Siasa za Kenya ni usanii mtupu, bora TZ yetu mara 10!

Siasa za Kenya ni usanii mtupu, bora TZ yetu mara 10!

Ndio gharama tulizolipa ili tufike mahali tupo. Kawaida hata kwenu siku mtaamka na kujitambua lazima mtalipa gharama kama za kwetu.
Forget that mzee, sisi sio wa mihemko, we think and analyse things before we act,
A reason why mmeduwaa usiku na mchana kama ni kweli hatukupigana uchaguzi wa 2015..
Sio rahisi kwa mtz atarisk maisha yake na familia yake sababu ya interest za mwanasiasa X..

The way we get candidates is quiet random to the extent that sio rahisi kutokea mgawanyiko kati yetu..
We are matured enough mkuu. Nyie hapo Kenya ni ukabila to the core, mihemko na kukurupuka kwa kwenda mbele, that will never happen in Tz.
 
Ndio gharama tulizolipa ili tufike mahali tupo. Kawaida hata kwenu siku mtaamka na kujitambua lazima mtalipa gharama kama za kwetu.
Sasa MK254, yani kupigana wenye kwa wenye ndio kujitambua ndugu yangu, Mmm, najuwa haya maneno hayatoki moyoni mwako
 
Sasa MK254, yani kupigana wenye kwa wenye ndio kujitambua ndugu yangu, Mmm, najuwa haya maneno hayatoki moyoni mwako

Nahisi utakua unachanganya madawa. Wewe umesema kwetu wanasiasa walitoweka, au kupatikana pembeni mwa barabara.
Nikakuambia hiyo ni gharama ambayo tulilipia ili tufike mahali tupo leo hii.
Watanzania kwa uwoga wenu hamna ubavu wa kulipia gharama kama hiyo. Alijaribu daktari Ulimboka kilichomkuta mbugani akabaki kimyaaaaaaa.
Wakenya walikua wanakutana na kama hayo ya Ulimboka halafu wanakua wajasiri zaidi. Leo hii tuna katiba bora zaidi ya zote Africa, tuna mfumo wa demokrasia bora zaidi, tumefaulu kubadilisha vyama vinavyoongoza sio kama nyie mliopakizwa na kukombwakombwa kwenye chama kimoja tangu mpate uhuru.

Nchi yetu inaongoza ukanda huu wote kwa kila kitu, kiuchumi, kiutaalam, kisiasa, kielimu n.k. kwa sababu tulilipia gharama.
 
Nahisi utakua unachanganya madawa. Wewe umesema kwetu wanasiasa walitoweka, au kupatikana pembeni mwa barabara.
Nikakuambia hiyo ni gharama ambayo tulilipia ili tufike mahali tupo leo hii.
Watanzania kwa uwoga wenu hamna ubavu wa kulipia gharama kama hiyo. Alijaribu daktari Ulimboka kilichomkuta mbugani akabaki kimyaaaaaaa.
Wakenya walikua wanakutana na kama hayo ya Ulimboka halafu wanakua wajasiri zaidi. Leo hii tuna katiba bora zaidi ya zote Africa, tuna mfumo wa demokrasia bora zaidi, tumefaulu kubadilisha vyama vinavyoongoza sio kama nyie mliopakizwa na kukombwakombwa kwenye chama kimoja tangu mpate uhuru.

Nchi yetu inaongoza ukanda huu wote kwa kila kitu, kiuchumi, kiutaalam, kisiasa, kielimu n.k. kwa sababu tulilipia gharama.
Ni ngumu mno ukweli kukubalika,
Tz bado nchi ya giza 80% hawajitambui wala kung'amua mambo
 
Nahisi utakua unachanganya madawa. Wewe umesema kwetu wanasiasa walitoweka, au kupatikana pembeni mwa barabara.
Nikakuambia hiyo ni gharama ambayo tulilipia ili tufike mahali tupo leo hii.
Watanzania kwa uwoga wenu hamna ubavu wa kulipia gharama kama hiyo. Alijaribu daktari Ulimboka kilichomkuta mbugani akabaki kimyaaaaaaa.
Wakenya walikua wanakutana na kama hayo ya Ulimboka halafu wanakua wajasiri zaidi. Leo hii tuna katiba bora zaidi ya zote Africa, tuna mfumo wa demokrasia bora zaidi, tumefaulu kubadilisha vyama vinavyoongoza sio kama nyie mliopakizwa na kukombwakombwa kwenye chama kimoja tangu mpate uhuru.

Nchi yetu inaongoza ukanda huu wote kwa kila kitu, kiuchumi, kiutaalam, kisiasa, kielimu n.k. kwa sababu tulilipia gharama.
Na kwanini tukimbile kwenye kuuwana wakati majibu ya shida zetu tunayo. Unajuwa mara nyingi kwenye debate, ngumi zinaanza pale hoja zinapo kwisha. Kwasababu kama mtu akishindwa kupata ushindi kwa manemo, anatumia silaha zingine kuhakikisha hoja yake ina inashinda. Sasa kama Tanzania hatujaishiwa hoja, mapanga ya nini?

Katiba ya Kenya bado ni haijajibu maswali ya wakenya, iliwekwa kuzuia ukabila, hiyo shida bado ipo. iliwekwa kuondowa rushwa mambo bado ni magumu. Iliwekwa ili watumishi wa umma wawe waaminifu ngoma ipo pale pale.
 
