Sielewi kwanini mtu aliyechakachua msaada wa serikali na kujimilikisha enzi za Kikwete, akaondolewa leo anateuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa

Ukosefu wa demokrasia miaka 5 ya muovu dikteta jiwe haikutoa fursa kwa wanasiasa wapya kuonesha vipaji vyao. Ndiyo maana watu wanaojulikana vipaji vyao ni wale wa enzi ya Kikwete.

Madhara ya kuongozwa na mwendazake ndiyo tunayaona
Bila ya kumtetea huyo 'dikteta', uozo mwingi umeenea ndani ya chama chenyewe, na hata katika jamii nzima sasa.
 
Kuna mwingine alikuwa waziri wakati wa JK akavurunda , akapewa ubalozi Japan akavurunda , Jiwe akampa ubalozi Kenya akavurunda , Mama kampa uRAS kwa wiki moja na kumpandisha kuwa mkuu wa mkoa .
 
Very strange!
 
Bila ya kumtetea huyo 'dikteta', uozo mwingi umeenea ndani ya chama chenyewe, na hata katika jamii nzima sasa.
Acha uongo. Si tunachotaka maendeleo na si maneno, Period! Eti wanasiasa wa Kikwete wapi hao wapiga maneno au. Hebu eleza kipi kikubwa alichokifanya!
 
Yaani kwa kweli hata sielewi tunakoelekea kwa kweli!
 
Kiongozi msafi tulimpata kwa ni tuliona matendo yake! Sasa tunalala!
 
Acha uongo. Si tunachotaka maendeleo na si maneno, Period! Eti wanasiasa wa Kikwete wapi hao wapiga maneno au. Hebu eleza kipi kikubwa alichokifanya!
Wewe hata kuandika tu vizuri ueleweke ni shida; sasa utaanzia wapi kuelewa kilichoandikwa!
 
Gentamycine, hii post uliyotoa hapa haifanani na wewe kabisa. Kama unasema kuna nongwa ya Batilda, halafu unauliza ni nani ana ushahidi kamili, unajuaje watu wanaooingelea hawana ushahidi? Yaani mtu akitaja kitu kwenye post lazima aweke ushahidi wote? Na usikimbilie kuwaambia watu wanatoa maoni yao kwa ajili ya wivu na unafiki wakati hujajua wako karibu kiasi gani na watajwa waliohusika. Kwa mfano, mimi naweza kuwa ndani ya wizara inayohusika na watu waliofanya matukio fulani, na ninajua ukweli wote. Sasa kwa kuwa sijafanya photocopy ya huo ukweli na kuupaste hapa mtandaoni usiwe na haraka kusema ninachosema msingi wake ni wivu na unafiki.

Hapa hatuko ku-present document ya mashitaka, bali kupresent context, na anapotajwa mtu inakuwa na namna fulani ya mfano kutokana na matukio halisi ambayo watu walisikia au kusoma kwenye vyombo vya habari. Sasa usisome kila comment humu ndani with the eyes of a lawyer. Huko ni kuwa na expectation kwamba kila mwana JF awe a learned lawyer.

Nimemuuliza mtu mmoja aliyetoa maneno kama yako, kwamba ina maana nikikuandika humu ndani umefanya mchoro fulani ambao uliipiga serikali ukafanikiwa, utakata shauri kwamba mimi ni mtu wa majungu, au nafanya hivyo kwa ajili ya wivu na unafiki? Labda pia na wewe nikuulize swali kama hilo. Je wewe ni aina ya Watanzania ambao nikipewa uwaziri wa ujenzi utaniambia nimeukata sana lakini nikipewa uwaziri wa utamaduni na michezo utaniona sijapata kitu?
 
Ukosefu wa demokrasia miaka 5 ya muovu dikteta jiwe haikutoa fursa kwa wanasiasa wapya kuonesha vipaji vyao. Ndiyo maana watu wanaojulikana vipaji vyao ni wale wa enzi ya Kikwete.

Madhara ya kuongozwa na mwendazake ndiyo tunayaona
Jiwe aliteua watu ambao aliona wakiwa na PhD kama yeye au maprofessor basi wataweza kuwa viongozi wazuri. Alikuwa na mentality ya ajabu sana huyu mtu.
 
Kuna mwingine alikuwa waziri wakati wa JK akavurunda , akapewa ubalozi Japan akavurunda , Jiwe akampa ubalozi Kenya akavurunda , Mama kampa uRAS kwa wiki moja na kumpandisha kuwa mkuu wa mkoa .
Hebu fikiria sasa, mtu kama huyo ana nini cha maana ambacho Watanzania wengine hawana, hadi unaendelea kumng'ang'ania wakati anaharibu?
 
Wewe ni mmbea. Taja jina wacha majungu
Huu uzi sio wa kujadili mtu, ni wa kujadili jambo. Sasa kama wewe umezoea kujadili watu nenda kule kwenye thread za Mwajua kakojoa kitandani siku ya harusi yake
 
Angalau weka code ya mkoa ili tuweze kuchangia vizuri
Hapana Mkuu, changieni tabia ya viongozi wetu kuteua watu waliofanya makosa au skendo na kuondolewa kisha kurudishwa, sio kuchangia kumsema mtu fulani.
 
Ni kwa sababu tunategemea kupata viongozi wa nchi tuwatakao kwa kupitia sanduku la kura.

Hali hii itabadilika pindi tutakapopata kiongozi asiyetokana na chama cha siasa wala asiyetokana na boksi la kura.
 
Mwanasiasa akikwambia toka nje kuna mvua, usikimbilie kumuazima mwamvuli bali jiongeze uhakikishe kweli kuna mvua!, vinginevyo unapigwa.
 
Ni kwa sababu tunategemea kupata viongozi wa nchi tuwatakao kwa kupitia sanduku la kura.

Hali hii itabadilika pindi tutakapopata kiongozi asiyetokana na chama cha siasa wala asiyetokana na boksi la kura.
Ninaweza kukubaliana nawe nikielewa atapatikana vipi/kwa njia zipi kiongozi huyo.

Lakini pia kuna njia nyingine ambayo sijui kwa nini inawawia vigumu waTanzania kuitumia njia hii rahisi, lakini wanakubali kuendelea tu na ulaghai wanaopewa miaka yote.

Labda niseme tu kwamba, pengine ni kukosa mtu/watu (wachache wanaowaamini kuwaongoza) ili wasimamie mabadiliko wanayoweza kuyafanya waTanzania wenyewe kwa umoja wao.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…