Mbona zipo option nyingi. Malori yanaweza kushushia mzigo hapo mpakani wakachukua kwa lori za Rwanda bila kulipia extra road toll.
All in all gharama za biashara zinaongezeka kwa wanyarwanda zaidi kuliko kwa watanzania.
au ndio keshawajua huku wengi tukiwa tumelala bado?
Mkuu, mkiona Kagame anapiga kelele ni amejaribu sana kuwa accomodating ila kuna mahali inafika mtu unashindwa kuvumilia. Tanzania inabidi mjirekebishe katika karne hii ya utandawazi na ushindani.
Kwani wenye magari watakuwa wapumbavu kiasi hiko na wao ongezeko la gharama si wanawatupia wenye mizigo, hawataki mizigo inadoda bandarini na gharama za kuifadhi juu; mpaka inabaki kuwa mali ya serikali ya Tanzania.
Hapa serikali irudishe compliments tu na magari yatakayo toka Rwanda yapate same treatment for now at least we should gain whilst they are still reinforcing their strategy of diverting their cargo to Mombasa.
Wana Jamiii
Nipo hapa Rusumo mpakani mwa Tanzania na Rwanda.....siamini ninachokiona machoni mwangu....kuanzia jana tarehe 1/09/2013 serekali ya Rwanda imeongeza ushuru wa barabara ( ROAD TOLL) kwa magari yote ya Mizigo ( Fuel and Dry Cargo) yenye plate numbers za Tanzania kutoka USD 152 mpaka USD 500 kwa kila gari.
Kwa taarifa ambazo sio rasmi kwa siku magari ya mizigo takribani 300 yanavuka hapa mpakani, na zaidi ya asilimia 95% ya magari hayo zina plate numbers za Tanzania.
Wanajamii hii ina madhara gani kwa uchumi wa Tanzania kwani akili ya harakaharaka hii ni some sort of Protectionism ila kwa mbali inaweza ikawa ni muendelezo wa chokochoko.
Taarifa yako haijakamilika. Haujasema kuwa magari ya rwanda yanayoingia tanzania yamekuwa yakitozwa hiyo dola 500 for many years. Wamejaribu ku plead serikali yenu ipunguze ili hiyo gharama iendane na za nchi nyingine wanachama wa East Africa. Tanzania walikuwa wanajishebedua.
Wana Jamiii
Nipo hapa Rusumo mpakani mwa Tanzania na Rwanda.....siamini ninachokiona machoni mwangu....kuanzia jana tarehe 1/09/2013 serekali ya Rwanda imeongeza ushuru wa barabara ( ROAD TOLL) kwa magari yote ya Mizigo ( Fuel and Dry Cargo) yenye plate numbers za Tanzania kutoka USD 152 mpaka USD 500 kwa kila gari.
Kwa taarifa ambazo sio rasmi kwa siku magari ya mizigo takribani 300 yanavuka hapa mpakani, na zaidi ya asilimia 95% ya magari hayo zina plate numbers za Tanzania.
Wanajamii hii ina madhara gani kwa uchumi wa Tanzania kwani akili ya harakaharaka hii ni some sort of Protectionism ila kwa mbali inaweza ikawa ni muendelezo wa chokochoko.
Watakaoumia ni wanyarwanda wenyewe,kwani ninachojua hakuna mfanyabiashara anayepata hasara hata siku moja! hivyo kama bidhaa kama zinapelekwa Rwanda bei ya bidhaa zitapanda tu!
Mimi nnadhani madhara ya kiuchumi yatatokea kwa upande wanTanzania,japo kwa kiwango fulani.Nnapata ukakasi kidogo kuchangia kwa ukamilifu kwa sababu hatujui gharama sahihi za kushusha/kupitishia mizigo ktk bandari ya Mombasa nchini Kenya vile vile kwa hapa kwetu Tanzania .
Ila kwa juu juu ni kuwa mfanyabiashara siku zote anahitaji unafuu katika biashara zake ili kupata faida na pia kuuza mali zake kwa wepesi hasa kutokana na bei.Kwa mfano wapo wanaosema wananchi wa Rwanda ndio watatishwa mzigo huu ulioongezwa na hilo nnakubaliana nalo ila tuchukulie mimi ni mfanyabiashara wa Rwanda nimeshusha mifuko ya saruji kupitia Tanzania na mfanyabiashara mwenzangu nae ameshusha hiyo hiyo mifuko ya saruji na yeye akatumia bandari ya Mombasa nchini Kenya.Swali la kujiuliza hapa ni hivi kama gharama za kushusha mzigo kupitia Mombasa zitakuwa ni za chini zaidi ya za Tanzania ni mfanyabiashara yupi atakubali kupitishia mzigo ktk bandari ya Tanzania.
Tukumbuke wafanyabiashara wanahitaji unafuu katika kazi zao ili waweze kwenda kushindana na soko huko wanapopeleka mizigo yao..
Nnawaomba wenzangu ktk jukwaa hili muache kuishambulia Rwanda na raisi wao,ile ni nchi na ina mamlaka zake tusiwaingilie ktk maamuzi yao hata kama watasema hakuna kuingiza magari yanayotoka Tanzania.Tujadili athari za kiuchumi kama mtoa mada alivyowasilisha,pia tungeomba wenye upeo zaidi katika taaluma ya uchumi waje huku watusaidie,lakini kuwashambulia kina Kagame na nchi yake haitotusaidia chochote.