Na kwanini tukimbile kwenye kuuwana wakati majibu ya shida zetu tunayo. Unajuwa mara nyingi kwenye debate, ngumi zinaanza pale hoja zinapo kwisha. Kwasababu kama mtu akishindwa kupata ushindi kwa manemo, anatumia silaha zingine kuhakikisha hoja yake ina inashinda. Sasa kama Tanzania hatujaishiwa hoja, mapanga ya nini?

Katiba ya Kenya bado ni haijajibu maswali ya wakenya, iliwekwa kuzuia ukabila, hiyo shida bado ipo. iliwekwa kuondowa rushwa mambo bado ni magumu. Iliwekwa ili watumishi wa umma wawe waaminifu ngoma ipo pale pale.

Utaendelea kujitoa ufahamu na kujifanya zezeta fulani hivi, lakini najua unanielewa tena vizuri. Hamna sehemu nimeshabikia kuuwana, mara nyingi huwa mnajificha kwa hilo, kila mmoja wenu akihoji mbona mambo hayaendi sawa na kudai katiba anatajiwa amani na mambo ya ugomvi Iraq, Burundi, Somalia na nchi zote zilizoharibika kwa ugomvi wa ndani na kuwekewa hotuba za Nyerere halafu anaishia kuwa kimya.

Nimekuambia gharama tulizolipia ni hizo za baadhi ya viongozi wetu waliothubutu kuhoji pale mwanzo tulipokua chini ya chama kimoja dhalimu, walifanyiwa hayo mliyomfania daktari Ulimboka, lakini wakakomaa tu, wengine wakauawa, wengine hadi leo ni vilema. Lakini walikazana hadi matunda ya mapambano yao tunayaona leo na tunawaenzi kama mashujaa.

Nchi yetu ilikua maskini, enzi za chama kile cha tangia uhuru, kilichotukandamiza miaka yote. Wananchi waliamua kwa kauli moja, viongozi wa upinzani wakakamatwa, wengine tukala mabomu ya machozi kama chakula, binafsi nilikua mwanaharakati kipindi kile. Tulikomaa hadi kikaeleweka, leo hii tunaona maendeleo mengi, najua hatujafika lakini ukilinganisha na maisha ya chini ya chama cha mwanzo, kuna tofauti kubwa.
 
Utaendelea kujitoa ufahamu na kujifanya zezeta fulani hivi, lakini najua unanielewa tena vizuri. Hamna sehemu nimeshabikia kuuwana, mara nyingi huwa mnajificha kwa hilo, kila mmoja wenu akihoji mbona mambo hayaendi sawa na kudai katiba anatajiwa amani na mambo ya ugomvi Iraq, Burundi, Somalia na nchi zote zilizoharibika kwa ugomvi wa ndani na kuwekewa hotuba za Nyerere halafu anaishia kuwa kimya.

Nimekuambia gharama tulizolipia ni hizo za baadhi ya viongozi wetu waliothubutu kuhoji pale mwanzo tulipokua chini ya chama kimoja dhalimu, walifanyiwa hayo mliyomfania daktari Ulimboka, lakini wakakomaa tu, wengine wakauawa, wengine hadi leo ni vilema. Lakini walikazana hadi matunda ya mapambano yao tunayaona leo na tunawaenzi kama mashujaa.

Nchi yetu ilikua maskini, enzi za chama kile cha tangia uhuru, kilichotukandamiza miaka yote. Wananchi waliamua kwa kauli moja, viongozi wa upinzani wakakamatwa, wengine tukala mabomu ya machozi kama chakula, binafsi nilikua mwanaharakati kipindi kile. Tulikomaa hadi kikaeleweka, leo hii tunaona maendeleo mengi, najua hatujafika lakini ukilinganisha na maisha ya chini ya chama cha mwanzo, kuna tofauti kubwa.

Ukiambiwa uchaguwe kuhamia Gaza au Oslo utachaguwa wapi, sisi tuna amani, tumeona wenzetu wengi walioyapata baada ya kuchezea amani. Amani sio bahati, ni kitu kina tengenezwa na binadamu pale anapokuwa na ufahamu wa umuhimu wa amani. Bara la ulaya walionja joto ya vita ya kwanza na ya pili, wakaapa hawato rudia tena, sio kwamba wanauwezo wa kuizuia bali wamejipanga kuvishambulia vishawishi na ndio maana wanakasirika sana waki mwona Putin akitishia kuwarudisha kule kubaya.
 
Kwa political unrest hiyo ni simple, Tanzania, Rome, Norway, Tuvalu, Canada na nyingine nyingi tuu
Mwenye alikudanganya mwambie akuelimishe vyema

Italy has had 13 yrs of civil war post world war 2 and a dictatorship rule upto 1983

Italian Civil war was worse than anything you see in Africa

Below They Hanged someone for being an Italian Republican

1478776663792.png

Below Italians Burning Other italians On their streets during The italian Civil war THAT WAS IN ROME: Mwanzi1

1478776692666.jpg


Kama Tanzania mnajidanganya mtapata Mabadiliko kwa njia ya Amani Mko in ur own delusional bubble blood must spill for Any change to occur!!
 
Ukiambiwa uchaguwe kuhamia Gaza au Oslo utachaguwa wapi, sisi tuna amani, tumeona wenzetu wengi walioyapata baada ya kuchezea amani. Amani sio bahati, ni kitu kina tengenezwa na binadamu pale anapokuwa na ufahamu wa umuhimu wa amani. Bara la ulaya walionja joto ya vita ya kwanza na ya pili, wakaapa hawato rudia tena, sio kwamba wanauwezo wa kuizuia bali wamejipanga kuvishambulia vishawishi na ndio maana wanakasirika sana waki mwona Putin akitishia kuwarudisha kule kubaya.

