Sifa za Manabii wa uongo

Sifa za Manabii wa uongo

Yesu Anakuja

JF-Expert Member
Joined
Apr 10, 2019
Posts
12,675
Reaction score
25,924
1. Wanajali zana pesa kuliko kumtumikia Mungu.

2. Wanaamini Yesu sio Mungu.

3. WANA MADHABAHU ZAO, hata maombi wanaomba kwa madhabahu ya mtumishi huo, sio kwa Jina la Yesu, wanaamini madhabahu yao ina nguvu, kumbe Nguvu zetu zinapaswa zitokane na Roho.

4. Injili zao muda mwingi ni za miujiza tu, kujisifia kuwa wana upako, hawahubiri wokovu, toba, utakatifu na uongozi wa Roho. Hii haimaanishi Mungu hawezi fanya miujiza, wanaifanya, ila wao wanaifanya ya shetani, hawana Mungu. Mungu anataka kwanza roho yako, mengine utazidishiwa.

5. Akiwa anahubiri, ANAKUWA NA LICHAWA PEMBENI la kupromote kurudia kile alichotamka, ili kumpa mori na kuhamasisha waumini, hii ni kwasababu hawana Roho Mtakatifu wa kugusa mioyo ya watu, wanatumia nguvu za mwili kuaminisha waumini kile wanachohubiri.

6. Wanapenda sana KUSIFIWA NA WAUMNINI wao kuliko hata kumsifia Mungu, wanapenda kutangazwa sana wao kuliko hata kumtangaza Mungu.

7. WANA KIBURI CHA PESA utafikiri za kwao kumbe ni zile zile sadaka mnatoa anajifanya za kwake na yeye ni tajiri, wanapenda sana kusifia serikali, kwasababu wanaiogopa.

8. WANATEMBEA NA MABODIGADI hata mahali pasipo na ulazima, ila waumini wanaowahubiria hawana ulinzi wowote.

9. WANAPENDA ANASA, muda mwingi wapo mitandaoni kurusha picha walivyovaa vizuri na kuwatamkia watu ahadi za mambo mema, badala ya kutangaza injili iletayo wokovu wa roho.

10. WANACHANGANYA BIASHARA NA INJILI. Huwezi kutumikia mabwana wawili, never.

11. Wanapinga Nguvu za Mungu, kwa maana ya ROHO MTAKATIFU, ujazo wa Roho na kuomba kwa Roho. Hutakuja kuwaona wanahubiri ujazo wa Roho, ni kwasababu hawanaye.

12. WANAUJENGA ZAIDI MWILI KULIKO ROHO
. Majority ni masharobaro, hata hujui wanamtafuta Mungu maombi na kufunga saa ngapi. Hatusemi mtu awe mchafu, ila unashangaa wao muda wote wamevaa kisharobaro, wanajichubua, wanaujali mwili zaidi kuliko hata roho zao.

13. MAHUBIRI YAO MAKAVUUU HATA KAMA UTAONA KUNA MIUJIZA. Ni kwasababu hawana Roho Mtakatifu, ila roho mchafu. Hiyo miujiza jua ni ya shetani, shetani naye hufanya miujiza ili kulaghai.

14. WANAVAA NGOZI YA KONDOO KUJIFANYA NI WATAKATIFU ILI WAWAPATE WENGI, lakini kumbe ni mbwa mwitu walaluao. Mabinti wengi wana siri nzito sana na hawa manabii wa uongo wa kisasa" Jihadharini na manabii wa uongo, watu wanaowajia wamevaa mavazi ya kondoo, walakini kwa ndani ni mbwa-mwitu wakali." (Mathayo 7:15)

15. Wapo kwa ajili ya kuwadanganya watu wasimwabudu Mungu wa kweli." Yesu akajibu, akawaambia, Angalieni, mtu asiwadanganye. Kwa sababu wengi watakuja kwa jina langu, wakisema, Mimi ni Kristo; nao watadanganya wengi."(Mathayo 24:4-5).

