Siasa za mimi Vs wengine sisi Vs wao na hatma ya nchi yetu

Siasa za mimi Vs wengine sisi Vs wao na hatma ya nchi yetu

Azizi Mussa

JF-Expert Member
Joined
May 9, 2012
Posts
9,186
Reaction score
7,492
Ndugu zangu, kuna tatizo lipo lakini ni kama kila mtu anajaribu kulifumbia macho wakati katika hatua yake ya juu kabisa itakuwa ni hasara ya watu wote.

Katika mazingira mbali mbali unakuta mtu anatetea kitu si kwa sababu kitu hicho ni sahihi bali kwa sababu kulingana na upande aliopo kwa wakati husika kitu hicho kinamnufaisha, au kinanufaisha watu wa kundi lake au kinawaumiza wengine. Hii inaweza kuwa katika level ya mtu, level ya vyama au makundi flani flani hivi.

Aidha, kuna watu wanapinga vitu, si kwa sababu vitu wanavyopinga ni vibaya kwa uhalisia wake bali kwa sababu vitu husika vikifanyika kwa usahihi au kwa haki; anayepinga anaona watanufaika wengine ‘wao’ na kinyume chake.

Kwa hiyo kabla mtu hajatetea au kupinga kitu, badala ya kujiuliza ‘ je! hii ni haki?’ au ‘je! Hii sio dhulma’ hijiuliza mimi nitanufaikaje? Kundi langu litanufaikaje? Siwezi kuwanufaisha wao bila kutarajia kweli? Lakini wanaoumia si wao sasa mimi nipate tabu ya nini? Na mtiririko huo wa fikra unaendelea…… bila kujua kuwa kitu ambacho ni sahihi ni sahihi tu na ambacho si sahihi si sahihi tu.

Ushahidi wa mambo haya ni pale unapoona mtu akiwa katika mazingira 'A' anaunga mkono jambo (Ikiwa ananufaika, au angalau haathiriki kwa wakati huo wakati wenzake wanaumia), na mtu huyo huyo akiwa katika mazingira 'B' ( hanufaiki au pengine anaumia wakati wenzake wananufaika) anapinga jambo lile lile na kinyume chake.

Mwishowe hali hii inasababisha tunakuwa hatuna ‘objective truth’ na hatuna ‘objective justice’. Kwa hiyo tunajikuta tunazunguka katika mhimili wa unafiki kiasi kwamba hakuna anayethubutu kuongea ukweli kama ulivyo.

Katika mazingira hayo, hakuna namna tunaweza kujenga jamii adili, tutakuwa tunajidanganya tu na madhara yake yatamgusa kila mmoja wetu. Labda muda tu ndio huweza kutofautiana kati ya mtu na mtu.

Ni vyema tukajilazimisha kutetea vitu kwa kuwa ni vya haki na muhimu na kukemea vitu kwa kuwa ni dhulma au sio sahihi bila kujali nani yuko wapi au nani ananufaika au kuumia. Kwa kufanya hivyo, ndio tunajenga nchi yenye uadilifu wa kweli ambapo ndio msingi mkuu wa kufanikiwa kama taifa. Kinyume chake ni vigumu kupata maendeleo ya kweli kwa kuwa tutakuwa hatuambiani ukweli na tutakuwa hatuaminiani.
 
Ni muhimu tujilazimishe kufanya mambo kama ambavyo tungependa kuona kila mtu anafanya na tujilazimishe kufanyia wengine kama vile ambavyo tungetamani tufanyiwe. Kwa Kabla hujaamua kuchukua au kutochukua hatua fulani inayomuathiri mtu mwingine kwa namna 'psitive' au 'negative' jaribu kujiweka kwenye nafasi yake kwanza halafu ndio uamue, hapo utajikuta unafanya uamuzi wa busara.
 