Ni wazi nikiambiwa nichague kati ya Gaza na Oslo nitachagua Oslo. Lakini pia lazima nijiulize maswali mengi. Ilitokeaje Gaza wakawa hivyo na Oslo wakawa walivyo. Hamna mtu yeyote hupenda fujo au ugomvi, kila mtu anataka akiamka anapiga mishe zake na kugeuza jioni kwenda kwa watoto wake wanakula na kunywa.

Kule Oslo unakuta wanalinda amani sio kwa maneno na hotuba za waasisi wao tu, bali kwa vitendo. Wanapiga vita ufisadi, wanaruhusiwa uhuru wa kujieleleza, wameboresha mifumo yao kiasi kwamba mwananchi itakua ujinga akitaka kuharibu. Lakini hapa Afrika, unakuta nchi ina raslimali nyingi, umaskini upo kila mahali wa kutupwa, mafisadi wanaitafuna nchi hadi maisha kitaa yanakua magumu balaa, lakini ukihoji kunani unaambiwa amani na kuwekewa hotuba za muasisi wa nchi ili utulie na kuwa kimya. Na ukizingua kuhoji zaidi basi unatulizwa na kuzimwa kibabe na ndio maana miafrika tutazidi kuishi kama tuliolaaniwa vile.

Kenya tulizoea kuishi hivyo kwa kuzimwa zimwa kila tulipohoji, lakini ikafikia mahala ikabidi tukomae, maana hapakua na jinsi. Watu walijitokeza barabarani kupinga udhalimu na unyanyasaji. Tukapigwa mabomu ya machozi, marisasi, viongozi wa upinzani baadhi yao wakazimwa na kulemazwa...yaani Kiafrika Afrika vile... lakini tukakomaa tu hadi kikaeleweka. Hatujafika tunakotaka kwenda, lakini hatua tumepiga za kweli.

Hivyo amani ni tamu, tunaipenda sote, lakini pia ukiwa hapo juu hakikisha unailinda kwa kunihakikishia niliye chini nitaishi nikifurahia matunda ya bidii yangu bila unyanyasaji. Ni formula rahisi sana, haihitaji kuumiza akili.
 
Mwenye alikudanganya mwambie akuelimishe vyema

Italy has had 13 yrs of civil war post world war 2 and a dictatorship rule upto 1983

Italian Civil war was worse than anything you see in Africa

Below They Hanged someone for being an Italian Republican

View attachment 432099
Below Italians Burning Other italians On their streets during The italian Civil war THAT WAS IN ROME: Mwanzi1

View attachment 432100

Kama Tanzania mnajidanganya mtapata Mabadiliko kwa njia ya Amani Mko in ur own delusional bubble blood must spill for Any change to occur!!
Hiyo Italy ilikuwa mtego kumbe na wewe unasomaga hukurupuki, but kwa sisi Tanzania tuna mifano mingi ya kujifunza kuhusi kulinda amani. Matunda yake tunayajuwa, hata Uhuru wetu tulijuwa jinsi ya "kula na kipofu" waingereza wakasema isiwe tatu, have your damn freedom. Mataifa makubwa kama USA yanashindwa kufanya tunacho kufanya Tanzania, haijalishi dini yako, rangi ya ngozi, lugha, kipato wala sehemu unayo ishi, we all have a short on this thing called Tanzania.
 
Ni wazi nikiambiwa nichague kati ya Gaza na Oslo nitachagua Oslo. Lakini pia lazima nijiulize maswali mengi. Ilitokeaje Gaza wakawa hivyo na Oslo wakawa walivyo. Hamna mtu yeyote hupenda fujo au ugomvi, kila mtu anataka akiamka anapiga mishe zake na kugeuza jioni kwenda kwa watoto wake wanakula na kunywa.

Kule Oslo unakuta wanalinda amani sio kwa maneno na hotuba za waasisi wao tu, bali kwa vitendo. Wanapiga vita ufisadi, wanaruhusiwa uhuru wa kujieleleza, wameboresha mifumo yao kiasi kwamba mwananchi itakua ujinga akitaka kuharibu. Lakini hapa Afrika, unakuta nchi ina raslimali nyingi, umaskini upo kila mahali wa kutupwa, mafisadi wanaitafuna nchi hadi maisha kitaa yanakua magumu balaa, lakini ukihoji kunani unaambiwa amani na kuwekewa hotuba za muasisi wa nchi ili utulie na kuwa kimya. Na ukizingua kuhoji zaidi basi unatulizwa na kuzimwa kibabe na ndio maana miafrika tutazidi kuishi kama tuliolaaniwa vile.

Kenya tulizoea kuishi hivyo kwa kuzimwa zimwa kila tulipohoji, lakini ikafikia mahala ikabidi tukomae, maana hapakua na jinsi. Watu walijitokeza barabarani kupinga udhalimu na unyanyasaji. Tukapigwa mabomu ya machozi, marisasi, viongozi wa upinzani baadhi yao wakazimwa na kulemazwa...yaani Kiafrika Afrika vile... lakini tukakomaa tu hadi kikaeleweka. Hatujafika tunakotaka kwenda, lakini hatua tumepiga za kweli.

