Sidhani kama Tanzania itaendelea katika uhai wetu

Sidhani kama Tanzania itaendelea katika uhai wetu

Sijali

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2010
Posts
2,672
Reaction score
1,814
Maendeleo ni ya watu, na si vitu. Maana hiyo ni mpaka hapo asilimia 80+ ya Watanzania watakapomudu kula milo mitatu ya wastani, kuwa na makazi yanayofaa binadamu kuishi, kuwa na huduma za elimu bora, afya, maji na usafiri wa kukidhi kwa wastani.

Zaidi ya hayo, kuwa na uhuru wa kutonyanyaswa na polisi, uhuru wa kutoa maoni, kuishi kwa amani bila hofu yeyote, kumchagua wampendaye kuwaongoza.

Sidhani haya yatapatikana katika miaka mingine 60 ijayo. Kama unaaamini yatapatikana niambie, vipi?
 
Tukiweza kujitambua (self determination) tu basi hayo yote yatawesekana.
 
Mbona unajichanganya!!!
Unasema Maendeleo ni ya watu, na si vitu hapo hapo unadai Watanzania watakapomudu ... kuwa na makazi yanayofaa binadamu kuishi, kuwa na huduma za elimu bora, afya, maji na usafiri wa kukidhi kwa wastani.
 
Mbona jini jiwe alisema nchi ishaendelea tayari? Alisema hii ni dona kantre.

Nasema uwongo ndugu zangu?
 
Kwa nini umefikiri hivyo?
 
Mbona unamuita marehemu mjina mabaya alikufanyia nn ndg
Aliteka watu, aliuwa watu, alipora fedha za watu aliwabomolea watu nyumba,aliwatumbua watu kwa madai ya kijinga eti Wana vyeti feki, alifanya mengi maovu
 
1. Una uhakika au na we we umesikia tuu !?
 
Maendeleo ni ya watu, na si vitu. Maana hiyo ni mpaka hapo asilimia 80+ ya Watanzania watakapomudu kula milo mitatu ya wastani, kuwa na makazi yanayofaa binadamu kuishi, kuwa na huduma za elimu bora, afya, maji na usafiri wa kukidhi kwa wastani.

Zaidi ya hayo, kuwa na uhuru wa kutonyanyaswa na polisi, uhuru wa kutoa maoni, kuishi kwa amani bila hofu yeyote, kumchagua wampendaye kuwaongoza.

Sidhani haya yatapatikana katika miaka mingine 60 ijayo. Kama unaaamini yatapatikana niambie, vipi?
Ni mada nzuri, tena umeweka mhtasari ulio shiba kabisa!

Nami ningetamani hayo uliyoyaeleza hapa yapatikane katika uhai wa kizazi hiki, na ninaamini yangewezekana kwa sehemu kubwa kutimia kama tungefanikiwa kuwa na viongozi 'determined' kabisa kuyatimiza. Viongozi ambao kuwepo kwao si kwa minajiri ya kujinufaisha au kujitafutia sifa.
Viongozi ambao wamejitoa kabisa kwa Tanzania yenye mafanikio hayo.

Viongozi ambao wanajua ni vipi vipaumbele vinavyotakiwa kufanywa ili kufika huko kwa haraka, na wako tayari kuwekeza raslimali katika maeneo hayo ya vipaumbele.

Viongozi wanaojua kwamba maendeleo hayo ya nchi yetu hayaletwi kwetu na watu wengine, bali kazi kubwa ya kuyaleta ni sisi wenyewe; kwa hiyo wangehimiza na kuelimisha wanchi waielewe hali hiyo na kuwapa nyenzo muhimu za kufanya hivyo

Ili uweze kutatua tatizo linalokukabili ni lazima ujuwe tatizo lenyewe lilivyo. Kwa hiyo viongozi hawa wanatakiwa kuwa na ufahamu mzuri kabisa ni wapi hasa panapotupa shida ya kutokwenda mbele haraka ili kufikia lengo hilo uliloliweka kwenye mada yako.
Viongozi wanaojipigia tu mradi liende, matokeo yake ni yaleyale ya kuzungukia humo humo tulimokwishapitia bila ya kwenda mbele.

Tazama, tupo kwenye hatua nzuri sana kuinuka kwa haraka na kufika huko unakokutamani. Chukulia mifano ya maji na umeme, kwa mfano, tukidhamiria kweli katika miaka mitano ijayo tukisema tunataka maji na umeme viwe vimesambaa maeneo yote ya nchi, hili kweli linaweza kutushinda? Inahitajika pesa kiasi gani ndani ya miaka mitano kufanya hili,- piga hesabu. Umeme, kama bwawa la Julius Nyerere litaweza kuzalisha umeme kiasi kile, kwa nini usiweze kusambaa na kumfikia kila mwananchi; lakini sasa nasikia mipango ya upigaji, akina Makamba wanaisuka na kupoteza lengo; wanatafuta umeme wa Jua/Upepo, n.k., tena wa kulangua! Usiniambie siutaki huo, lakini hiyo kwa wakati huu ni kupoteza lengo tu na kutafuta upigaji kwenda mbele.

Kwani hawa raia (wengi wao wako vijijini) wakulima wa jembe la mkono, zaidi ya asilimia 60, wako huko vijijini, ndio unaowazungumzia kwa huduma ulizo orodhesha hapo wazipate?
Kiongozi anayetafuta maendeleo ya nchi kwa kwenda kuleta watu toka nje waje hapa kuwainua hawa wananchi kutokana na hali zao duni, unamwamini kweli?
Fanya kazi na hawa watu huko makazini kwao wachakalike, wapate haki ya juhudi zao, utaona nchi inabadilika haraka sana. Unakwenda kutafuta watu, tena toka nje waje wawakamue hawa hawa unaotaka wapate maji, umeme , n.k., itakuchukua muda gani kufika huko!
 
