Si mlikuwa mnamsingizia Magufuri kuwa ana uhusiano na majirani? Sasahivi lawama mnamtwisha nani! maana mwenye kubebeshwa mabaya yote hayupo.Mwambieni Samia maana alituambia amefungua Nchi
Akina Hamza wa ccm??Timu gaidi watashangilia
Kila mtu ashinde mechi zake Go go Haikainde30 September 2021
HAIKANDE HICHILEMA - NO TIMBER LICENSE FOR FOREIGNERS
Licences will go to Zambians , no timber licence for foreigners says President Haikande Hichilema of Zambia
Source : LITOVIA TV
Nini hasa hoja yako? Kwamba jamaa ni muongo au?Bila shaka wewe unajaribu kuleta uchonganishi baina ya tx na zm, kisa wao wameperusha vyema bendera kuwazidi kwa mambo yenu ya hovyo, hujaeleweka uhusiano Kati ya Drc, zambia na tz, vinginevyo kama sii majungu na kuutumia uzuzu wa wengi kwa manufaa na maslahi ya wenye kuyatazama manufaa ya wachache.
Na hiyo foleni pale Malawi Cargo Kurasini ambapo madereva wanadai wamekaa kwa zaidi ya siku tano bila kushusha mzigo toka Malawi!30 September 2021
Kasumbalesa
Mpakani mwa DR Congo na Zambia
na Nakonde Zambia
Zaidi wa malori 150 ya Tanzania pamoja na madereva wake wazuiwa kuendelea na safari yao baada ya kuvuka mpaka na makontena ya magogo toka nchini DR Congo. Tayari siku thelathini zimepita bila kupatikana ruhusa ya kuendelea na safari. Huku wengine pia wakisema wao wana siku 90 wamekwama nchini Zambia.
Madereva na wamiliki wa malori wamefanya juhudi kuwasiliana na ubalozi wa Tanzania mjini Lusaka Zambia na idara mbalimbali za serikali nyumbani Tanzania bila mafanikio.
Madereva hao wapo ktk kituo cha forodha mpakani nchini Zambia baada ya kuvuka na mzigo huo wenye nyaraka zote halali za mizigo na zinazoonesha wamiliki wa magogo ni wa Nchi DR Congo.
Maafisa wa forodha wa Zambia walidai kuwa magogo hayo ni ya kutoka nchini Zambia. Makontena yalifunguliwa na kufanyiwa uhakiki na kufungwa tena kwa seal lakini bado malori hayo ya Tanzania hayajaruhusiwa kuendelea na safari kuelekea bandari ya Dar es Salaam Tanzania.
Source : Global TV online
Hapa magufuli alijua jinsi ya kuchezaMwanzilishi wa hizi fitna ni Edgar Lungu tena kama si kosei ni kwenye miezi hii ya karibuni baada ya kupitisha sheria zao tata za kulinda maslahi ya nchi yao na watu wao.
Nadhani na sisi tunatakiwa tuwe na sheria za aina hii hii, za jino kwa jino. Magufuli alijitahidi sana kwenye sarakasi za aina hii. Ngoja tuone na Chifu Hangaya nae atachukua hatua gani.