Hivyo amani ni tamu, tunaipenda sote, lakini pia ukiwa hapo juu hakikisha unailinda kwa kunihakikishia niliye chini nitaishi nikifurahia matunda ya bidii yangu bila unyanyasaji. Ni formula rahisi sana, haihitaji kuumiza akili.
Unaongea upuuzi mtupu, machafuko yenu yote ni ya kikabila na sio kupigania haki. Hadi leo hii bado mnapigwa mabomu na polisi mkiandamana, ufisadi umetamalaki Kenya na kila aina ya ujinga mnafanyiwa na serikali yenu. Umeamua kujitoa akili ili kujifurahisha.
 
Ni wazi nikiambiwa nichague kati ya Gaza na Oslo nitachagua Oslo. Lakini pia lazima nijiulize maswali mengi. Ilitokeaje Gaza wakawa hivyo na Oslo wakawa walivyo. Hamna mtu yeyote hupenda fujo au ugomvi, kila mtu anataka akiamka anapiga mishe zake na kugeuza jioni kwenda kwa watoto wake wanakula na kunywa.

Kule Oslo unakuta wanalinda amani sio kwa maneno na hotuba za waasisi wao tu, bali kwa vitendo. Wanapiga vita ufisadi, wanaruhusiwa uhuru wa kujieleleza, wameboresha mifumo yao kiasi kwamba mwananchi itakua ujinga akitaka kuharibu. Lakini hapa Afrika, unakuta nchi ina raslimali nyingi, umaskini upo kila mahali wa kutupwa, mafisadi wanaitafuna nchi hadi maisha kitaa yanakua magumu balaa, lakini ukihoji kunani unaambiwa amani na kuwekewa hotuba za muasisi wa nchi ili utulie na kuwa kimya. Na ukizingua kuhoji zaidi basi unatulizwa na kuzimwa kibabe na ndio maana miafrika tutazidi kuishi kama tuliolaaniwa vile.

Kenya tulizoea kuishi hivyo kwa kuzimwa zimwa kila tulipohoji, lakini ikafikia mahala ikabidi tukomae, maana hapakua na jinsi. Watu walijitokeza barabarani kupinga udhalimu na unyanyasaji. Tukapigwa mabomu ya machozi, marisasi, viongozi wa upinzani baadhi yao wakazimwa na kulemazwa...yaani Kiafrika Afrika vile... lakini tukakomaa tu hadi kikaeleweka. Hatujafika tunakotaka kwenda, lakini hatua tumepiga za kweli.

Hivyo amani ni tamu, tunaipenda sote, lakini pia ukiwa hapo juu hakikisha unailinda kwa kunihakikishia niliye chini nitaishi nikifurahia matunda ya bidii yangu bila unyanyasaji. Ni formula rahisi sana, haihitaji kuumiza akili.

Hizo hotuba na mambo mengine ni silaha baridi ya kuwatoa watu jazba. Mtu anaenda kanisani au msikitini kusikiliza neno linalompa faraja au amani moyoni. Akitoka huko ni mara chache ataenda kutafuta ugomvi. (Japo wale Al Shabaan wanaenda msikitini kwa nia tofauti lakini hayo ni mengine) Tatizo Kenya sio kama mmeamka na sasa mnajuwa kudai haki yenu, mnafanya hivyo kwasababu viongozi wenu hawasikilizi, kila mara wananchi wakipiga kelele rushwa, au hakuna kazi, au bei ya chakula imepanda, viongozi wanaziba masiko huku wakisali watu wasahau haraka na kurudisha makazini. Ndio maana watu wanachoka wanaamuwa kuingia mtaani. Lakini kama Kenya mgekuwa mmewalea watu wenu kwa kutumia silaha baridi sidhani kama serikali isingezitumia pale inapotakikana.

Angilia nchi kubwa kama Marekani, wamemaliza uchaguzi mkubwa wenye jazba nyingi, lakini haraka haraka pande zote mbili wameingia kwenye mapatano (reconciliation). Wanjuwa kama wakizubaa kidigo tuu, nchi italipuka na mlipuko huo utakuwa na madhara makubwa ya kiuchumi na kitaifa kwa ujumla. Kwa upande wa Kenya, kuna vitu vinakwenda tangu wakati wa mkoloni ambavyo havija ongelewa wala kuguswa. Huwezi kuwa na amani kama bado una makando kando.
 
Nawaona wazalendo wa kikenya wakijitahidi kuleta hoja mfu. Ni hivi mazee wa Kenya, issue nzima inarudi kwenye root, baba wa taifa la Tz alikuwa genious, baba wa taifa la kenya alikuwaaa, tuseme a tribalist business oriented man.
You see, sasa kila taifa limekuwa kutokana na misingi ya hao waanzilishi.
So you guys from that perspective your country is fvcked up from the beginning, Kenyatta alikaribisha wazungu zaidi kuja kujimilikisha maardhi, Nyerere aliwatimua akataifisha mali, mashamba yao wananchi wakayachukua, Nyerere alihakikisha umoja kwanza unakuwepo Tz, Jomo alihakikisha english ndio lugha ya taifa, he had little concerns about tribalism, na msimlaumu sana Jomo, kuna yule judge i thnk, sijui Njoronge, yule alikuwa mshauri mkubwa sana wa Jomo, na you know his views about Africans and former EAC etc, he was fvcked up as wello.

Kwa iyo mbongo haoni sababu ya yeye kwenda kujitoa maisha kisa mwanasiasa, because many people can afford life somehow, kuliko kwenda kuwekea vifua wanasiasa.
Ila Kenya sasa shiidaa mingi kwa walio wengi, to the extent kujitoa mhanga ni kazi ndogo tu, dakika sifuri.

