Nikifa MkeWangu Asiolewe
JF-Expert Member
- Feb 26, 2024
- 6,944
- 14,351
Heshima kwenu wakuu!
Niliazimia siku Moja nitembelee morogoro wilaya ya Gairo na Mvumero! Hatimae ikawadia na ikaenda sawa sawia kabisaa...
Kutoka kahama Hadi Gairo morogoro safari ilianza saa2:30.
Gari ilikuwa na changamoto kadhaa hasa kuharibika na Hadi kufika saa9 arasiri nikawa nimewasili salama Gairo.
Fuatana Nami nikupitishe Kwa machache kati ya mengi niliyoyaona.
Nilianza kuangalia Fursa zilizopo kandokando ya barabara kuu ya yaani ya kwenda Dar.
Fursa za uwekezaji zilizo Nje Nje nilizo ziona.
Maeneo hayo unaweza Jenga shule, ufugaji na kilimo Cha umwagiliaji japo itakupasa uchimbe kisima Kwa maji ya Uhakika
Safari yangu ndefu Sasa imetoka Barabara kuu na kushika barabara ya IYOGWE barabara hii itanipeleka hadi mpakani kati ya Morogoro na Tanga(Gairo &Tanga)
Nikiwa na usafiri wa pikpik Mimi pamoja na mwenyeji wangu. Sikuwa na budi ya kuweka full Tank maana nilihakikishiwa sitajutia kabisa na safari.....
Tukaanza ardhi yenye rutuba kiasi baridi kiasi likituandama huku milima ya uluguru ikiwa imefunikwa na wingu zito na mwonekano maridhawa kabisa.
Safari yetu iliendelea vizuri kabisa Na Hivi ndivyo vijiji nilivyo vipita Gairo ukielekea mpakani.
Br ya iyogwe:-
chakwale,
Nguyami,
Idibo,
itaragwe,
makuyu na Iyogwe.
(Kuna baadhi ya vijiji sikuona ubao) Pikipiki ilikuwa masaa....
Vijijini Hivi vipi wilaya ya Gairo morogoro
Na vinafaa sana Kwa ufugaji ila mifugo kama kuku,nguruwe ama ng'ombe wa maziwa kwani ni makazi ya watu.
Ukifuga mbuzi bila shaka utasumbuana na wakazi.
Nimefika mpakani Sasa
Sasa unaingia Mkoa wa Tanga..
Baada tu ya kutoka mpakani Kuna mto nahisi ndo unatenganisha Gairo na kikunde.
Hapo unakutana na mto na wakazi wake waliendelea na shughuli za kilimo Cha umwagiliaji.
Kwa namna nilichoona pale jinsi ya eneo lilivyo na kinachofanyika pale niliona ni mzaha mkubwa. Maji ni ya kutekenya tu lakini kinacholimwa ni kidogo sana ardhi Ina rutuba Hali ya hewa nzuri.
Nilipofika KIKUNDE SENTA Nilikuta vijana wamekaa wanaotoa moto hawana habari na wengine nikawaona wanaranda tu mtaani kwenye vijiwe nilisitikika sana kuona vijana hawana habari kabisa na fursa nilizo ziona Mimi!!
Ukweli ni kwamba pamoja na ardhi kuanzia kikunde nk Inakubali sana Kwa mazao kama mahindi, maharage,mihogo, Kwa kifupi karibia Kila zao la nafaka linakubali maeneo hayo
Wenyeji watatusaidia hapa.
Tu
Ardhi yenye rutuba mito yenye maji lakini hakuna mazao ya umwagiliaji!
Ardhi inalipa sana Kwa kilimo Cha matunda kwani Kwa macho yangu nimeona miti ya miembe(kienyeji) imestawi sana na Bahati nzuri lazima bondeni kuwe na mto
Ardhi ni nzuri Kwa uwekezaji wa kilimo na huku Sasa hata ufunge ng'ombe wa kwenda kuchunga na jioni uwarudishe panastahili!
Shauku Bado ikiwa inahitaji kuendelea kusonga mbele zaidi na kuona namna halisi ya Nchi ya maziwa na Asali
Baada ya kutoka Kikunde Kuna vijiji kama..
kikunde,
ludewa,
mafulila,Tunguli,
Lusane
Hapo Tunguli Kuna pori kubwa na zuri Kwa kilimo na ufugaji barabara ya uhakika japo ni vumbi.
Tunguli ni pazuri sana Kwa uwekezaji mkubwa.
Nimeona Kwa macho yangu watu wakifyeka pori Kwa ajiri ya
kilimo nk.
Hatimae kipande Cha Tanga nikakimaliza na kuingia wilaya ya Mvomero (morogoro)
Swadakta kabisaa mazingira & Hali ya hewa ilinivutia kuliko kifani!!!
Ikanilazimu kutoka moyoni nipambatize Kwa jina jipya la Thailand.