Na ni vyema watanzania tukajifunza kutokana na matukio. Binadamu ni kiumbe dhaifu mno bila kujali circumstances, na dunia ni kigeu geu. Angalau anapata uimara kwa kufanya maamuzi yenye uadilifu kila mara. unaweza kuwa chini mara ghafla uko juu. una mamlaka mara huna. Upo upo tu mara una mamlaka. Una ushawishi mara huna. ulikuwa nje mara upo ndani n.k

Kwa hiyo njia pekee ya kujihakikishia kwamba kila mmoja wetu anakuwa na usalama na amani ya kudumu ni kufanya maamuzi ya uadilifu wakati wote bila kutumia fikra za mimi na yeye, sisi na wao ambapo hiyo hupelekea kutoona vitu kwenye mwanga sahihi.

Atakayezingatia haya hatajuta katika mazingira yoyote atakayojikuta wakati wowote.
 
Tatizo binadamu tunajisahau mno na kudhani hali tulizonazo ni 'permanent' hasa tunapopata mafanikio fulani. Ni muhumu kujifunza kuwa na 'universal fairness' ili kupata moral authority ya ku mind pale inapotokea mtu, watu au makundi yanazingua. otherwise kila mtu atajuta kwa wakati wake na muda wa majuto ya mtu huwa wengine wanakuwa wanamcheki tu katika mazingira ambayo unafiki unakuwa umekita mizizi.
 
Tulishakemea na kuonya kitambo juu ya haya Mkuu, lakini kwa sababu kuna "wao na wale..., hawa si wenzetu.., wale wanatumika..., sisi wazalendo wale vibaraka..."
Na tusibiri matokeo maana ni yarabi nafsi...
 
Kuna alternative facts,ndio dunia ya Trump, nahuku kwetu imeanza kushika kasi.
Labda swali la kujiuliza kwanini watu wengine wanafurahia alternative facts.
 
Vipi na wale wanaopinga bila kuwa na sababu za msingi, wanapinga tu hata wakiwekewa ushahidi wa kile wanachokipinga hakipo hivyo bado hawataki kukubali, unaweza jikuta na wewe upo kwenye kundi hilo hapo hujajiuliza tu vizuri na nafsi yako, au unajijua ila umejikausha tu.

Watu wanajisikia raha kupinga hata bila sababu za msingi, na hata wakiambiwa pale walipo kuna tatizo kama hilo kwanini wasianze kukemea hapo kwao kabla hawajatoka nje hawana jibu, ni wanafiki, hawa wanachagua "easy target" kushambulia, wapuuzi wa aina hii sio wa kuchekewa au kuwalea hata kidogo, lazima waambiwe ukweli wakome uzandiki wao.
 
Kuna alternative facts,ndio dunia ya Trump, nahuku kwetu imeanza kushika kasi.
Labda swali la kujiuliza kwanini watu wengine wanafurahia alternative facts.
Unakusudia nini mkuu 'unaposema altanative facts'?
 
Vipi na wale wanaopinga bila kuwa na sababu za msingi, wanapinga tu hata wakiwekewa ushahidi wa kile wanachokipinga hakipo hivyo bado hawataki kukubali, unaweza jikuta na wewe upo kwenye kundi hilo hapo hujajiuliza tu vizuri na nafsi yako, au unajijua ila umejikausha tu.

Watu wanajisikia raha kupinga hata bila sababu za msingi, na hata wakiambiwa pale walipo kuna tatizo kama hilo kwanini wasianze kukemea hapo kwao kabla hawajatoka nje hawana jibu, ni wanafiki, hawa wanachagua "easy target" kushambulia, wapuuzi wa aina hii sio wa kuchekewa au kuwalea hata kidogo, lazima waambiwe ukweli wakome uzandiki wao.
Mkuu uko sahihi kwenye hoja ya jumla. Ila hapo unaponiambia 'hata wewe' hata mimi ni mtu, kwa hiyo kwa vyovyote vile nitakuwa nakosea hapa na pale. Kwa hiyo kama nakosea, hakufanyi hilo kosa lisiwe kosa na nisingesema kwa sababu hiyo, ningekuwa nisehemu ya tatizo la msingi kwenye hoja ya msingi.