So i understand juacali, MK254 huyo anajipiga piga kifua tu kama kawaida yake, huyu bado anataka Uhuru na jubilee ashinde. Mnufaikaji mkubwa wa mfumo huyu bwana.
 
Hizo hotuba na mambo mengine ni silaha baridi ya kuwatoa watu jazba. Mtu anaenda kanisani au msikitini kusikiliza neno linalompa faraja au amani moyoni. Akitoka huko ni mara chache ataenda kutafuta ugomvi. (Japo wale Al Shabaan wanaenda msikitini kwa nia tofauti lakini hayo ni mengine) Tatizo Kenya sio kama mmeamka na sasa mnajuwa kudai haki yenu, mnafanya hivyo kwasababu viongozi wenu hawasikilizi, kila mara wananchi wakipiga kelele rushwa, au hakuna kazi, au bei ya chakula imepanda, viongozi wanaziba masiko huku wakisali watu wasahau haraka na kurudisha makazini. Ndio maana watu wanachoka wanaamuwa kuingia mtaani. Lakini kama Kenya mgekuwa mmewalea watu wenu kwa kutumia silaha baridi sidhani kama serikali isingezitumia pale inapotakikana.

Angilia nchi kubwa kama Marekani, wamemaliza uchaguzi mkubwa wenye jazba nyingi, lakini haraka haraka pande zote mbili wameingia kwenye mapatano (reconciliation). Wanjuwa kama wakizubaa kidigo tuu, nchi italipuka na mlipuko huo utakuwa na madhara makubwa ya kiuchumi na kitaifa kwa ujumla. Kwa upande wa Kenya, kuna vitu vinakwenda tangu wakati wa mkoloni ambavyo havija ongelewa wala kuguswa. Huwezi kuwa na amani kama bado una makando kando.

Umesababisha nicheke hapa kama chizi uliposema suala la viongozi kuskliza hapa Afrika. Unataka kujidanganya na kujiaminisha eti Afrika kuna viongozi waskifu bila kukemewa kwa nguvu. Eti kwamba viongozi wa Tanzania ndio huwaskliza wananchi wake, hicho ni kicheko balaa.

Viongozi wenu wapo wanapeta hata baada ya kuitafuna nchi miaka nenda miaka rudi, kisa hawajakemewa halafu nyie mna hulka ya uwoga uwoga. Nimesoma historia yenu vizuri na pia kuishi kwenu, kidogo wakati wa Nyerere kwenye suala la kukemea ufisadi mlijaribu. Nyerere alikemea sana na kupiga ufisadi kwa matendo, lakini siku hizi mumejaa fisi watupu huko juu, kutafuna hadi mnabaki mahandaki matupu, na wananchi wanapohoji mbona nchi inaliwa hivi mnawawekea hotuba za Nyerere na kuwazima halafu hata bila aibu unalinganisha na ibada ya kanisani.

Hauwezi linganisha nchi za Kiafrika na Marekani au hata hiyo Norway, wale wana demokrasia ya kweli mambo wanayaona ya kweli. Hata hao waliojitokeza kuandamana kisa Trump amechaguliwa, walifanya hivyo kwa kumchukia Trump lakini sio kwamba kura ziliibiwa, wanajua fika uchaguzi ulikua wa haki, lakini imewauma tu kwamba Wamarekani wenzao walimchagua Trump.
Sasa ije Afrika, watu huwa tunaandamana kwa kulalamika dhidi ya wizi wa kura au mambo yasio ya haki mfano wa yale mliyafanya Zanzibar hadi mkaanza kunyimwa misaada. Ni vigumu sana uchaguzi kukamilika Afrika bila upande ulioshindwa kulalamika, Tanzania kiongozi wa upinzani bwana Lowassa aliongea kwa machungu sana kuwa kaibiwa kura, akajaribu kuwasilisha ushahidi kwa Lubuva akazimwa. Ndio hizo za Afrika, hamna nini wala nini, ni ubabe kwenda mbele.

Magufuli kidogo amekuja kwa ukali ukali wa kukemea rushwa na ufisadi, japo akapiga brake na kusema hatafukua makaburi ya zamani, hivyo ufisadi wote wa hapo awali inawezekana akaachia tu, mambo kama ya IPTL, Escrow n.k. Lakini hata hivyo kwenye awamu yake hii bado kuna chembe chembe za ufisadi zinazotajwa, kwa mfano juzi nimesoma sehemu wabunge wa CCM wamegawana mamilioni pesa za umma ili kupitisha hoja fulani. Hayo ni mambo ya aibu ya Kiafrika ambayo hutakaa ulinganishe na wenzetu wa Ulaya hata kidogo.
 
Umesababisha nicheke hapa kama chizi uliposema suala la viongozi kuskliza hapa Afrika. Unataka kujidanganya na kujiaminisha eti Afrika kuna viongozi waskifu bila kukemewa kwa nguvu. Eti kwamba viongozi wa Tanzania ndio huwaskliza wananchi wake, hicho ni kicheko balaa.

Viongozi wenu wapo wanapeta hata baada ya kuitafuna nchi miaka nenda miaka rudi, kisa hawajakemewa halafu nyie mna hulka ya uwoga uwoga. Nimesoma historia yenu vizuri na pia kuishi kwenu, kidogo wakati wa Nyerere kwenye suala la kukemea ufisadi mlijaribu. Nyerere alikemea sana na kupiga ufisadi kwa matendo, lakini siku hizi mumejaa fisi watupu huko juu, kutafuna hadi mnabaki mahandaki matupu, na wananchi wanapohoji mbona nchi inaliwa hivi mnawawekea hotuba za Nyerere na kuwazima halafu hata bila aibu unalinganisha na ibada ya kanisani.

