Sijajutia kabisa safari yangu ya Morogoro kuangalia maeneo (ardhi) ya uwekezaji

Sijajutia kabisa safari yangu ya Morogoro kuangalia maeneo (ardhi) ya uwekezaji

Heshima kwenu wakuu!

Niliazimia siku Moja nitembelee morogoro wilaya ya Gairo na Mvumero! Hatimae ikawadia na ikaenda sawa sawia kabisaa...

Kutoka kahama Hadi Gairo morogoro safari ilianza saa2:30.

Gari ilikuwa na changamoto kadhaa hasa kuharibika na Hadi kufika saa9 arasiri nikawa nimewasili salama Gairo.

Fuatana Nami nikupitishe Kwa machache kati ya mengi niliyoyaona.

Nilianza kuangalia Fursa zilizopo kandokando ya barabara kuu ya yaani ya kwenda Dar.

Fursa za uwekezaji zilizo Nje Nje nilizo ziona.

Maeneo hayo unaweza Jenga shule, ufugaji na kilimo Cha umwagiliaji japo itakupasa uchimbe kisima Kwa maji ya Uhakika

Safari yangu ndefu Sasa imetoka Barabara kuu na kushika barabara ya IYOGWE barabara hii itanipeleka hadi mpakani kati ya Morogoro na Tanga(Gairo &Tanga)

Nikiwa na usafiri wa pikpik Mimi pamoja na mwenyeji wangu. Sikuwa na budi ya kuweka full Tank maana nilihakikishiwa sitajutia kabisa na safari.....

Tukaanza ardhi yenye rutuba kiasi baridi kiasi likituandama huku milima ya uluguru ikiwa imefunikwa na wingu zito na mwonekano maridhawa kabisa.View attachment 3154970

Safari yetu iliendelea vizuri kabisa Na Hivi ndivyo vijiji nilivyo vipita Gairo ukielekea mpakani.

Br ya iyogwe:-
chakwale,
Nguyami,
Idibo,
itaragwe,
makuyu na Iyogwe.
(Kuna baadhi ya vijiji sikuona ubao) Pikipiki ilikuwa masaa....

Vijijini Hivi vipi wilaya ya Gairo morogoro

Na vinafaa sana Kwa ufugaji ila mifugo kama kuku,nguruwe ama ng'ombe wa maziwa kwani ni makazi ya watu.

Ukifuga mbuzi bila shaka utasumbuana na wakazi.

Nimefika mpakani Sasa
Sasa unaingia Mkoa wa Tanga..

View attachment 3154977
Baada tu ya kutoka mpakani Kuna mto nahisi ndo unatenganisha Gairo na kikunde.
Hapo unakutana na mto na wakazi wake waliendelea na shughuli za kilimo Cha umwagiliaji.

Kwa namna nilichoona pale jinsi ya eneo lilivyo na kinachofanyika pale niliona ni mzaha mkubwa. Maji ni ya kutekenya tu lakini kinacholimwa ni kidogo sana ardhi Ina rutuba Hali ya hewa nzuri.

Nilipofika KIKUNDE SENTA Nilikuta vijana wamekaa wanaotoa moto hawana habari na wengine nikawaona wanaranda tu mtaani kwenye vijiwe nilisitikika sana kuona vijana hawana habari kabisa na fursa nilizo ziona Mimi!!

Ukweli ni kwamba pamoja na ardhi kuanzia kikunde nk Inakubali sana Kwa mazao kama mahindi, maharage,mihogo, Kwa kifupi karibia Kila zao la nafaka linakubali maeneo hayo

Wenyeji watatusaidia hapa.


Tu

View attachment 3154979

View attachment 3154981
Ardhi yenye rutuba mito yenye maji lakini hakuna mazao ya umwagiliaji!
View attachment 3154983
Ardhi inalipa sana Kwa kilimo Cha matunda kwani Kwa macho yangu nimeona miti ya miembe(kienyeji) imestawi sana na Bahati nzuri lazima bondeni kuwe na mto

Ardhi ni nzuri Kwa uwekezaji wa kilimo na huku Sasa hata ufunge ng'ombe wa kwenda kuchunga na jioni uwarudishe panastahili!