16. WANAFANYA MIUJIZA KWA NJIA ZISIZO ZA KI MUNGU ili waweze kuwapoteza watu. " Kwa maana watatokea makristo wa uongo, na manabii wa uongo, nao watatoa ishara kubwa na maajabu; wapate kuwapoteza, kama yamkini, hata walio wateule."(Mathayo 24:24).

17. WANAMWABUDU, WANAMTANGAZA NA KUFANYA KAZI ZA MPINGA KRISTO. " Watoto, ni wakati wa mwisho; na kama vile mlivyosikia kwamba mpinga Kristo yuaja, hata sasa wapinga Kristo wengi wamekwisha kuwapo. Kwa sababu hiyo twajua ya kuwa ni wakati wa mwisho."(1Yohana 2:18)

18. Hawamkubali Yesu hata kama wanajionyesha kuwa wanamwamini lakini kazi zao siyo za Kikristo kwa hiyo hawana Mungu ndani yao. " Ni nani aliye mwongo ila yeye akanaye ya kuwa Yesu ni Kristo? Huyo ndiye mpinga Kristo, yeye amkanaye Baba na Mwana.

19. Kila amkanaye Mwana, hanaye Baba; amkiriye Mwana anaye Baba pia." (1Yohana 2:22-23)

20. Kazi zao hazitokani na Mungu. " Wapenzi, msiiamini kila roho, bali zijaribuni hizo roho, kwamba zimetokana na Mungu; kwa sababu manabii wa uongo wengi wametokea duniani." (1Yohana 4:1).

21. MAFUNDISHO YAO NI YA UONGO. " Lakini kuliondokea manabii wa uongo katika wale watu, kama vile kwenu kutakavyokuwako waalimu wa uongo, watakaoingiza kwa werevu uzushi wa kupoteza, wakimkana hata Bwana aliyewanunua, wakijiletea uharibifu usiokawia." (2Petro 2:1).

22. UNABII WAO NI KWA MTAZAMO WAO NA MAAGIZO KUTOKA KUZIMU. " Ndipo BWANA akaniambia, Hao manabii wanatabiri uongo kwa jina langu mimi; mimi sikuwatuma, wala sikuwaamuru, wala sikusema nao; wanawapeni unabii wa maono ya uongo, na uaguzi, na neno la ubatili, na hadaa ya mioyo yao." (Yeremia 14:14).

23. Wengi wanaigiza na kulitaja jina la Bwana visivyo katika unabii wao na miujiza yao ili watu wajue kuwa wanatumiwa na kumbe siyo kweli. " Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi?" (Mathayo 7:22).
 
Ni muhimu kuelewa hili. Ukristo wa kweli upo, na tupo wakristo wengi tu wa kweli. ila kuna mambwa mwitu kibao wameingia, wengine walikuwa waislam, kama yule jamaa alikuwa muislam akawa mchungaji anayehubiri zinaa tu na kulala na wanawake. wamepotoka, wanatafuta pesa. tukiandika hivi tunashauri watu wawe makini, watu wa dini zote wameanza kujifanya wakristo ili wapige pesa, ila generally, usipokuwa Mkristo sehemu yako ni katika ziwa liwakalo moto na kiberiti. kama ukisema ulinganishe, dini ya mood ndiyo ya uongo kuliko dini hata za kipagani. haina reasonability kabisa kabisa.

kwenu ninyi mlioamua kuwa wakristo, jueni kwamba wapo manabii wa uongo ambao Yesu alitabiri watatokea. na hii inaonyesha kwamba Ukristo ni imani ya kweli, ndio maana hata Yesu aliyoyatabiri yanatokea, alisema kutatokea manabii wa uongo, na kweli wametokea. Yesu asingesema haya yangetokea, tungedoubt ukristo.
 