Hauwezi linganisha nchi za Kiafrika na Marekani au hata hiyo Norway, wale wana demokrasia ya kweli mambo wanayaona ya kweli. Hata hao waliojitokeza kuandamana kisa Trump amechaguliwa, walifanya hivyo kwa kumchukia Trump lakini sio kwamba kura ziliibiwa, wanajua fika uchaguzi ulikua wa haki, lakini imewauma tu kwamba Wamarekani wenzao walimchagua Trump.
Sasa ije Afrika, watu huwa tunaandamana kwa kulalamika dhidi ya wizi wa kura au mambo yasio ya haki mfano wa yale mliyafanya Zanzibar hadi mkaanza kunyimwa misaada. Ni vigumu sana uchaguzi kukamilika Afrika bila upande ulioshindwa kulalamika, Tanzania kiongozi wa upinzani bwana Lowassa aliongea kwa machungu sana kuwa kaibiwa kura, akajaribu kuwasilisha ushahidi kwa Lubuva akazimwa. Ndio hizo za Afrika, hamna nini wala nini, ni ubabe kwenda mbele.

Magufuli kidogo amekuja kwa ukali ukali wa kukemea rushwa na ufisadi, japo akapiga brake na kusema hatafukua makaburi ya zamani, hivyo ufisadi wote wa hapo awali inawezekana akaachia tu, mambo kama ya IPTL, Escrow n.k. Lakini hata hivyo kwenye awamu yake hii bado kuna chembe chembe za ufisadi zinazotajwa, kwa mfano juzi nimesoma sehemu wabunge wa CCM wamegawana mamilioni pesa za umma ili kupitisha hoja fulani. Hayo ni mambo ya aibu ya Kiafrika ambayo hutakaa ulinganishe na wenzetu wa Ulaya hata kidogo.


Angalau hata mimi nimekuchekesha kuliko wale watanzania wanao watowa jasho hapa. Sasa kwa kicheko hicho shushua kahawa bora ya Kilimajaro au Konyagi safi ya Tanzania.

kwa ueleo wako utalinganisha ufisadi wa kenya na Tanzania? kenya nchi ina kopa mamilioni toka nje halafu hela wanagawana wakubwa huku siku ya kulipa wakenya wote wanalipishawa. Ufisadi Tanzania ulijitokeza wakati ya Mkapa na Kikwete, wenzenu tumesha badili gia na wewe unalijuwa hilo. Ukija kwenye issue ya CCM mamilioni waliogawana, unacheza kwenye karata za upinzani wa Tanzania kuaminisha watu pasipo na ushahidi. Na unafikiri upinzani wa Tanzania walijifunzia wapi kudangaya wananchi kama sio kenya? uchaguzi ulio pita wakenya wali jaa Tanzania wakiwafundisha upinzania tabia zao mbaya za wizi wizi. wengine tukaona janja yenu tukapiga mtu chini. ukija kenye ufisadi wa Tanzania, utakuta kuna mikono ya kenya ndani ya ufisadi huo. kama sio benki basi mfanyabiashara fulani katia mkono. Wanachi wakenya wako radhi kuandamana na kupigana na polisi hadi kufa kwasababu hakuna namna nyingine ya kutatuwa matatizo yao. Tanzania unaweza ukawa masikini wa kutupa lakini una uwezo wakumuona waziri na akakusikiliza, au hata ukanya naye chai, Mwabie waziri kenya excuse me please... hujamaliza kusema please uko jela na mlango unafungwa Pwaaaa.
 
Angalau hata mimi nimekuchekesha kuliko wale watanzania wanao watowa jasho hapa. Sasa kwa kicheko hicho shushua kahawa bora ya Kilimajaro au Konyagi safi ya Tanzania.

kwa ueleo wako utalinganisha ufisadi wa kenya na Tanzania? kenya nchi ina kopa mamilioni toka nje halafu hela wanagawana wakubwa huku siku ya kulipa wakenya wote wanalipishawa. Ufisadi Tanzania ulijitokeza wakati ya Mkapa na Kikwete, wenzenu tumesha badili gia na wewe unalijuwa hilo. Ukija kwenye issue ya CCM mamilioni waliogawana, unacheza kwenye karata za upinzani wa Tanzania kuaminisha watu pasipo na ushahidi. Na unafikiri upinzani wa Tanzania walijifunzia wapi kudangaya wananchi kama sio kenya? uchaguzi ulio pita wakenya wali jaa Tanzania wakiwafundisha upinzania tabia zao mbaya za wizi wizi. wengine tukaona janja yenu tukapiga mtu chini. ukija kenye ufisadi wa Tanzania, utakuta kuna mikono ya kenya ndani ya ufisadi huo. kama sio benki basi mfanyabiashara fulani katia mkono. Wanachi wakenya wako radhi kuandamana na kupigana na polisi hadi kufa kwasababu hakuna namna nyingine ya kutatuwa matatizo yao. Tanzania unaweza ukawa masikini wa kutupa lakini una uwezo wakumuona waziri na akakusikiliza, au hata ukanya naye chai, Mwabie waziri kenya excuse me please... hujamaliza kusema please uko jela na mlango unafungwa Pwaaaa.