Shauku Bado ikiwa inahitaji kuendelea kusonga mbele zaidi na kuona namna halisi ya Nchi ya maziwa na Asali

Baada ya kutoka Kikunde Kuna vijiji kama..

kikunde,
ludewa,
mafulila,Tunguli,
Lusane

Hapo Tunguli Kuna pori kubwa na zuri Kwa kilimo na ufugaji barabara ya uhakika japo ni vumbi.

Tunguli ni pazuri sana Kwa uwekezaji mkubwa.

Nimeona Kwa macho yangu watu wakifyeka pori Kwa ajiri ya
kilimo nk.
View attachment 3154985
View attachment 3154986
Hatimae kipande Cha Tanga nikakimaliza na kuingia wilaya ya Mvomero (morogoro)

Swadakta kabisaa mazingira & Hali ya hewa ilinivutia kuliko kifani!!!

Ikanilazimu kutoka moyoni nipambatize Kwa jina jipya la Thailand.

Kwani sehemu hii ni sehemu ambayo kijogorafia imekaa kama ughaibuni(Thailand japo sijafika)

Misitu minene yenye ukijani kibichi kabisa kama paradiso! Ukiangalia baadhi ya clip za Thailand utakubaliana Nami pasina shaka yoyote Ile!

Kwa wale wafanyakazi unayependa mazingira kama Yale ni muda wako Sasa wa kwenda kuona huko kwenye vijiji Hivi...

kibati,
kibogoji,
masimba,
Difinga,
Apendae,
Kwakwempe,
magotwe,
Kwa Dole
Lusanga
Tuliani,
manyiga,
mlaguzi.
Dakawa,
Hembeti,
Magole,
Dumila feli,
Dumila,

Hapa Kwa Retirement panafaa mnoo Kuna baadhi ya sehem nzuri,nzuri sana,na nzuri kabisa!!!

Ni juu Yako wewe Sasa wapi utapapenda

Hapo nimeunganisha Hadi Dumila.. maeneo yote hayo unalima muda wowote ukitaka

Niliona Kwa macho yangu Nchi hii Ina Tiririka maziwa na Asali.
************************
Pamoja na hayo yote nilichojifunza nikuwa
Vijana wa maeneo Tajwa ni wavivu usipime!

Nilicho shangaa nikaenda kupata supu halafu tukakoswa limao na kuletewa limao la unga zile zinauzwa kwenye pakiti Ili Hali ardhi Ile ukipanda mti haihitaji hata kumwagilia Cha ajabu limao ni anasa na vijana wapo tu.

Vijana nawaomba tutoke mjini kama huna issue ya maana.
Manyanza Toka magetoni Toka Dar uachane na biashara ya kupiga chabo wazaramo wakimwanga ladhi.

Niishie hapa nitaendelea kwenye comment
View attachment 3154987
Haya ndiyo mazingira murua kabisa ya baadhi ya vijiji/vitongoji Tajwa hapo juu.View attachment 3154988
Fenesi hili nilijipatia Kwa Tsh1000 hapo ni Kwa Apendae.



Ardhi yenye maziwa na Asali.View attachment 3154992View attachment 3154993
Sehemu tulivu sana huku sauti ndege za ndege zikiimba utukufu wa Mungu!!View attachment 3154998hapo passion3 zinauzwa Kwa 200 ndizi3 sh 200 embe2 dodo og zinauzwa500.View attachment 3155001View attachment 3155000
Tafadhar Endelea kubaki hapa.
View attachment 3155002
Nyumba hizi uzionazo ni kando kando ya barabara.uzuri ni kwamba njia inapitika Kwa Uzuri bila shida yoyote.


NB: Picha zote hizi zimepigwa kiangazi 17/11/2024.

Kama mahitaji video zipo nzuri kabisaa!! Niwezeshe vocha iwe ya jero ama buku niweke hapa nitumie Pm.

Ahsanteen sana.
Duuh kweli utajiri unakuja kwa kuwa na taarifa sahhhi mapasheni hayo 3 ya 200 huku towmn moto mjini ni 1000 matatu maana yake hapo ukiweka transport ya sh 150 kwenye hiyo 200 ukija mjini kuna faida yako ya 650 kwa hayo mapasheni umenunua 200.

