Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Mbona mimi ni wa kike mkuu😃😃Mbona kama kuna dalili huwa una mtongozA afu design demu nahisi hakupendi anakulia tu hela zAko...... najua umeandika msaada ila kama mwana saikolojia inaoneka unajitoa ila umgonge sasa mambo yameenda mlama.......
Dem asipokupenda ndo walivyo mkuu
Duuh, sawa.. Ila nadhani ungesoma kwanza kwa utulivu na kunielewa, ni sahihi kwake hata hajanipa taarifa kama wameruhusiwa na wanaendelea vizuri hadi narudi tena hospitali hawapo??? Seriously??Mimi nadhani tatizo ni wewe, sio huyo rafiki yako.
Msaada hasa wa matibabu ni spiritual and goal oriented. Ulipotoa msaada ulikua unalenga mtoto apone. Wewe mwenyewe umeshiriki matibabu na umejiridhisha kuwa ametibiwa, kiimani umeshapata baraka na malipo kwa Mungu. Inatosha. Sasa kama unataka ushukuriwe Na upostiwe, basi wewe hukutoa msaada kwa mtoto.
be thanksful, mtoto amepona.
Hello Ms Leejay49 , Pole sana kwa hili lilikutokea na ndivyo ilivyo watu wenye moyo wa huruma kama wewe ni wepesi sana wa kuumizwa. Ninachokushauri jitahidi sana kufanya mambo kwa kiasi na ukifanya jambo fanya pasipo kutegemea kupewa feedback au shukrani yoyote. Najua sana umbali wa kutoka Songea mjini mpaka Peramiho ni 25KM. Huyo Shoga yako hana shukrani ishi nae kwa akili na usijitoe sana kwake na hata kama unamsaidia msaidie nusu nusu sio full msaada, kwa mfano akitaka 10,000 mpe 7000 au 5000 tu na usitegemee shukraniHabari za asubuhi wana JF,
Iko hivi, nina rafiki yangu ana mtoto (naweza nikasema ni single mom) ila isieleweke vibaya, nilisomaga nae O level huko ila nikama bahati tu tumejikuta tunaishi tena mtaa mmoja.
Ijumaa jioni wakati natoka tu ofisini alinipigia Simu akaniambia anashida kama naweza nipitie nyumbani kwao nikamuone, kwakua nilikua sina ratiba nyingine nikasema isiwe tabu kabla sijafika nyumbani nikapitia.
Nilimkuta yuko good ila mwanaye alikua anaumwa sana ile mtoto kazidiwa na akaniambia ameshindwa kwenda hospitali hana hela na almost kila aliyempigia simu wamemuahidi tu tangu asubuhi na hakuna aliyemtumia mpaka muda huo sa 1 jioni inaelekea saa 2.
Kiukweli sikua na hela and i was totally broke, yaani wiki ile iliyoisha mwenyewe nimeishi tu kwasababu nina wazazi maana nilikua nina mambo mengi yananihitaji hela kiasi kwamba sikua nimebakiwa na hata Mia mbovu. Lakini nikasema kwenye suala la kuokoa maisha ya mtoto isiwe kesi nikamwambia ngoja nirudi kwanza nyumbani, nikamsimulia mama tukaongea na dada yangu wakasema tu hapa kwa harakaharaka hatuna namna tumdanganye tu mzee kitu chochote jioni hii atupe hela, kweli tukamshawishi mzee bila hiyana akanipa 150k nikamfata kwao tukaenda hospitali usiku uleule.
Mtoto akapewa huduma ya kwanza na baadhi ya vipimo wakamlaza ili asubuhi aendelee na matibabu mengine (muda wote huo anawapigia ndugu zake wakiwemo na baba wa mtoto hata simu hawampokelei wengine), asubuhi yake niliomba ruhusa kazini nikawaambia nitachelewa ili nione mtoto atakua anaendeleaje.
Case ya mtoto ikawa kubwa wakasema tuende nae hospitali nyingine kubwa (Peramiho nadhani watu wa songea wanaijua), kuna vipimo alivyoambiwa wampime vilikua vinahitaji hela almost kama laki 2 tena nikamwambia mama akanitumia tukafanikisha. Kwasababu kazini walikua wanapigapiga sana simu na nikaona wanaendelea vizuri na mama yake alikua ashafika nikamwambia naenda ofisini incase kimetokea chochote utatuambia nikampa na namba ya mama kama mimi nisipopokea ampigie, nikaondoka. The bad thing is nilikua busy busy sana hadi siku ikaisha sikuwatafuta tena.