Hehehe! Eti Kenya utatiwa ndani kwa kumwamkua waziri, jameni Watanzania huwa mumeaminishwa mambo ya kiajabu ajabu ya Kikenya. Kuna wakati huwa nikiwa Tanzania halafu nawaskliza vijiweni mkiijadili Kenya bila kunishtukia kwamba mimi Mkenya, yaani vioja, sijui nani kawahubiria na kuwaaminisha hayo yote huwa nawaskia mkiyasema kuhusu Kenya na Wakenya.

Anyway, ukirejelea mada, kwenye masuala ya ufisadi, hamna sehemu nimesema kwamba Kenya hakuna ufisadi. Upo tena maeneo mengi, pamoja na kwamba tumewekeza sana kwenye mifumo. Fahamu kwamba Kenya ilianza kibepari, watu walijua hela tangu hapo awali na rais muasisi wa taifa letu kaendekeza ufisadi na ukabila. Hivyo sio kazi rahisi kuufuta huo mfumo wote, ni hatua kwa hatua. Lakini Tanzania, mlianza kiujamaa, ambapo mfumo wenyewe unapunguza tamaa ila unalemaza uwezo wa watu kutumia akili na kujituma. Wanakua wazembe na kutegemeana bila kuloa jasho, ikawafanya muwe maskini sana hadi mnakuja kubadilisha wakati Nyerere ananyanyua miko na kuachia, mlikua mumeisha kabisa, umaskini ulikua umewatafuna.

Tatizo sasa mliingia kwenye mfumo wa ubepari bila kujifunza kwa hatua, mkaanza kwa pupa, mafisadi mkaanza kuitafuna nchi, vitalu vya madini vikaanza kubaki mahandaki. Mkaanza kutafuna kila kitu kwa pupa, hadi inatajwa eti mnasafirisha meno ya tembo na twiga kwa ndege ya rais. Yaani ikawa yote ruksa, kula huku kula kule, wengine wanawatambia wenzao eti hela ya mboga, mara chenji, mara nyoka mwenye makengeza. Yaani vituko vya wizi kweli kweli, na kila wananchi wakihoji wanawekewa hotuba za Nyerere halafu wanabaki kimya.

Halafu unasema mamilioni waliyogawana wabunge wa CCM kwamba ni propaganda za upinzani, sasa mbona hata katibu wa CCM Bunge mwenyewe alikiri, hebu fuata hii link uone wenzio ambao hawakupata mgao wanavyolalamika Wabunge wa CCM wagawana hela za CCM, Je wanachama tutagawiwa lini?
 
Hehehe! Eti Kenya utatiwa ndani kwa kumwamkua waziri, jameni Watanzania huwa mumeaminishwa mambo ya kiajabu ajabu ya Kikenya. Kuna wakati huwa nikiwa Tanzania halafu nawaskliza vijiweni mkiijadili Kenya bila kunishtukia kwamba mimi Mkenya, yaani vioja, sijui nani kawahubiria na kuwaaminisha hayo yote huwa nawaskia mkiyasema kuhusu Kenya na Wakenya.

Anyway, ukirejelea mada, kwenye masuala ya ufisadi, hamna sehemu nimesema kwamba Kenya hakuna ufisadi. Upo tena maeneo mengi, pamoja na kwamba tumewekeza sana kwenye mifumo. Fahamu kwamba Kenya ilianza kibepari, watu walijua hela tangu hapo awali na rais muasisi wa taifa letu kaendekeza ufisadi na ukabila. Hivyo sio kazi rahisi kuufuta huo mfumo wote, ni hatua kwa hatua. Lakini Tanzania, mlianza kiujamaa, ambapo mfumo wenyewe unapunguza tamaa ila unalemaza uwezo wa watu kutumia akili na kujituma. Wanakua wazembe na kutegemeana bila kuloa jasho, ikawafanya muwe maskini sana hadi mnakuja kubadilisha wakati Nyerere ananyanyua miko na kuachia, mlikua mumeisha kabisa, umaskini ulikua umewatafuna.

Tatizo sasa mliingia kwenye mfumo wa ubepari bila kujifunza kwa hatua, mkaanza kwa pupa, mafisadi mkaanza kuitafuna nchi, vitalu vya madini vikaanza kubaki mahandaki. Mkaanza kutafuna kila kitu kwa pupa, hadi inatajwa eti mnasafirisha meno ya tembo na twiga kwa ndege ya rais. Yaani ikawa yote ruksa, kula huku kula kule, wengine wanawatambia wenzao eti hela ya mboga, mara chenji, mara nyoka mwenye makengeza. Yaani vituko vya wizi kweli kweli, na kila wananchi wakihoji wanawekewa hotuba za Nyerere halafu wanabaki kimya.

Halafu unasema mamilioni waliyogawana wabunge wa CCM kwamba ni propaganda za upinzani, sasa mbona hata katibu wa CCM Bunge mwenyewe alikiri, hebu fuata hii link uone wenzio ambao hawakupata mgao wanavyolalamika Wabunge wa CCM wagawana hela za CCM, Je wanachama tutagawiwa lini?

Unaona eh, na wewe umesha anza kuamini hadhithi za kupika na kukanga za Chadema, kwanza hakuna cheo kinaitwa Katibu wa CCM Bunge. Hii ni hadhithi tuu, hata nilisha iandika humu kwenye thread zingine. Kwani kuna tatizo gani ccm akiwapa wabunge wake hela? hela ni za ccm sio za serikali wala za wananchi. Kama Chadama inaweza kuwa motivate wabunge wake iwape.