Hata hiyo mada hii hainizungumziii mimi au wewe, inazungumzia tatizo la jumla. Kwa hiyo nadhani si busara kumtuhumu mleta mada katika muktadha kama huo.
 
Mkuu uko sahihi kwenye hoja ya jumla. Ila hapo unaponiambia 'hata wewe' hata mimi ni mtu, kwa hiyo kwa vyovyote vile nitakuwa nakosea hapa na pale. Kwa hiyo kama nakosea, hakufanyi hilo kosa lisiwe kosa na nisingesema kwa sababu hiyo, ningekuwa nisehemu ya tatizo la msingi kwenye hoja ya msingi.

Hata hiyo mada hii hainizungumziii mimi au wewe, inazungumzia tatizo la jumla. Kwa hiyo nadhani si busara kumtuhumu mleta mada katika muktadha kama huo.
Kama hutaki kukubali tatizo linaanzia kwako na solution itaanzia kwako vilevile basi huwezi kumaliza hilo tatizo, utazunguka sana, ukitaka kuwa mwalimu wa wenzio lazima wewe uwe ume-graduate, huwezi kuwa mwalimu kama ulikimbia darasa kama unavyosema hapa.
 
Kama hutaki kukubali tatizo linaanzia kwako na solution itaanzia kwako vilevile basi huwezi kumaliza hilo tatizo, utazunguka sana, ukitaka kuwa mwalimu wa wenzio lazima wewe uwe ume-graduate, huwezi kuwa mwalimu kama ulikimbia darasa.
Nakubaliana na wewe.
 
Ok, ukikubali hivyo sasa ndio uwafundishe na wale wengine, "kabla hawajatoa kibanzi kwenye macho ya wenzao, watoe kwanza boriti kwenye macho yao"
Ukikubali x

Tukikubali √

Sasa uwafundishe X

Sasa tufundishe√

Sasa tufundishane√

Sasa tushawishiane √

Ukitumia maneno kama 'ukikubali' 'uwafundishwe' usipo.... Huta... Basi fanya..... Tunarudi kwenye tatizo la umimi, uwewe,uwao na.k ambapo hilo ndio tatizo linalotutafuna sasa.
 
Ndugu zangu, kuna tatizo lipo lakini ni kama kila mtu anajaribu kulifumbia macho wakati katika hatua yake ya juu kabisa itakuwa ni hasara ya watu wote.

Katika mazingira mbali mbali unakuta mtu anatetea kitu si kwa sababu kitu hicho ni sahihi bali kwa sababu kulingana na upande aliopo kwa wakati husika kitu hicho kinamnufaisha, au kinanufaisha watu wa kundi lake au kinawaumiza wengine. Hii inaweza kuwa katika level ya mtu, level ya vyama au makundi flani flani hivi.

Aidha, kuna watu wanapinga vitu, si kwa sababu vitu wanavyopinga ni vibaya kwa uhalisia wake bali kwa sababu vitu husika vikifanyika kwa usahihi au kwa haki; anayepinga anaona watanufaika wengine ‘wao’ na kinyume chake.

Kwa hiyo kabla mtu hajatetea au kupinga kitu, badala ya kujiuliza ‘ je! hii ni haki?’ au ‘je! Hii sio dhulma’ hijiuliza mimi nitanufaikaje? Kundi langu litanufaikaje? Siwezi kuwanufaisha wao bila kutarajia kweli? Lakini wanaoumia si wao sasa mimi nipate tabu ya nini? Na mtiririko huo wa fikra unaendelea…… bila kujua kuwa kitu ambacho ni sahihi ni sahihi tu na ambacho si sahihi si sahihi tu.