Fenesi kubwa kama hilo la 1000 ukija town hukosi faida ya kuanzia 3000. Maana yake ukiwekeza 400,000 kwa mwezi, una uwezo wa kupata faida mara mbili yake yaani 800,000 kama faida kila mwezi.

Assuming mzigo utaonunua utauzika bila kelele
 
Heshima kwenu wakuu!

Niliazimia siku Moja nitembelee morogoro wilaya ya Gairo na Mvumero! Hatimae ikawadia na ikaenda sawa sawia kabisaa...

Kutoka kahama Hadi Gairo morogoro safari ilianza saa2:30.

Gari ilikuwa na changamoto kadhaa hasa kuharibika na Hadi kufika saa9 arasiri nikawa nimewasili salama Gairo.

Fuatana Nami nikupitishe Kwa machache kati ya mengi niliyoyaona.

Nilianza kuangalia Fursa zilizopo kandokando ya barabara kuu ya yaani ya kwenda Dar.

Fursa za uwekezaji zilizo Nje Nje nilizo ziona.

Maeneo hayo unaweza Jenga shule, ufugaji na kilimo Cha umwagiliaji japo itakupasa uchimbe kisima Kwa maji ya Uhakika

Safari yangu ndefu Sasa imetoka Barabara kuu na kushika barabara ya IYOGWE barabara hii itanipeleka hadi mpakani kati ya Morogoro na Tanga(Gairo &Tanga)

Nikiwa na usafiri wa pikpik Mimi pamoja na mwenyeji wangu. Sikuwa na budi ya kuweka full Tank maana nilihakikishiwa sitajutia kabisa na safari.....

Tukaanza ardhi yenye rutuba kiasi baridi kiasi likituandama huku milima ya uluguru ikiwa imefunikwa na wingu zito na mwonekano maridhawa kabisa.View attachment 3154970

Safari yetu iliendelea vizuri kabisa Na Hivi ndivyo vijiji nilivyo vipita Gairo ukielekea mpakani.

Br ya iyogwe:-
chakwale,
Nguyami,
Idibo,
itaragwe,
makuyu na Iyogwe.
(Kuna baadhi ya vijiji sikuona ubao) Pikipiki ilikuwa masaa....

Vijijini Hivi vipi wilaya ya Gairo morogoro

Na vinafaa sana Kwa ufugaji ila mifugo kama kuku,nguruwe ama ng'ombe wa maziwa kwani ni makazi ya watu.

Ukifuga mbuzi bila shaka utasumbuana na wakazi.

Nimefika mpakani Sasa
Sasa unaingia Mkoa wa Tanga..

View attachment 3154977
Baada tu ya kutoka mpakani Kuna mto nahisi ndo unatenganisha Gairo na kikunde.
Hapo unakutana na mto na wakazi wake waliendelea na shughuli za kilimo Cha umwagiliaji.

Kwa namna nilichoona pale jinsi ya eneo lilivyo na kinachofanyika pale niliona ni mzaha mkubwa. Maji ni ya kutekenya tu lakini kinacholimwa ni kidogo sana ardhi Ina rutuba Hali ya hewa nzuri.

Nilipofika KIKUNDE SENTA Nilikuta vijana wamekaa wanaotoa moto hawana habari na wengine nikawaona wanaranda tu mtaani kwenye vijiwe nilisitikika sana kuona vijana hawana habari kabisa na fursa nilizo ziona Mimi!!

Ukweli ni kwamba pamoja na ardhi kuanzia kikunde nk Inakubali sana Kwa mazao kama mahindi, maharage,mihogo, Kwa kifupi karibia Kila zao la nafaka linakubali maeneo hayo

Wenyeji watatusaidia hapa.


Tu

View attachment 3154979

View attachment 3154981
Ardhi yenye rutuba mito yenye maji lakini hakuna mazao ya umwagiliaji!
View attachment 3154983
Ardhi inalipa sana Kwa kilimo Cha matunda kwani Kwa macho yangu nimeona miti ya miembe(kienyeji) imestawi sana na Bahati nzuri lazima bondeni kuwe na mto

Ardhi ni nzuri Kwa uwekezaji wa kilimo na huku Sasa hata ufunge ng'ombe wa kwenda kuchunga na jioni uwarudishe panastahili!