Kwani sehemu hii ni sehemu ambayo kijogorafia imekaa kama ughaibuni(Thailand japo sijafika)
Misitu minene yenye ukijani kibichi kabisa kama paradiso! Ukiangalia baadhi ya clip za Thailand utakubaliana Nami pasina shaka yoyote Ile!
Kwa wale wafanyakazi unayependa mazingira kama Yale ni muda wako Sasa wa kwenda kuona huko kwenye vijiji Hivi...
kibati,
kibogoji,
masimba,
Difinga,
Apendae,
Kwakwempe,
magotwe,
Kwa Dole
Lusanga
Tuliani,
manyiga,
mlaguzi.
Dakawa,
Hembeti,
Magole,
Dumila feli,
Dumila,
Hapa Kwa Retirement panafaa mnoo Kuna baadhi ya sehem nzuri,nzuri sana,na nzuri kabisa!!!
Ni juu Yako wewe Sasa wapi utapapenda
Hapo nimeunganisha Hadi Dumila.. maeneo yote hayo unalima muda wowote ukitaka
Niliona Kwa macho yangu Nchi hii Ina Tiririka maziwa na Asali.
************************
Pamoja na hayo yote nilichojifunza nikuwa
Vijana wa maeneo Tajwa ni wavivu usipime!
Nilicho shangaa nikaenda kupata supu halafu tukakoswa limao na kuletewa limao la unga zile zinauzwa kwenye pakiti Ili Hali ardhi Ile ukipanda mti haihitaji hata kumwagilia Cha ajabu limao ni anasa na vijana wapo tu.
Vijana nawaomba tutoke mjini kama huna issue ya maana.
Manyanza Toka magetoni Toka Dar uachane na biashara ya kupiga chabo wazaramo wakimwanga ladhi.
Niishie hapa nitaendelea kwenye comment
Haya ndiyo mazingira murua kabisa ya baadhi ya vijiji/vitongoji Tajwa hapo juu.
Fenesi hili nilijipatia Kwa Tsh1000 hapo ni Kwa Apendae.
Ardhi yenye maziwa na Asali.
Sehemu tulivu sana huku sauti ndege za ndege zikiimba utukufu wa Mungu!!
hapo passion3 zinauzwa Kwa 200 ndizi3 sh 200 embe2 dodo og zinauzwa500.
Tafadhar Endelea kubaki hapa.
Nyumba hizi uzionazo ni kando kando ya barabara.uzuri ni kwamba njia inapitika Kwa Uzuri bila shida yoyote.
NB: Picha zote hizi zimepigwa kiangazi 17/11/2024.
Kama mahitaji video zipo nzuri kabisaa!! Niwezeshe vocha iwe ya jero ama buku niweke hapa nitumie Pm.
Ahsanteen sana.
Niliazimia siku Moja nitembelee morogoro wilaya ya Gairo na Mvumero! Hatimae ikawadia na ikaenda sawa sawia kabisaa...
Kutoka kahama Hadi Gairo morogoro safari ilianza saa2:30.
Gari ilikuwa na changamoto kadhaa hasa kuharibika na Hadi kufika saa9 arasiri nikawa nimewasili salama Gairo.
Fuatana Nami nikupitishe Kwa machache kati ya mengi niliyoyaona.
Nilianza kuangalia Fursa zilizopo kandokando ya barabara kuu ya yaani ya kwenda Dar.
Fursa za uwekezaji zilizo Nje Nje nilizo ziona.
Maeneo hayo unaweza Jenga shule, ufugaji na kilimo Cha umwagiliaji japo itakupasa uchimbe kisima Kwa maji ya Uhakika
Safari yangu ndefu Sasa imetoka Barabara kuu na kushika barabara ya IYOGWE barabara hii itanipeleka hadi mpakani kati ya Morogoro na Tanga(Gairo &Tanga)
Nikiwa na usafiri wa pikpik Mimi pamoja na mwenyeji wangu. Sikuwa na budi ya kuweka full Tank maana nilihakikishiwa sitajutia kabisa na safari.....
Tukaanza ardhi yenye rutuba kiasi baridi kiasi likituandama huku milima ya uluguru ikiwa imefunikwa na wingu zito na mwonekano maridhawa kabisa.
Safari yetu iliendelea vizuri kabisa Na Hivi ndivyo vijiji nilivyo vipita Gairo ukielekea mpakani.
Br ya iyogwe:-
chakwale,
Nguyami,
Idibo,
itaragwe,
makuyu na Iyogwe.
(Kuna baadhi ya vijiji sikuona ubao) Pikipiki ilikuwa masaa....
Vijijini Hivi vipi wilaya ya Gairo morogoro
Na vinafaa sana Kwa ufugaji ila mifugo kama kuku,nguruwe ama ng'ombe wa maziwa kwani ni makazi ya watu.
Ukifuga mbuzi bila shaka utasumbuana na wakazi.
Nimefika mpakani Sasa
Sasa unaingia Mkoa wa Tanga..
Baada tu ya kutoka mpakani Kuna mto nahisi ndo unatenganisha Gairo na kikunde.