Kinachoniumiza ni kwamba, jana mchana nilimpigia simu hakupokea nikaenda kwao sikukuta mtu, nikaenda hadi Peramiho tena kulivyo mbali nikaambiwa wameruhusiwa na hakunipa taarifa. Jioni nimeingia WhatsApp naona ameweka status nyingi nyingi kufungua nikawa naona amescreenshot miamala yote ya watu waliokua wanamtumia hela na kuwapa credits Mungu awabariki sana kwa kuokoa maisha ya mwanae maana alikua kwenye hali mbaya sana na nini nini. Screenshot kama kumi na kitu hivi na amewataja na majina kabisa...
Cha ajabu hiyo miamala hakuna hata wa mtu mmoja uliofikia hata 30k, wote ni hizo hizo tu efu10 ef5 ef7, kawaandikia macaption mazito mazito. Nimebaki najiuliza mbona alikua ananiambia hawapokei simu, na hela inaonekana walimtumia siku ileile ambayo aliniambia na mimi niende kwake kumuona( Nilikua nasoma tarehe na muda wa zile transactions ).
Mimi ambaye nilikua nae kuanzia siku ile hadi usiku nikaacha na kwenda kazini na tumeclear bills zote hata asante hajaniambia na wala taarifa kama wameruhusiwa hajanipa. Nimesubiri jana yote hadi leo saizi hajanipigia hata simu, Kina mama wananiuliza wanaendeaje nawaambia tu wanaendelea vizuri huku roho inauma.
Nimetenda wema nimeenda zangu wakuu, lakini bado roho inaniuma aisee, sijui nifanye nini nikae sawa😥😥
Asante mkuu, inabidi nianze kujifunza roho mbayaHello Ms Leejay49 , Pole sana kwa hili lilikutokea na ndivyo ilivyo watu wenye moyo wa huruma kama wewe ni wepesi sana wa kuumizwa. Ninachokushauri jitahidi sana kufanya mambo kwa kiasi na ukifanya jambo fanya pasipo kutegemea kupewa feedback au shukrani yoyote. Najua sana umbali wa kutoka Songea mjini mpaka Peramiho ni 25KM. Huyo Shoga yako hana shukrani ishi nae kwa akili na usijitoe sana kwake na hata kama unamsaidia msaidie nusu nusu sio full msaada, kwa mfano akitaka 10,000 mpe 7000 au 5000 tu na usitegemee shukrani
I hope hamna common friends maana kituo kinachofata ni "yule mnavoona ana kazi kumbe poyoyo, hela anaomba kwa wazazi wake...hana lolote...."Mimi angenishukuru tu ingetosha mkuu🙏.. Anionee wivu na aliona kabisa sina hela nilimuomba mama jamani😃😃
Watu tumetoka kwenye kaubavu kenu halafu mnataka tufanane. Huwez pingana na nature, mwanaume ni mwanaume tu.Binafsi nimefurahi.
Sikujua kumbe na nyie wanawake mnaumiaga mkifanywa chuma ulete.
Mwanaume akija kulalamika humu kafanywa chuma ulete na mdada, mnamponda mwanaume kuwa hana hela, wanaume wa jf tunanalalamika sana, tunakimbia majukumu, tule kwa jasho etc , mnamtetea mdada aliemchuna uyo mwanaume.
Itabidi mjue how it feels like, mtu ukijua kwamba ulikuwa used.
Ndo mpate taste ya sisi wanaume tunavojisikia Leejay49 Mrs Van
Pole Sana,Katika nafsi yako Na Moyo Wako Mkaribishe Mungu,Hesabu umetoa sadaka,peleka Maombi yako Kwa Mungu atakuondolea Maumivu Na utaendelea kusikia furahaNdio maana mimi sipendagi ujinga, acha wakuone na roho mbaya tu, unaweza kujitoa kumsaidia mtu na kumsomesha lakini na bado asione thamani yako ni kawaida tu, wewe ili moyo wako uwe na amani mchana aisee, mwambie ukweli kabisa ili uwe huru.
📌📌Huna haja ya kusubiri hiyo taarifa wala asante yake. Ukifanya jambo amua unalifanya kwa ajili ya wewe na sio kwa ajili ya mtu mwingine. Kwa hiyo ukifanya unakuwa umetimiza nia yako na kama mazingira hayakupi favour kuendelea na hilo, unaishia hapo kama ilivyotokea kwako.