utakayo tumia
 
hata kama hakuna mabadiliko tunalazimika kuing'oa ccm, hayo mengine yatajulikana mbeleni.
Yawezekana uko sahihi inategemea una nafasi gani kama ni mtu wa mstari wa mbele kwenye chama fulani unakuwa na uhakika kikishika madaraka na wewe una fungu lako lakini kama unatokea ndolezi/kwenye kimondo kama mimi endelea kulima kahawa kwa nguvu msimu wa mavuno uuze ya kutosha
 
W
Wewe ndo mtoa roho,
Hata wewe zamu yako inakuja utainama tu.
 
hawa ccm waliojipa kazi ya kuuza raslimali za nchi kwa maslahi binafsi hawatufai hata kidogo, ni bora kuweka utawala mpya hata kama watakua wabovu.
 
hawa ccm waliojipa kazi ya kuuza raslimali za nchi kwa maslahi binafsi hawatufai hata kidogo, ni bora kuweka utawala mpya hata kama watakua wabovu.
Kwani una uhakika gani kwamba wao hawatauza!? Siji kusahau kijana mmoja alisafiri kwa baiskeli umbali mrefu sana akiwa amevaa skafu na sare za chama fulani pinzani alafu ilikuwa safari ya kutwa nzima akiwa amejaa mabango na mabandiko ya mgombea fulani yaani humwambii kitu, ila baada ya kuikosa nafasi yule mgombea akakikacha chama
 
unadhani wazalendo kama nyerere nchini wameisha? huo mtindio ubongo wa kuamini na wengine wataiba akati hawajepewa madraka ndo kunafanya ccm waendelee kufanya watakavyo
 
Umenena
 
Unahoaja ya msingi sana,
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…