Zote ni sahihi isipokuwa No.2
2. Wanaamini Yesu sio Mungu.
Yohana 20:17
Yesu akamwambia: “Acha kuning’ang’ania, kwa maana bado sijapanda kwenda kwa Baba. Lakini nenda kwa ndugu zangu, nawe uwaambie, ‘Ninapanda kwenda kwa Baba yangu na Baba yenu na kwa Mungu wangu na Mungu wenu.

Yesu sio Mungu.
Mathayo 16:16,17
Simoni Petro akajibu: “Wewe ndiye Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai.” 17 Yesu akamwambia: “Mwenye furaha ni wewe, Simoni mwana wa Yona, kwa sababu mwili na damu havikukufunulia hilo, bali Baba yangu aliye mbinguni ndiye aliyekufunulia.
 
Namba 13 mahubiri yao ni makavuu, unamaanisha nini kusema mahubiri yao ni makavu?
 
wa kwanza Mwamposa kwa hapa tz for now.

sijui kwa nini watu akil8 zao zikoje yani, wanadanganywa kipuuzi wananunu sjui maji sjui mafuta ati imeombewa.

anyway nisiongee sana cas namjua personally, ni anatafta pesa tu kwa hiyo njia, na wajinga mnapatwa kwelikweli.

Mungu yupo, muombe wewe binafsi atasikia maombi yako na atajibu anavoona yeye, ndio nenda mskitini, nenda kanisani ili kufundishwa maelekekezo ya Mungu, sio kwa hao wahuni kina mwamposa, au hadi tuwaletee ushahidi ndio muelewe? haya sasa
 
Namba 13 mahubiri yao ni makavuu, unamaanisha nini kusema mahubiri yao ni makavu?
Ni makavu maana utendaji wa miujiza yao unatokea nje ya mioyo yao .
Mithali 4:23 - Linda moyo wako kuliko yote uyalindayo , maana ndiko zitokako chemchemi za uzima . Chemchemi za mto ( Roho mtakatifu) zinatiririka kutokea ndani ya moyo wa mtu , sio nje .
 
Zote ni sahihi isipokuwa No.2
2. Wanaamini Yesu sio Mungu.
Yohana 20:17
Yesu akamwambia: “Acha kuning’ang’ania, kwa maana bado sijapanda kwenda kwa Baba. Lakini nenda kwa ndugu zangu, nawe uwaambie, ‘Ninapanda kwenda kwa Baba yangu na Baba yenu na kwa Mungu wangu na Mungu wenu.

Yesu sio Mungu.
Mathayo 16:16,17
Simoni Petro akajibu: “Wewe ndiye Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai.” 17 Yesu akamwambia: “Mwenye furaha ni wewe, Simoni mwana wa Yona, kwa sababu mwili na damu havikukufunulia hilo, bali Baba yangu aliye mbinguni ndiye aliyekufunulia.
kwa msiojua, kwa literal meaning ya kiyahudi, mtu akisema yeye ni mwana wa Mungu maana yake ni kwamba "yeye ni Mungu aliyekuja kujidhihirisha katika Mwili" ila ni yule yule Mungu, ndio maana Wayahudi walikuwa wanaokota mawe na kutaka kumpiga kwasababu walisema anajiita yeye ni Mungu. na hata kwenye mashtaka yake, wayahudi walitoa hoja kwamba huyu anajifanya yeye ni Mungu, ndio maana walitaka asulibishwe. hivyo, Yesu mwenyewe kujiita Mwana wa Mungu, alikuwa anamaanisha yeye ndiye Mungu. kwahiyo jueni kwamba Yesu ni Mungu, na alijiita Mungu.
 