Shauku Bado ikiwa inahitaji kuendelea kusonga mbele zaidi na kuona namna halisi ya Nchi ya maziwa na Asali

Baada ya kutoka Kikunde Kuna vijiji kama..

kikunde,
ludewa,
mafulila,Tunguli,
Lusane

Hapo Tunguli Kuna pori kubwa na zuri Kwa kilimo na ufugaji barabara ya uhakika japo ni vumbi.

Tunguli ni pazuri sana Kwa uwekezaji mkubwa.

Nimeona Kwa macho yangu watu wakifyeka pori Kwa ajiri ya
kilimo nk.
View attachment 3154985
View attachment 3154986
Hatimae kipande Cha Tanga nikakimaliza na kuingia wilaya ya Mvomero (morogoro)

Swadakta kabisaa mazingira & Hali ya hewa ilinivutia kuliko kifani!!!

Ikanilazimu kutoka moyoni nipambatize Kwa jina jipya la Thailand.

Kwani sehemu hii ni sehemu ambayo kijogorafia imekaa kama ughaibuni(Thailand japo sijafika)

Misitu minene yenye ukijani kibichi kabisa kama paradiso! Ukiangalia baadhi ya clip za Thailand utakubaliana Nami pasina shaka yoyote Ile!

Kwa wale wafanyakazi unayependa mazingira kama Yale ni muda wako Sasa wa kwenda kuona huko kwenye vijiji Hivi...

kibati,
kibogoji,
masimba,
Difinga,
Apendae,
Kwakwempe,
magotwe,
Kwa Dole
Lusanga
Tuliani,
manyiga,
mlaguzi.
Dakawa,
Hembeti,
Magole,
Dumila feli,
Dumila,

Hapa Kwa Retirement panafaa mnoo Kuna baadhi ya sehem nzuri,nzuri sana,na nzuri kabisa!!!

Ni juu Yako wewe Sasa wapi utapapenda

Hapo nimeunganisha Hadi Dumila.. maeneo yote hayo unalima muda wowote ukitaka

Niliona Kwa macho yangu Nchi hii Ina Tiririka maziwa na Asali.
************************
Pamoja na hayo yote nilichojifunza nikuwa
Vijana wa maeneo Tajwa ni wavivu usipime!

Nilicho shangaa nikaenda kupata supu halafu tukakoswa limao na kuletewa limao la unga zile zinauzwa kwenye pakiti Ili Hali ardhi Ile ukipanda mti haihitaji hata kumwagilia Cha ajabu limao ni anasa na vijana wapo tu.

Vijana nawaomba tutoke mjini kama huna issue ya maana.
Manyanza Toka magetoni Toka Dar uachane na biashara ya kupiga chabo wazaramo wakimwanga ladhi.

Niishie hapa nitaendelea kwenye comment
View attachment 3154987
Haya ndiyo mazingira murua kabisa ya baadhi ya vijiji/vitongoji Tajwa hapo juu.View attachment 3154988
Fenesi hili nilijipatia Kwa Tsh1000 hapo ni Kwa Apendae.



Ardhi yenye maziwa na Asali.View attachment 3154992View attachment 3154993
Sehemu tulivu sana huku sauti ndege za ndege zikiimba utukufu wa Mungu!!View attachment 3154998hapo passion3 zinauzwa Kwa 200 ndizi3 sh 200 embe2 dodo og zinauzwa500.View attachment 3155001View attachment 3155000
Tafadhar Endelea kubaki hapa.
View attachment 3155002
Nyumba hizi uzionazo ni kando kando ya barabara.uzuri ni kwamba njia inapitika Kwa Uzuri bila shida yoyote.


NB: Picha zote hizi zimepigwa kiangazi 17/11/2024.

Kama mahitaji video zipo nzuri kabisaa!! Niwezeshe vocha iwe ya jero ama buku niweke hapa nitumie Pm.

