Siasa ya Kutofungamana na upande wowote: Tukilifanya hili Kiuchumi tunaweza faidika kuliko Taifa lolote lile Africa.

Siasa ya Kutofungamana na upande wowote: Tukilifanya hili Kiuchumi tunaweza faidika kuliko Taifa lolote lile Africa.

Lord denning

JF-Expert Member
Joined
Jun 3, 2015
Posts
15,819
Reaction score
33,255
Habari za Jumapili Wanabodi,

Kati ya maeneo ambayo inawezekana Tanzania hatujaweza kuyatumia vizuri kunufaika kiuchumi basi ni hili eneo la Siasa ya kutofungamana na Upande Wowote

Sote tumeona jirani yetu Kenya anavyonufaika na msimamo wake wa wazi wa kuegemea upande wa Magharibi (West) ambapo kwa sasa makampuni makubwa ya Ulaya na Marekani yanafungua Ofisi zake za Afrika nchini Kenya mfano Benki ya JP Morgan, Microsoft, BBC, Google na mengineyo mengi.

Tanzania tunajinasibu sana kuwa na siasa ya kutofungamana na upande wowote ila kiuhalisia tumeegemea sana China ambapo hata hivyo hatujatumia akili zetu vizuri kumfanya hata afungue makampuni yake makubwa nchini kwetu.

China ana benki kubwa kama HSCB ambayo ndiyo inasemwa kuweza kulinganishwa na Benki ya Marekani ya JP Morgan. Ila hadi sasa hatujaweza hata kuwashawishi wafungue tawi lake kwa Afrika hapa Tanzania.

Kwa urusi wanafanya biashara kubwa sana ya Gesi ulaya ila kwetu sisi kila siku tunaagiza mafuta, hatujaweza hata kumshawishi Mrusi kutengeneza mtandao wa usambazaji wa Gesi kwa Tanzania ili tuwe na matumizi ya gesi nchini mwetu na kuondokana na utegemezi wa mafuta kutoka nje ya Tanzania.

Nilitegemea kwa msimamo wetu wa kutofungamana na upande wowote Nchi yetu ndo ingekuwa kinara wa uwekezaji wa mataifa ya Ulaya, Marekani, Urusi na China.

Nilitegemea Makampuni ya Marekani, China, Ulaya na Urusi ndo yangekuwa na uwekezaji mkubwa hapa Tanzania kuliko nchi nyingine yeyote ile kwa sababu sie hatuna upande na tunawakaribisha wote.

Rai yangu kwa think tank wa Tanzania. Acheni kuwaza ndani ya boksi, anzeni kuwaza nje ya boksi. Tanzania inaweza kuwa Economic power kwa Afrika na Dunia endapo mtawaza vizuri na kuendekeza mambo mazito kwa uchumi wetu. Tanzania kulifanyia kazi hili wazo.

Tanzania ndiyo inapaswa kuwa centre ya uwekezaji mkubwa wa Magharibi na Mashariki kwa hapa Africa. Tumieni akili zenu kuwaza vyema kwa faida ya nchi kiuchumi kwa vizazi vingi vijavyo.



Lord Denning
Mwanza.
 
Kenya raia wanaongea siasa zaidi wakati bongo raia wanaongea mpira wa Simba na Yanga zaidi
 
Tulishajiunga na hiyo movement hata kabla uhuru hatujauonja vizuri.

Movement ilikua inaitwa NAM (Non Aligned Movement)
Ni vizuri usome kabla ya ku comment. Uzi unazungumzia namna ya kufaidika na hiyo NAM kiuchumi sio kujiunga
 
Habari za Jumapili Wanabodi,

Kati ya maeneo ambayo inawezekana Tanzania hatujaweza kuyatumia vizuri kunufaika kiuchumi basi ni hili eneo la Siasa ya kutofungamana na Upande Wowote

Sote tumeona jirani yetu Kenya anavyonufaika na msimamo wake wa wazi wa kuegemea upande wa Magharibi (West) ambapo kwa sasa makampuni makubwa ya Ulaya na Marekani yanafungua Ofisi zake za Afrika nchini Kenya mfano Benki ya JP Morgan, Microsoft, BBC, Google na mengineyo mengi.

Tanzania tunajinasibu sana kuwa na siasa ya kutofungamana na upande wowote ila kiuhalisia tumeegemea sana China ambapo hata hivyo hatujatumia akili zetu vizuri kumfanya hata afungue makampuni yake makubwa nchini kwetu.

China ana benki kubwa kama HSCB ambayo ndiyo inasemwa kuweza kulinganishwa na Benki ya Marekani ya JP Morgan. Ila hadi sasa hatujaweza hata kuwashawishi wafungue tawi lake kwa Afrika hapa Tanzania.

Kwa urusi wanafanya biashara kubwa sana ya Gesi ulaya ila kwetu sisi kila siku tunaagiza mafuta, hatujaweza hata kumshawishi Mrusi kutengeneza mtandao wa usambazaji wa Gesi kwa Tanzania ili tuwe na matumizi ya gesi nchini mwetu na kuondokana na utegemezi wa mafuta kutoka nje ya Tanzania.

Nilitegemea kwa msimamo wetu wa kutofungamana na upande wowote Nchi yetu ndo ingekuwa kinara wa uwekezaji wa mataifa ya Ulaya, Marekani, Urusi na China.

Nilitegemea Makampuni ya Marekani, China, Ulaya na Urusi ndo yangekuwa na uwekezaji mkubwa hapa Tanzania kuliko nchi nyingine yeyote ile kwa sababu sie hatuna upande na tunawakaribisha wote.

Rai yangu kwa think tank wa Tanzania. Acheni kuwaza ndani ya boksi, anzeni kuwaza nje ya boksi. Tanzania inaweza kuwa Economic power kwa Afrika na Dunia endapo mtawaza vizuri na kuendekeza mambo mazito kwa uchumi wetu. Tanzania kulifanyia kazi hili wazo.

Tanzania ndiyo inapaswa kuwa centre ya uwekezaji mkubwa wa Magharibi na Mashariki kwa hapa Africa. Tumieni akili zenu kuwaza vyema kwa faida ya nchi kiuchumi kwa vizazi vingi vijavyo.



Lord Denning
Mwanza.
Mimi napata shida kidogo kuhusu mazingira wezeshi ya ufanyaji biashara tunahitaji kuwa na weledi kwenye mazingira wezeshi yenye uwiano ambayo yatawezesha wazawa kufanikiwa, ili isije ikatokea watu wa nchi za nje ndiyo wakatawala, (dominate), vyanzo vyetu vikuu, (njia zetu za), vya uchumi

Neocolonialism will affect business when our national leaders collaborate with foreigner leaders through one's interest, with little concern of national development

Tumekuwa tunashuhudia, Bill Gates na Tony Brayor wakikutana na viongozi wetu kwa siri.

Hoja kuu hapo tusije tukasinzia nchi za Afrika zikatawaliwa hata kiuchumi kwasasa tunatumia bidhaa ambazo nyingi hatuzizalishi, hapa nilipo ninavyoandika, (changia), huu uzi, nguo zote nilizovaa hazijazalishwa nchini
 
Ni vizuri usome kabla ya ku comment. Uzi unazungumzia namna ya kufaidika na hiyo NAM kiuchumi sio kujiunga
Sababu ya kuandika vile ni kama nimesema tunayo kwa muda mkubwa na haijasaidia katika uchumi.
 
Back
Top Bottom