Ni muhimu kuelewa hili. Ukristo wa kweli upo, na tupo wakristo wengi tu wa kweli. ila kuna mambwa mwitu kibao wameingia, wengine walikuwa waislam, kama yule jamaa alikuwa muislam akawa mchungaji anayehubiri zinaa tu na kulala na wanawake. wamepotoka, wanatafuta pesa. tukiandika hivi tunashauri watu wawe makini, watu wa dini zote wameanza kujifanya wakristo ili wapige pesa, ila generally, usipokuwa Mkristo sehemu yako ni katika ziwa liwakalo moto na kiberiti. kama ukisema ulinganishe, dini ya mood ndiyo ya uongo kuliko dini hata za kipagani. haina reasonability kabisa kabisa.

kwenu ninyi mlioamua kuwa wakristo, jueni kwamba wapo manabii wa uongo ambao Yesu alitabiri watatokea. na hii inaonyesha kwamba Ukristo ni imani ya kweli, ndio maana hata Yesu aliyoyatabiri yanatokea, alisema kutatokea manabii wa uongo, na kweli wametokea. Yesu asingesema haya yangetokea, tungedoubt ukristo.
Kwaiyo hata mwamposa alikuwa muislam,kiboko ya wachawi nae alikuwa muislam,gwajima nae muislam.
 
wa kwanza Mwamposa kwa hapa tz for now.

sijui kwa nini watu akil8 zao zikoje yani, wanadanganywa kipuuzi wananunu sjui maji sjui mafuta ati imeombewa.

anyway nisiongee sana cas namjua personally, ni anatafta pesa tu kwa hiyo njia, na wajinga mnapatwa kwelikweli.

Mungu yupo, muombe wewe binafsi atasikia maombi yako na atajibu anavoona yeye, ndio nebda mskitini, nenda kanisani ili kufundishwa maelekekezo ya Mungu, sio kwa hao wahuni kina mwamposa, au hadi tuwaletee ushahidi ndio muelewe? haya sasa
Acha wapigwe,ukiwasanua watakuambia we kobazi gaidi
 
kuna nabii kamla mke waaliekua katibuwake walipishana kwenye mambo yamaslahi katibu anaenda kufunga kanisa lake

mke wakatibu alikua mtunza hazina Wakanisa mchungaji akatumia nafasi hio kumla mke wamwenzake😁😁😁😁

haowaumini anavyowala sasa siopoa
 
Hapo namba 7 pamenigusa kuwa wanapenda kujikomba kwa serikali maana wanaogopa
Nimekumbuka mhubiri mmoja wa hivi karibuni kesha wageuka wenzake tayari kuwa YESU sio MUNGU hata mimi nakubaliana naye YESU sio MUNGU wala sio nabii ila YESU ni Masiha cheo cha juu kuliko nabii ila cha chini ya MUNGU Sawa na mama Samia na Kassim Majaliwa
 
kwa msiojua, kwa literal meaning ya kiyahudi, mtu akisema yeye ni mwana wa Mungu maana yake ni kwamba "yeye ni Mungu aliyekuja kujidhihirisha katika Mwili" ila ni yule yule Mungu, ndio maana Wayahudi walikuwa wanaokota mawe na kutaka kumpiga kwasababu walisema anajiita yeye ni Mungu. na hata kwenye mashtaka yake, wayahudi walitoa hoja kwamba huyu anajifanya yeye ni Mungu, ndio maana walitaka asulibishwe. hivyo, Yesu mwenyewe kujiita Mwana wa Mungu, alikuwa anamaanisha yeye ndiye Mungu. kwahiyo jueni kwamba Yesu ni Mungu, na alijiita Mungu.
Swali kwako Yesu Anakuja, MUNGU aliwahi kufa?
 
Manabii wote na viongozi wote wa dini ni waongo kwa vile huyo Mungu wanaye hangaika kumhubiri miaka nenda rudi, hajawahi kuwepo, hayupo na hata uwezekano wa kuwepo kwake Haupo.
 
Hata wewe haufi mkuu bali unatoka tu kwenye huu mwili uharibikao ambao asili yake ni udongo hivyo unarudi kwenye udongo.
Sawa, mimi nataka jibu la Mungu alikufa? Mwili wa Bwana Yesu ulirudi mavumbini?

Usome Wafilipi 2: 5 - 6, Nimeanza na mstari wa 5 ili upate kujua anayezungumzwa ni nani, lengo kuu ni mstari wa 6
 
Back
Top Bottom