Sijali wewe at your personal level umejiendeleza na umeendeleza nchi kwa kiasi gani kimaendeleo? Usije kujibu ati unalipa Kodi sijui kitu gani! Kama wewe katika individual level umeshindwa kuwa na maendeleo usitarajie nchi kuwa na maendeleo! Kila moja wetu ajiendeleze ktk hatua yake.
 
Sidhani haya yatapatikana katika miaka mingine 60 ijayo. Kama unaaamini yatapatikana niambie, vipi?
Utakuwa bado upo mkuu 'sijali'?
Hivi kuna mifano ya nchi ambazo zimepata maendeleo haraka chini ya umri huo? Malaysia na wengine...

Najuwa kuna mifano ya nchi zilizochukua muda mrefu sana kufikia hatua hiyo na nyingine bado hata kukaribia huko hazionyeshi, mfano Haiti!

Egypt, Ethiopia, Turkey..., hii imeinuka hivi karibuni, na Egypt.
ipo njiani; Ethiopia inasuasua, lakini ilikuwa imeanza kuonyesha dalili za kuinuka, sasa wamevurugika tena.

Hapo hapo usisahau, hakuna tena anayetafuta kugundua gurudumu upya kabisa katika nyanja za maendeleo ya nchi. Sasa hata kugezea walichofanya wengine pia tushindwe?
Haiwezekani kamwe kuchukua muda wa miaka 60 mingine, ila labda kama tukiendelea kuvurugwa na hawa CCM na mambo zao, tutaendelea kuwa kama Haiti, mpaka vikina Rwanda vije kututawala ndipo akili inaweza kutuingia tena kichwani.
 
Haiwezekani.

Miaka 60 baada ya uhuru bado maadui wetu ni wale wale watatu ( ujinga, maradhi, na umasikini).

Lately ameongezeka adui mwingine wa nne, CCM; huyu nae ametuzalia watoto kibao kama uvunjifu wa haki za binadamu, na tatizo la utawala bora.

Nadhani kuwatokomeza hawa wote na mizizi yao itachukua karne au zaidi.
 
Maendeleo ni ya watu, na si vitu. Maana hiyo ni mpaka hapo asilimia 80+ ya Watanzania watakapomudu kula milo mitatu ya wastani, kuwa na makazi yanayofaa binadamu kuishi, kuwa na huduma za elimu bora, afya, maji na usafiri wa kukidhi kwa wastani.

Zaidi ya hayo, kuwa na uhuru wa kutonyanyaswa na polisi, uhuru wa kutoa maoni, kuishi kwa amani bila hofu yeyote, kumchagua wampendaye kuwaongoza.

Sidhani haya yatapatikana katika miaka mingine 60 ijayo. Kama unaaamini yatapatikana niambie, vipi?
Kama Lowasa akiwa na miaka 65+ aliamini tutapara maendeleo kupitia yeye wewe kijana nini kinakukatisha tamaa mapema hivi.
 
Haiwezekani.

Miaka 60 baada ya uhuru bado maadui wetu ni wale wale watatu ( ujinga, maradhi, na umasikini).

Lately ameongezeka adui mwingine wa nne, CCM.

Nadhani kuwatokomeza hawa wote na mizizi yao itachukua karne au zaidi.
🤣🤣🤣
 
Maendeleo sio kitu rahisi rahisi kinachopatikana kwa watu kubembelezwa bembelezwa na kulia kulia kila siku..

Maendeleo yanapatikana kwa watu kufanya kazi kwa bidii usiku na mchana vizazi na vizazi, baada ya vizazi kadhaa kusucrifice kwa ajili ya Taifa lao ndio huja vizazi vitakavyoneemeka..

Mpaka sasa Tanzania hakuna kizazi kilichojitolea kuleta maendeleo na kizazi kingine kikaendeleza kilipoishia kizazi kilichopita...Maendeleo sio jambo la kulala usiku mchana maendeleo yakaja, watu lazima wajitolee kweli..

Ulaya na America tayari vizazi na vizazi huko nyuma vilijitolea kuleta maendeleo kwa kufanya kazi kwa bidii na nguvu zote usiku mchana, jua mvua, jasho na damu..
 
Haiwezekani.

Miaka 60 baada ya uhuru bado maadui wetu ni wale wale watatu ( ujinga, maradhi, na umasikini).

Lately ameongezeka adui mwingine wa nne, CCM.

Nadhani kuwatokomeza hawa wote na mizizi yao itachukua karne au zaidi.

Umejitoleaje kuhakikiaha hao maadui akiwemo huyo CCM wanaondoka...Anza hapo ulipo kujitolea kwa jasho na damu kwa maendeleo ya vitukuu vyako..
 
CCM iweke kama sehemu muhimu ya kututia umasikini

Wapi umejitolea ukatoka damu na jasho ikiwezekana kufa ili hiyo CCM itoke na hayo maendeleo yaje...anza sasa hapo ulipo kwa manufaa ya vitukuu vyako....Tunaposema maendeleo yanahitaji jasho na damu hii ndio tafsiri yake....watu kuumia kwa kuondoa kila aina ya ujinga unaokwamisha maendeleo..
 
Mbona unajichanganya!!!
Unasema Maendeleo ni ya watu, na si vitu hapo hapo unadai Watanzania watakapomudu ... kuwa na makazi yanayofaa binadamu kuishi, kuwa na huduma za elimu bora, afya, maji na usafiri wa kukidhi kwa wastani.
Maendeleo ya watu ni miundombinu! Ukiona mtu anapinga hilo jua ni mpuuzi kama Tundu Lissu
 
Back
Top Bottom