Sijui kwanini nimeumia hivi

Sijui kwanini nimeumia hivi

ukute ndio tabia yake na hata baba mtoto ameshajionea mengi zaidi ya uliyoona wewe.. hapo unaweza kuita baba mtoto ni katili ukute ata alishaambiwa si mtoto wake!.
huko kupost jua kuna mtu alikuwa anapewa ujumbe na huyo wakupewa huo ujumbe ni aidha huyohuyo baba mtoto!. pole limekukuta na likushuke hivyo ndivyo baadhi ya wadada mlivyo ni wabinafsi wamwisho hakuna anaewafikia!.

kuhusu shukurani we tulia atakutafuta huenda kuna kitu ame plan.
Asante mkuu kwa ushauri mzuri 🙏🙏
 
Pole sana aisee.. Walau nimepata ahueni baada ya kuandika hapa maana nilikua naumia tu ndani kwa ndani
Utakuwa sawa ni suala la muda tu, mimi huwa nachekaga tu kama kontawa.

Watu wasichokijua watu wenye mioyo ya kusaidia ni wengi ila wenye uwezo wa kusaidia ni wachache mno na hustahili kuwapoteza hata mmoja labda wapoteze uhai.
 
Punguzeni kujifanya miungu watu.
Ww umeombwa hela huna unaanza kuomba na ww.

Ww sio Mungu, kama umeshindwa kumsaidia Mungu wake atamsaidia kupitia wengine, ww sema sina endelea na maisha yako.

Siwezi kukulaumu sana kwa sababu ww ni mwanamke, labda uliingiwa na roho ya huruma,. Ila ndo upate taste ya sisi tunavyojisikua tukihudumia na tunda likamegwa na mwingine, ww hapo umenyimwa credits tu umeumia hvo, hahahahaaa

Anyway pole. Jifunze kutokujiona mungu mtu, saidia unapoweza na kwa uwezo wako, ukiona unaingia hadi kukopa kisa kusaidia mtu basi fikiri mara 10 sabab inawezekana ukawa unafanya mistake kubwa sana
Ushauri mzuri sana

Unasaidia ulichonacho, unatoa sadaka ulichovuna wewe.

Sio ukope halafu usaidie, au katoe sadaka haiji. Wenye hekima walishasema kopesha kile unachoweza kupoteza. Sasa iweje ukopeshe kile usichoweza hata kuafford!! Why
 
Habari za asubuhi wana JF,

Iko hivi, nina rafiki yangu ana mtoto (naweza nikasema ni single mom) ila isieleweke vibaya, nilisomaga nae O level huko ila nikama bahati tu tumejikuta tunaishi tena mtaa mmoja.

Ijumaa jioni wakati natoka tu ofisini alinipigia Simu akaniambia anashida kama naweza nipitie nyumbani kwao nikamuone, kwakua nilikua sina ratiba nyingine nikasema isiwe tabu kabla sijafika nyumbani nikapitia.

Nilimkuta yuko good ila mwanaye alikua anaumwa sana ile mtoto kazidiwa na akaniambia ameshindwa kwenda hospitali hana hela na almost kila aliyempigia simu wamemuahidi tu tangu asubuhi na hakuna aliyemtumia mpaka muda huo sa 1 jioni inaelekea saa 2.

Kiukweli sikua na hela and i was totally broke, yaani wiki ile iliyoisha mwenyewe nimeishi tu kwasababu nina wazazi maana nilikua nina mambo mengi yananihitaji hela kiasi kwamba sikua nimebakiwa na hata Mia mbovu. Lakini nikasema kwenye suala la kuokoa maisha ya mtoto isiwe kesi nikamwambia ngoja nirudi kwanza nyumbani, nikamsimulia mama tukaongea na dada yangu wakasema tu hapa kwa harakaharaka hatuna namna tumdanganye tu mzee kitu chochote jioni hii atupe hela, kweli mzee bila hiyana tukamshawishi akanipa 150k nikamfata kwao tukaenda hospitali usiku uleule.

Mtoto akapewa huduma ya kwanza na baadhi ya vipimo wakamlaza ili asubuhi aendelee na matibabu mengine (muda wote huo anawapigia ndugu zake wakiwemo na baba wa mtoto hata simu hawampokelei wengine), asubuhi yake niliomba tu ruhusa kazini nikawaambia nitachelewa ili nione mtoto atakua anaendeleaje.

Case ya mtoto ikawa kubwa wakasema tuende nae hospitali nyingine kubwa (Peramiho nadhani watu wa songea wanaijua), kuna vipimo alivyoambiwa wampime vilikua vinahitaji hela almost kama laki 2 tena nikamwambia mama akanitumia tukafanikisha. Kwasababu kazini walikua wanapigapiga sana simu na nikaona wanaendelea vizuri na mama yake alikua ashafika nikamwambia naenda ofisini incase kimetokea chochote utatuambia nikampa na namba ya mama kama mimi nisipopokea ampigie, nikaondoka. The bad thing is nilikua busy busy sana hadi siku ikaisha sikuwatafuta tena.

Kinachoniumiza ni kwamba, jana mchana nilimpigia simu hakupokea nikaenda kwao sikukuta mtu, nikaenda hadi Peramiho tena kulivyo mbali nikaambiwa wameruhusiwa na hakunipa taarifa. Kuanzia jioni nimeingia WhatsApp naona ameweka status nyingi nyingi kufungua nikawa naona amescreenshot miamala yote ya watu waliokua wanamtuma hela na kuwapa credits Mungu awabariki sana kwa kuokoa maisha ya mwanae maana alikua kwenye hali mbaya sana na nini nini. Screenshot kama kumi hivi na kitu na amewataja na majina kabisa...

Cha ajabu hiyo miamala hakuna hata wa mtu mmoja uliofikia hata 30k, wote ni hizo hizo tu efu10 ef5 ef7, kawaandikia macaption mazito mazito. Nimebaki najiuliza mbona alikua ananiambia hawapokei simu, na hela inaonekana walimtumia siku ileile ambayo aliniambja na mimi niende kwake kumuona.

Mimi ambaye nilikua nae kuanzia siku ile hadi usiku nikaacha na kwenda kazini na tumeclear bills zote hata asante hajaniambia na wala taarifa kama wameruhusiwa hajanipa. Nimesubiri jana yote hadi leo saizi hajanipigia hata simu, Kina mama wananiuliza wanaendeaje nawaambia tu wanaendelea vizuri huku roho inauma.

Nimetenda wema nimeenda zangu wakuu, lakini bado roho inaniuma aisee😥😥
Watu wengi hawana shukrani na ni wanyenyekevu tu wakiwa na shida. Inaumiza mbaya aisee lakini wewe kausha na kuna siku atakuja kwenye 18 zako.
 
Duuh...! Nimeumia pia. Najua situation uliyopitia. Ndivyo MUNGU alivyopanga kwa tukio lako.

Fanya hivi nenda kamjulie khali na mwambie yote. Pia mwambie tu hajakufanyia sawa. Ukitoka hapo moyo wako utaachia. Pia naomba nieleweke maana ya kumwambia ni kuondoa mashtaka yako kwa MUNGU. Ksbb ukikaa kimya ukaendelea kuumia peke yako Kwanza utakuwa unaendelea kujiumiza hata wewe. Pili ukikaa kimya na ukasamehe bila kuongea nae wazi ni shtaka kubwa sana mbele za MUNGU.

Kwa hiyo nikuombe ukaongee nae. Ili pia uutengeneze moyo wako. MUNGU akupe wepesi.
 
Back
Top Bottom