Ahsanteen sana.
Hongera sana ndugu yangu tatizo watu wanakimbia vijijini.sababu ya Uchawi,nenda ukalime uone utakachovuna ndiyo maana watu wanajikatia tamaa
 
Kweli nchi yetu Mungu ameibariki sana ni sisi tu tunakosa hamasa pia serikali ndio ingewekeza maeneo kama hayo kupitia BBT na project nyingine nyingi sasa hivi tusingekuwa tunaletewa mahindi ya msaada na ngano kutoka Ukraine au Russia.
Ni aibu sana mkuu kuletewa chakula na sio aibu tu ni laana ndio maana inatutafuna Hadi Leo hii.

Nimepita maeneo kadhaa naona watu wanapalilia mpunga wengine wanavuna imagine!!

Hiyo barabara ya kutoka Turiani wanavuna mpunga sio mchezo.

Unapoamabiwa tuna uhaba na sukari unashindwa kuelewa serikali yetu Iko wapi na inafanya Nini!

Ng'ombe kule wanachunga ka wapo Eden japo hatujaiona
 
Hapo uliposema kuna pumba nyingi na za bei rahisi ndio pa kutia kambi ya kufuga nguruwe na kuku , unayanenepesha kwa wingi unapakia kwenda kuuza Dar ,aisee bonge la fursa mkuu
Chakula cha kuku na nguruwe hasa pumba maeneo mengi ni ghali sana
Nitakucheki pm
Mkuu ramani inasoma ni maeneo ya Tunguli Tanga tulipita kwenye machine Moja ya kusaga na kukoboa niliona na kushanga sana. Mimi pia ni mfugaji wa kuku kwetu Sasa Hivi ni 25k debe6 hapo ni kujaza gunia sio kupima halafu 10k

Unaweza ukatetema
 
Duuh kweli utajiri unakuja kwa kuwa na taarifa sahhhi mapasheni hayo 3 ya 200 huku towmn moto mjini ni 1000 matatu maana yake hapo ukiweka transport ya sh 150 kwenye hiyo 200 ukija mjini kuna faida yako ya 650 kwa hayo mapasheni umenunua 200.

Fenesi kubwa kama hilo la 1000 ukija town hukosi faida ya kuanzia 3000. Maana yake ukiwekeza 400,000 kwa mwezi, una uwezo wa kupata faida mara mbili yake yaani 800,000 kama faida kila mwezi.

Assuming mzigo utaonunua utauzika bila kelele
Mwaka 2017 nilinunua Dar embe dodo og 1500. Lakini hapo jero500 unapewa mawili mawili laiti kama tungeenda na gari mbona ningerudi na nauli yangu ingekuja Rudi tu!

Nilichukua mzigo mkubwa gharama ikaja kama6000 nikampa 15,000/= kulikuwa na watoto nikawachia buku2 kama urafiki nilikuwa na furaha sana
 
Hongera sana ndugu yangu tatizo watu wanakimbia vijijini.sababu ya Uchawi,nenda ukalime uone utakachovuna ndiyo maana watu wanajikatia tamaa
Kwakweli wachawi wanafelisha sana watu asee!! Isingelikuwa hivyo daah sijui tu. Lakini nitaenda nilishindwa Mimi ardhi wataikuta Watoto wetu na mambo yatakuwa yamebadilika
 
Tunguli Tanga
20241117_091751.jpg
 
Mkuu ramani inasoma ni maeneo ya Tunguli Tanga tulipita kwenye machine Moja ya kusaga na kukoboa niliona na kushanga sana. Mimi pia ni mfugaji wa kuku kwetu Sasa Hivi ni 25k debe6 hapo ni kujaza gunia sio kupima halafu 10k

Unaweza ukatetema
Kabisa , hapo ukiwa na kimtaji kiasi ,unafuga nguruwe wananenepa hasa ,msosi wa kutosha
 
Hili jina mbona linatisha mkuu ?
Tunguli tena ? ,Walifikiri nini mpaka kupaita tunguli ,au ni kijiji cha walozi na wachawi ?
Hata Mimi niliuliza mara3 nikaambiwa andika hivyo Tunguli mkuu. Bado nahitaji wenyeji wa eneo husika watupe abc zake. Hapa Kuna ardhi nzuri mno ya kulima matunda hasa maembe.
 
Back
Top Bottom