Afadhali wambie Kamanda, unajua Watanzania ni kama tumelogwa. Tunashabikia mambo bila kufikiria, watakao umia ni haohao wanaomiliki biashara za malori. Na hii maana ya haraka haraka ni kuanza ku discourage mizigokushushiwa Dar sasa watalazimika kwenda Bandari ya Mombasa.
Mambo mengine adghabu zake ni hapa hapa tu hakuna kungojea,
TAFAKARI
Taarifa yako haijakamilika. Haujasema kuwa magari ya rwanda yanayoingia tanzania yamekuwa yakitozwa hiyo dola 500 for many years. Wamejaribu ku plead serikali yenu ipunguze ili hiyo gharama iendane na za nchi nyingine wanachama wa East Africa. Tanzania walikuwa wanajishebedua.
Mkuu weka tofauti kando kaka, Hii ni business usifanye mchezo. Mwanzoni walikuwa wakitoza 150 USD per truck sasa wameongeza mpaka 500USD kwa magari ya TZ pekee, Ya nchi zingine wanachaji hiyohiyo 150usd. Sasa inaonekana hujui hali ipoje kaka.
Ikiwa kweli hali ndio iko hivyo, ni vema tujue charge kwa upande wa Rwanda/Kenya; Rwanda/Uganda na Rwanda/Burundi (ceteris paribus). Tukijua hivyo tutaweza kuona nini Tanzania inaweza kufanya. Na nmna mojawapo ni kutumia "US style"; kiburi cha Rwanda kinatoka Kenya, Mombasa Port na Trilateral cooperation lakini Kenya inauza Tanzania zaidi ya 50% ya mauzo yake yote EAC; hivyo namna rahisi ni ku-deal na Kenya kwa kumuanzishia masharti magumu ya kuingiza bidhaa zake Tanzania (based on cost-benefit analysis). Hii itamlazimisha Kenya apeleke hoja EAC kwanini Tanzania imeweka masharti mapya na hapo ndipo Tanzania ita-lobby kupata maamuzi yatakayotengua tozo mpya ya Rwanda (Reverts all new rates imposed by any EAC country on specific dates before negotiating) .
Usiwe mwepesi mkuu, ngoja kwanza atupe info zaidi huyu murutongore kama yuko sahihi. Sioni kwanini Rwanda ilikuwa inataka kuwa na rate moja na Tanzania bilateral badala ya Regional? Na je vigezo gani havina budi kutumika kama tutafikia kuwa na equal rates wakati (huenda) magari kutoka kila upande yanatumia barabara umbali tofauti?This is "news" to me! Kumbe haya malalamiko yetu hayana msingi wowote kata hali ni hii unayoisema!
Toa maelezo zaidi acha unazi, Rusumo/Kigali-Rusumo/Dar how? Na je kwanini accomodating ya Kigali iwe bilateral badala ya Regional approach kama hiyo ndiyo hoja?Mkuu, mkiona Kagame anapiga kelele ni amejaribu sana kuwa accomodating ila kuna mahali inafika mtu unashindwa kuvumilia. Tanzania inabidi mjirekebishe katika karne hii ya utandawazi na ushindani.
Wana Jamiii
Nipo hapa Rusumo mpakani mwa Tanzania na Rwanda.....siamini ninachokiona machoni mwangu....kuanzia jana tarehe 1/09/2013 serekali ya Rwanda imeongeza ushuru wa barabara ( ROAD TOLL) kwa magari yote ya Mizigo ( Fuel and Dry Cargo) yenye plate numbers za Tanzania kutoka USD 152 mpaka USD 500 kwa kila gari.
Kwa taarifa ambazo sio rasmi kwa siku magari ya mizigo takribani 300 yanavuka hapa mpakani, na zaidi ya asilimia 95% ya magari hayo zina plate numbers za Tanzania.
Wanajamii hii ina madhara gani kwa uchumi wa Tanzania kwani akili ya harakaharaka hii ni some sort of Protectionism ila kwa mbali inaweza ikawa ni muendelezo wa chokochoko.
Ni hiv: Kuna tetesi kwamba wafanya biashara wote wa Rwanda, wameambiwa wasipitishe mizigo katika Bandari ya Dar. Hii ni njia mojawapo ya kuwafanya wasipitishe mizigo hapa. Kuongeza ushuru wa barabara kutawafanya Wafanyabiashara wengi kuacha kutumia bandari yetu. Na hii ina madhara ya kiuchumi kwa serikali na watu binafsi pia. Wharfage na handling ambayo walikuwa wanalipa bandarini kwetu haitakuwepo tena na pia wasafirishaji watakosa mizigo....ajira hakuna.
Kwa hili haongezi gharama kwa watu wake ila faida kwa mwenye gari inapungua au inaondoka kabisa. Lengo lake ni kulazimisha waagizaji mizigo watumie bandari ya Mombasa badala ya Dar es Salaam. Watapata msukosuko kwa muda tu then wakianza kupitia Mombasa mambo yatatulia.
Ina maana gani kwetu? Tuboreshe reli ya kati. Hao wenye malori ndio walikuwa wanahujumu reli ya kati isifanye kazi au isiboreshwe. Tena wengi wao ni wakubwa haohao.