Sie tunasajiri nyie mnatuangalia tu

ibanezafrica

JF-Expert Member
Joined
Oct 23, 2014
Posts
7,261
Reaction score
6,553
Muda utaongea,Yanga na Azam tu ndiyo zimeonekana kama vilabu pekee zenye kujiamini katika kujipanga kuelekea msimu mpya wakati vilabu vingine vikipigwa butwaa bila hata kujua wafanye nini.

Tukumbuke safari hii muda wa pre season ni mfupi mno, timu zinatakiwa kujipanga mapema.

Naona kuna kila dalili msimu ujao kuna timu itapigania kumaliza top 4..tupo hapa, wakati ndio huu.
 
Mbona Habibu Kiyombo tayari ni wa kwetu! Tena tumetumia jeuri ya pesa kwa kuvunja mkataba wake na Singida Big Stars!

Na sasa tuko katika mazungumzo ya mwisho kabisa kumsainisha Saido Ntibazonkiza ili aongeze chachu ya mafanikio msimu ujao! Eeehh bado tu unalalamika?
 
Toka lini ukawa msemaji wa ze simba fc nyie sajilini kwani nyie mnataka nini kila mtu aishi kwake
 
Kwani Dirisha la usajili si limefinguliwa tarehe 1 Julai hadi Agosti 31, 2022?

Tukisema mashabiki wa yanga huwa wanafikiria kwa kutumia viungo vinavyopatakana chini ya shingo....mtasema tuna matusi

Nyie si mnasajili buana, endeleni kusajili[emoji2]
 

Yaani kuvunja mkataba na vitimu vya ligi kuu ndio UANAUME?

Wanaume wamevunja mkataba wa Aziz KI huko...kumbuka Simba SC walishindwa.

Kwa Moses Phiri nako mulishindwa mkaamua kusubiri mpaka mkataba wake uishe.

Kwa adebayor ndio wala tusizungumze.
 
Yaani kuvunja mkataba na vitimu vya ligi kuu ndio UANAUME?

Wanaume wamevunja mkataba wa Aziz KI huko...kumbuka Simba SC walishindwa.

Kwa Moses Phiri nako mulishindwa mkaamua kusubiri mpaka mkataba wake uishe.

Kwa adebayor ndio wala tusizungumze.
Huna akili.

Utopolo hawawezi kuvunja mkataba hata wa CHIDY MCHELENGA wa INSTA UNITED.

KAMBOLE FREE
KI AZIZI FREE
BANGALA FREE
MAYELE FREE
DIARA FREE

TIMU NZIMA FREE



Sent from my PBBM00 using JamiiForums mobile app
 
Malalamilko fc, kila kitu nyie ni kulalamika.
 
Yaani kuvunja mkataba na vitimu vya ligi kuu ndio UANAUME?

Wanaume wamevunja mkataba wa Aziz KI huko...kumbuka Simba SC walishindwa.

Kwa Moses Phiri nako mulishindwa mkaamua kusubiri mpaka mkataba wake uishe.

Kwa adebayor ndio wala tusizungumze.

So, unataka useme Yanga wana-pesa kuliko simba?

au

Simba hawana uwezo wa kutoka kiasi alichotoa Yanga kwa hao wachezaji?

Milionea kumzidi Bilionea katika mnada, hamfanyi milionea kuwa bilionea and vice versa is true; Ila hapo mipango na mahesabu tu tumetofautiana(usifananishe na ubahili)

Yaani Bajeti yako unataka kununua kitanda kizuri, godoro zuri, mashuka mazuri (Full set), ila unaenda dukani...kwakua umependa kitanda sana(au unataka kuwaonesha watu unapesa) unaamua kutoa bajeti yako yote kwenye kitanda tu...unabaki kulala kwenye Chaga tu....Hii ni akili? au hapo utasema unapesa? [emoji23]

N.B, Kama hujaelewa, soma tena, tena taratibu[emoji41]
 
Ushamba na ulimbukeni tu unawasumbua nyie mbwakoko kama alivyowaita Luc. Simba hawana haja ya kupiga tarumbeta kila wanachofanya kutangaza
 
Ukweli ni kwamba ukimya wa Simba kwenye usajili unawaumiza utopolo
Si kweli tunajua hamba mipango wala scouring bora na vile mzee Hans pope ametangulia mbele ya haki mtapata taabu sana
 
Manara ndo alikuwa mnafiki anayevujisha siri za simba nyie fanyeni mambo yenu mambo ya simba hayawahusu subirini champion's league ianze muanze kwenda airport kuwapokea wageni wenu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…