Hapo unakutana na mto na wakazi wake waliendelea na shughuli za kilimo Cha umwagiliaji.
Kwa namna nilichoona pale jinsi ya eneo lilivyo na kinachofanyika pale niliona ni mzaha mkubwa. Maji ni ya kutekenya tu lakini kinacholimwa ni kidogo sana ardhi Ina rutuba Hali ya hewa nzuri.
Nilipofika KIKUNDE SENTA Nilikuta vijana wamekaa wanaotoa moto hawana habari na wengine nikawaona wanaranda tu mtaani kwenye vijiwe nilisitikika sana kuona vijana hawana habari kabisa na fursa nilizo ziona Mimi!!
Ukweli ni kwamba pamoja na ardhi kuanzia kikunde nk Inakubali sana Kwa mazao kama mahindi, maharage,mihogo, Kwa kifupi karibia Kila zao la nafaka linakubali maeneo hayo
Wenyeji watatusaidia hapa.
Tu
Ardhi yenye rutuba mito yenye maji lakini hakuna mazao ya umwagiliaji!
Ardhi inalipa sana Kwa kilimo Cha matunda kwani Kwa macho yangu nimeona miti ya miembe(kienyeji) imestawi sana na Bahati nzuri lazima bondeni kuwe na mto
Ardhi ni nzuri Kwa uwekezaji wa kilimo na huku Sasa hata ufunge ng'ombe wa kwenda kuchunga na jioni uwarudishe panastahili!
Shauku Bado ikiwa inahitaji kuendelea kusonga mbele zaidi na kuona namna halisi ya Nchi ya maziwa na Asali
Baada ya kutoka Kikunde Kuna vijiji kama..
kikunde,
ludewa,
mafulila,Tunguli,
Lusane
Hapo Tunguli Kuna pori kubwa na zuri Kwa kilimo na ufugaji barabara ya uhakika japo ni vumbi.
Tunguli ni pazuri sana Kwa uwekezaji mkubwa.
Nimeona Kwa macho yangu watu wakifyeka pori Kwa ajiri ya
kilimo nk.
Hatimae kipande Cha Tanga nikakimaliza na kuingia wilaya ya Mvomero (morogoro)
Swadakta kabisaa mazingira & Hali ya hewa ilinivutia kuliko kifani!!!
Ikanilazimu kutoka moyoni nipambatize Kwa jina jipya la Thailand.
Kwani sehemu hii ni sehemu ambayo kijogorafia imekaa kama ughaibuni(Thailand japo sijafika)
Misitu minene yenye ukijani kibichi kabisa kama paradiso! Ukiangalia baadhi ya clip za Thailand utakubaliana Nami pasina shaka yoyote Ile!
Kwa wale wafanyakazi unayependa mazingira kama Yale ni muda wako Sasa wa kwenda kuona huko kwenye vijiji Hivi...
kibati,
kibogoji,
masimba,
Difinga,
Apendae,
Kwakwempe,
magotwe,
Kwa Dole
Lusanga
Tuliani,
manyiga,
mlaguzi.
Dakawa,
Hembeti,
Magole,
Dumila feli,
Dumila,
Hapa Kwa Retirement panafaa mnoo Kuna baadhi ya sehem nzuri,nzuri sana,na nzuri kabisa!!!
Ni juu Yako wewe Sasa wapi utapapenda
Hapo nimeunganisha Hadi Dumila.. maeneo yote hayo unalima muda wowote ukitaka
Niliona Kwa macho yangu Nchi hii Ina Tiririka maziwa na Asali.
************************
Pamoja na hayo yote nilichojifunza nikuwa
Vijana wa maeneo Tajwa ni wavivu usipime!
Nilicho shangaa nikaenda kupata supu halafu tukakoswa limao na kuletewa limao la unga zile zinauzwa kwenye pakiti Ili Hali ardhi Ile ukipanda mti haihitaji hata kumwagilia Cha ajabu limao ni anasa na vijana wapo tu.
Vijana nawaomba tutoke mjini kama huna issue ya maana.
Manyanza Toka magetoni Toka Dar uachane na biashara ya kupiga chabo wazaramo wakimwanga ladhi.
Niishie hapa nitaendelea kwenye comment
Haya ndiyo mazingira murua kabisa ya baadhi ya vijiji/vitongoji Tajwa hapo juu.
Fenesi hili nilijipatia Kwa Tsh1000 hapo ni Kwa Apendae.
Ardhi yenye maziwa na Asali.
Sehemu tulivu sana huku sauti ndege za ndege zikiimba utukufu wa Mungu!!
Tafadhar Endelea kubaki hapa.
Nyumba hizi uzionazo ni kando kando ya barabara.uzuri ni kwamba njia inapitika Kwa Uzuri bila shida yoyote.
NB: Picha zote hizi zimepigwa kiangazi 17/11/2024.
Kama mahitaji video zipo nzuri kabisaa!! Niwezeshe vocha iwe ya jero ama buku niweke hapa nitumie Pm.
Ahsanteen sana.