Ushahidi wa mambo haya ni pale unapoona mtu akiwa katika mazingira 'A' anaunga mkono jambo (Ikiwa ananufaika, au angalau haathiriki kwa wakati huo wakati wenzake wanaumia), na mtu huyo huyo akiwa katika mazingira 'B' ( hanufaiki au pengine anaumia wakati wenzake wananufaika) anapinga jambo lile lile na kinyume chake.

Mwishowe hali hii inasababisha tunakuwa hatuna ‘objective truth’ na hatuna ‘objective justice’. Kwa hiyo tunajikuta tunazunguka katika mhimili wa unafiki kiasi kwamba hakuna anayethubutu kuongea ukweli kama ulivyo.

Katika mazingira hayo, hakuna namna tunaweza kujenga jamii adili, tutakuwa tunajidanganya tu na madhara yake yatamgusa kila mmoja wetu. Labda muda tu ndio huweza kutofautiana kati ya mtu na mtu.

Ni vyema tukajilazimisha kutetea vitu kwa kuwa ni vya haki na muhimu na kukemea vitu kwa kuwa ni dhulma au sio sahihi bila kujali nani yuko wapi au nani ananufaika au kuumia. Kwa kufanya hivyo, ndio tunajenga nchi yenye uadilifu wa kweli ambapo ndio msingi mkuu wa kufanikiwa kama taifa. Kinyume chake ni vigumu kupata maendeleo ya kweli kwa kuwa tutakuwa hatuambiani ukweli na tutakuwa hatuaminiani.
Huu ni uzi wenye maneno ya kiungwana sana tena sana natarajia uzi huu upate like za kutosha kutoka GT wote humu ndani

Huu ni ukweli unaodhihiri na hii ndio hali halisi iliyopo kwa sasa. Jambo hili hapo mwanzo lilikuwapo lakini halikudhihiri kwa kiwango cha sasa nanilikua rahisi kukontrol emotions za watu lakini kwasasa limevuka kiwango na kumekua na uongozi wa kinafiki uliojaa uongo na chuki kila kiongozi aneshikilia sector fulani amukuwa muongo kupitiliza

Bila ya kuficha wala kupepesa macho jambo hili ndilo litakalo mgharimu Mwendazake JPM kwani yeye ndie chanzo cha kuchochea hali hii kutokana na siasa za kibaguzi na upendeleo alizo zalisha katika wakati wake

Leo hii katuachia ushindani wa siasa za uhasama usio na tija kwa Taifa ama hakika hili jambo halitomuacha salama huko aliko ALLAH amuhukumu kwa anavyostahili katuachia siasa mbaya sana ambazo zimeleta mpasuko wenye haiba ya unafiki na uzandiki wa kiwango cha SHETANI

Hili ni jambo baya sana. Binafsi namuomba kwa baraka za muda huu awaangamize wooote waliokalia uongozi kwa njia ya ghilba isiyokua na radhi na matakwa ya wananchi. ALLAH awangamize wasifike 2025 kwa uweza wake yeye awasitishe katika nafasi zao kwa namna yeyote awezayo iwe kwa kifo, ugonjwa au ulemavu wa kudumu.

Walaaaniwe wooote wanaoshawishi, kuunga mkono au kubeba siasa za chuki hasa Ndg. JOB NDUGAI, ALLAH nakuomba umdhibiti kiumbe huyu si mtu wa haki nakuomba ya ALLAH upitishe lako katika hawa na huyu binadam mlimwengu

Wapenda haki tuseme Aaaamiiin [emoji2969][emoji2969][emoji2969]
 
Kama hutaki kukubali tatizo linaanzia kwako na solution itaanzia kwako vilevile basi huwezi kumaliza hilo tatizo, utazunguka sana, ukitaka kuwa mwalimu wa wenzio lazima wewe uwe ume-graduate, huwezi kuwa mwalimu kama ulikimbia darasa kama unavyosema hapa.
Hebu nikuulize swali Ndugu Je, COVID-19 ni wabunge halali?
 