Anyway back to mada, sio kweli kwaba ujamaa ndio ulifanaya Tanzania kushuka kiuchimi nilitegemea ulie soma historia ya Tanzania ungejuwa ilikuwaje. Tanzania ilikuwa nchi iliyojiweka kati kati ya cold war. Nchi ilijikuta inasogea sana upande wa mashariki ambapo marafiki wakubwa walikua China, Russia, North Korea hata Cuba. Wa magharibi hawakulipenda hilo ukilinganisha tulikuwa tunapigana kukomboa mataifa ya kusini mwa Afrika na wao huko ndio kulikuwa ngome wazungu wa magharibi. Kwasababu tulikuwa marafiki wakubwa China na Russian hawakuweza kutuvamia kwasababu hawataki vita karibu na ngome yao nyingine Kenya. Nyerere alilijuwa hilo na akatumia vizuri mwamvuli wa Kenya. Lakini waliweza kutuzamisha kiuchumi, huku tuna vita ya Uganda, taifa linahitaji hela na silaa tukakopa. Upande mwingine tunapigana vita kusini mwa Afrika huku tunaangaika na uchumi, huku tunajanga jina kimataifa. Lazima uende kimoja kitakuponyoka, baada ya yote hayo inabidi tujipange upyawati Kenya mnakula maraha sisi tunajifunza kuwa wajasiri kama nchi. Sio kwamba Tanzania tumeingia ubepari halafu hatuujuwi, ubepari wetu umechaganyika na ujamaa, kwamba kila mtu afaidike na zao la nchi. Kutoka wa chini kabisa hadi wa juu, kitu ambacho wakenya maskini wamelili weeeeeeee!!!!!!! mpaka machozi yamekauka.
 
Unaona eh, na wewe umesha anza kuamini hadhithi za kupika na kukanga za Chadema, kwanza hakuna cheo kinaitwa Katibu wa CCM Bunge. Hii ni hadhithi tuu, hata nilisha iandika humu kwenye thread zingine. Kwani kuna tatizo gani ccm akiwapa wabunge wake hela? hela ni za ccm sio za serikali wala za wananchi. Kama Chadama inaweza kuwa motivate wabunge wake iwape.

Anyway back to mada, sio kweli kwaba ujamaa ndio ulifanaya Tanzania kushuka kiuchimi nilitegemea ulie soma historia ya Tanzania ungejuwa ilikuwaje. Tanzania ilikuwa nchi iliyojiweka kati kati ya cold war. Nchi ilijikuta inasogea sana upande wa mashariki ambapo marafiki wakubwa walikua China, Russia, North Korea hata Cuba. Wa magharibi hawakulipenda hilo ukilinganisha tulikuwa tunapigana kukomboa mataifa ya kusini mwa Afrika na wao huko ndio kulikuwa ngome wazungu wa magharibi. Kwasababu tulikuwa marafiki wakubwa China na Russian hawakuweza kutuvamia kwasababu hawataki vita karibu na ngome yao nyingine Kenya. Nyerere alilijuwa hilo na akatumia vizuri mwamvuli wa Kenya. Lakini waliweza kutuzamisha kiuchumi, huku tuna vita ya Uganda, taifa linahitaji hela na silaa tukakopa. Upande mwingine tunapigana vita kusini mwa Afrika huku tunaangaika na uchumi, huku tunajanga jina kimataifa. Lazima uende kimoja kitakuponyoka, baada ya yote hayo inabidi tujipange upyawati Kenya mnakula maraha sisi tunajifunza kuwa wajasiri kama nchi. Sio kwamba Tanzania tumeingia ubepari halafu hatuujuwi, ubepari wetu umechaganyika na ujamaa, kwamba kila mtu afaidike na zao la nchi. Kutoka wa chini kabisa hadi wa juu, kitu ambacho wakenya maskini wamelili weeeeeeee!!!!!!! mpaka machozi yamekauka.

Hapo ndio huwa mnachanganya changanya, wengi mnaijadili historia ya nchi yenu kwa kutegemea mambo ya vijiweni lakini sio kwa kuisoma ilivyo. Vita dhidi ya Id Amin viltendeka juzi sana 1978. Japo nakubali ni mojawapo wa sababu za umaskini wenu.

Tatizo mlijiingiza katika kila ugomvi Afrika, mkamchokonoa Id Amin kwa kuwalea waasi wake akina Museveni. Mzungu anasema pick your fights well, sio kuingia katika kila ugomvi na vurugu kisa uonekane mbabe. Mkaiga Mrusi eti kutunisha misuli dhidi ya Muingereza na Mumarekani ilihali leo hii hao hao Waingereza na Wamarekani ndio mnawazungushia vibakuli vya misaada.

Hauwezi ukafanya experiments za hivyo huku ukitumia watu wako maskini ilhali nchi yako hujaiboresha kiuchumi. Utaishia kuwalemaza watu wako.

Halafu hilo la umaskini huwa naona mnapenda kuimba kwamba Tanzania maskini wake wanaishi kwa raha na eti sio wengi. Tatizo huwa wengi wenu hamjui na wala hamsomi taarrifa, mnaishi kwa kujidanganya na kudanganywa na wanasiasa. Fuata vizuri takwimu, na ujue kudadavua data kisayansi, leo hii
- Tanzania ina njaa zaidi ya Kenya - hili tuliwahi kulijadili huku Mataifa majirani wa Kenya wana njaa zaidi yetu
- Tanzania ina raia wengi maskini zaidi ya Kenya, kulingana na takwimu za Benki kuu ya dunia 70% ya Watanzania ni maskini wanaoishi chini ya $2
 
Back
Top Bottom