Huu ni uzi wenye maneno ya kiungwana sana tena sana natarajia uzi huu upate like za kutosha kutoka GT wote humu ndani

Huu ni ukweli unaodhihiri na hii ndio hali halisi iliyopo kwa sasa. Jambo hili hapo mwanzo lilikuwapo lakini halikudhihiri kwa kiwango cha sasa nanilikua rahisi kukontrol emotions za watu lakini kwasasa limevuka kiwango na kumekua na uongozi wa kinafiki uliojaa uongo na chuki kila kiongozi aneshikilia sector fulani amukuwa muongo kupitiliza

Bila ya kuficha wala kupepesa macho jambo hili ndilo litakalo mgharimu Mwendazake JPM kwani yeye ndie chanzo cha kuchochea hali hii kutokana na siasa za kibaguzi na upendeleo alizo zalisha katika wakati wake

Leo hii katuachia ushindani wa siasa za uhasama usio na tija kwa Taifa ama hakika hili jambo halitomuacha salama huko aliko ALLAH amuhukumu kwa anavyostahili katuachia siasa mbaya sana ambazo zimeleta mpasuko wenye haiba ya unafiki na uzandiki wa kiwango cha SHETANI

Hili ni jambo baya sana. Binafsi namuomba kwa baraka za muda huu awaangamize wooote waliokalia uongozi kwa njia ya ghilba isiyokua na radhi na matakwa ya wananchi. ALLAH awangamize wasifike 2025 kwa uweza wake yeye awasitishe katika nafasi zao kwa namna yeyote awezayo iwe kwa kifo, ugonjwa au ulemavu wa kudumu.

Walaaaniwe wooote wanaoshawishi, kuunga mkono au kubeba siasa za chuki hasa Ndg. JOB NDUGAI, ALLAH nakuomba umdhibiti kiumbe huyu si mtu wa haki nakuomba ya ALLAH upitishe lako katika hawa na huyu binadam mlimwengu

Wapenda haki tuseme Aaaamiiin [emoji2969][emoji2969][emoji2969]
Mkuu, ni vyema hata kama mtu kakosea amma ukamuelewesha au kumshawishi lakini sio kumlaani au kumuombea mabaya.

Aidha, kama nilivyosema kuwa uadilifu ni kufanya vitu kwa namna ambayo ungetamani kila mtu awe anafanya, sasa fikiria kila mtu akimlaani yule ambaye anaona anakosea hauoni mwishowe tutalaaniana na kuombeana mabaya wote ikiwemo na wewe?

Halafu pia kumuombea mabaya kiongozi akiwa madarakani, ni sawa na kumuombea dereva wa basi apate ajali ukiwa ndani ya basi. Hata kama huyo dereva anakosea, wewe unakuwa umekosea zaidi.

Kwa hiyo nadhani tushawishiane in a positive way hii itatusaidia tuwe pazuri zaidi leo kuliko jana na kesho kuliko leo.
 
Ukikubali x

Tukikubali √

Sasa uwafundishe X

Sasa tufundishe√

Sasa tufundishane√

Sasa tushawishiane √

Ukitumia maneno kama 'ukikubali' 'uwafundishwe' usipo.... Huta... Basi fanya..... Tunarudi kwenye tatizo la umimi, uwewe,uwao na.k ambapo hilo ndio tatizo linalotutafuna sasa.
Unatakiwa ukae na wenzio mnaofanana muelekezane kabla mimi nisiefanana nao kuwakalisha chini hawatanielewa, ndio maana hata nikiwawekea ushahidi kile wanachopigia kelele hakiko hivyo bado hawataki kukubali, kwasababu wameshakariri miaka yote makosa huanzia kwa wenzao, sio kwao, sasa wewe ukae nao naamini watakuelewa upesi ukitoka huko ndio mje na jibu moja, kama mtakuwa tayari kukubali udhaifu wenu lakini, sio kulazimisha tu udhaifu upo kwa wenzenu.
 
Back
Top Bottom