Sijui kwanini nimeumia hivi

Sijui kwanini nimeumia hivi

Iliwahi kunitokea nashukuru nilisahau hata alivonitafuta miezi saba badae sikuwa na kinyongo naye


NB single mom hawasaidiwagi
 
Nahic hata hakukutaja kwenye screenshot hiyo ya miamala mwambie ahsante kama mtoto amepona tu bc sio rfk huyo endelea na yako
 
Pole sans mkuu, lakini jifunze siku nyingine mwanamke aliezaliswha na mtu usihangaike nae utapotea. Shukuru kaposti miamala, je angepost kaenda kwa jamaa na alisema hapokei simu kumpa hela ya matibabu ya mtoto ungejisikiaje japo sio mpenzi wako. Anyway huend anataka kuja kukupa SPECIAL THANKS kuwa mvumilivu ule tunda.
 
Kuna watu wana roho za tofauti sana na huyo shoga ako ana tabia za kiswahili. Ndio umeumia sana lakini overtime utakua sawa.

Cha kufanya delete namba yake akikutafuta muulize yeye nani. Mpotezee mazima hafai kabisa. Amekuona wewe ndio chuma ulete wake
Wewe utakuwa pacha wangu manake una roho mbaya kama mimi na akili kama zangu🤣🤣
 
Ubinadamu kazi my dear

And it's okay moyo kukuuma

Lakini usiruhusu kuumia sana

Take it easy, umefanya kwa nafasi yako kadri ulivoweza

Mengine mwachie yeye na Mungu wake watajuana wenyewe
 
Mpigie simu toa dukuduku lako au mtumie sms then kata mawasiliano nae, watu ni washenzi saana
 
Huyo atakuja tena mwenyewe shida haziishi na sikuzote jua mkataa pema pabaya panamwita huyo akirudi na shida usimuonee tena huruma mwache afe na matatizo yake kuna watu hawastahili huruma ni vile tu tunajipendekezaga
 
Siku zote ishi kwa kusaidia bila kutegemea malipo yeyote. Iwe ya shukrani ama chochote.

Kwa sababu hata shukrani isingekuongezea chochote.
Shukrani inafaida kubwa sana kwa pande zote mbili ndio maana kwenye dini pia kuna kutoa sadaka.

Kutokutoa shukrani kunaweza mfanya mtu asisaidie tena mtu yoyote kwa kujitoa kiasi hicho, shukrani ni lazima na muhimu sana.

Hizi stori za sijui tenda wema nenda zako ni kama zimepitwa na wakati, sahivi tenda wema alafu kaa angalia huo wema umeleta faida gani au umetapeliwa na wahuni. Muhimu kujua na kujifunza pia.
 
Habari za asubuhi wana JF,

Iko hivi, nina rafiki yangu ana mtoto (naweza nikasema ni single mom) ila isieleweke vibaya, nilisomaga nae O level huko ila nikama bahati tu tumejikuta tunaishi tena mtaa mmoja.

Ijumaa jioni wakati natoka tu ofisini alinipigia Simu akaniambia anashida kama naweza nipitie nyumbani kwao nikamuone, kwakua nilikua sina ratiba nyingine nikasema isiwe tabu kabla sijafika nyumbani nikapitia.

Nilimkuta yuko good ila mwanaye alikua anaumwa sana ile mtoto kazidiwa na akaniambia ameshindwa kwenda hospitali hana hela na almost kila aliyempigia simu wamemuahidi tu tangu asubuhi na hakuna aliyemtumia mpaka muda huo sa 1 jioni inaelekea saa 2.

Kiukweli sikua na hela and i was totally broke, yaani wiki ile iliyoisha mwenyewe nimeishi tu kwasababu nina wazazi maana nilikua nina mambo mengi yananihitaji hela kiasi kwamba sikua nimebakiwa na hata Mia mbovu. Lakini nikasema kwenye suala la kuokoa maisha ya mtoto isiwe kesi nikamwambia ngoja nirudi kwanza nyumbani, nikamsimulia mama tukaongea na dada yangu wakasema tu hapa kwa harakaharaka hatuna namna tumdanganye tu mzee kitu chochote jioni hii atupe hela, kweli tukamshawishi mzee bila hiyana akanipa 150k nikamfata kwao tukaenda hospitali usiku uleule.

Mtoto akapewa huduma ya kwanza na baadhi ya vipimo wakamlaza ili asubuhi aendelee na matibabu mengine (muda wote huo anawapigia ndugu zake wakiwemo na baba wa mtoto hata simu hawampokelei wengine), asubuhi yake niliomba ruhusa kazini nikawaambia nitachelewa ili nione mtoto atakua anaendeleaje.

Case ya mtoto ikawa kubwa wakasema tuende nae hospitali nyingine kubwa (Peramiho nadhani watu wa songea wanaijua), kuna vipimo alivyoambiwa wampime vilikua vinahitaji hela almost kama laki 2 tena nikamwambia mama akanitumia tukafanikisha. Kwasababu kazini walikua wanapigapiga sana simu na nikaona wanaendelea vizuri na mama yake alikua ashafika nikamwambia naenda ofisini incase kimetokea chochote utatuambia nikampa na namba ya mama kama mimi nisipopokea ampigie, nikaondoka. The bad thing is nilikua busy busy sana hadi siku ikaisha sikuwatafuta tena.

Kinachoniumiza ni kwamba, jana mchana nilimpigia simu hakupokea nikaenda kwao sikukuta mtu, nikaenda hadi Peramiho tena kulivyo mbali nikaambiwa wameruhusiwa na hakunipa taarifa. Jioni nimeingia WhatsApp naona ameweka status nyingi nyingi kufungua nikawa naona amescreenshot miamala yote ya watu waliokua wanamtumia hela na kuwapa credits Mungu awabariki sana kwa kuokoa maisha ya mwanae maana alikua kwenye hali mbaya sana na nini nini. Screenshot kama kumi na kitu hivi na amewataja na majina kabisa...

Cha ajabu hiyo miamala hakuna hata wa mtu mmoja uliofikia hata 30k, wote ni hizo hizo tu efu10 ef5 ef7, kawaandikia macaption mazito mazito. Nimebaki najiuliza mbona alikua ananiambia hawapokei simu, na hela inaonekana walimtumia siku ileile ambayo aliniambia na mimi niende kwake kumuona( Nilikua nasoma tarehe na muda wa zile transactions ).

Mimi ambaye nilikua nae kuanzia siku ile hadi usiku nikaacha na kwenda kazini na tumeclear bills zote hata asante hajaniambia na wala taarifa kama wameruhusiwa hajanipa. Nimesubiri jana yote hadi leo saizi hajanipigia hata simu, Kina mama wananiuliza wanaendeaje nawaambia tu wanaendelea vizuri huku roho inauma.

Nimetenda wema nimeenda zangu wakuu, lakini bado roho inaniuma aisee, sijui nifanye nini nikae sawa😥😥
shida ni kwamba ulikuwa unasaidia mtu ili upate credit/shukran. unaposaidia mtu, saidia kama kwa Mungu, usitegemee shukrani, akikushukuru umeshapata thawabu au kwa lugha nyingine shukran izo ziende kwa Mungu ili Mungu akubariki wewe, ukizipokea wewe basi umekwishapata thwawabu hivyo hutabarikiwa. wewe saidia, nenda zako, kama amekudanganya sawa asipokudanganya sawa, atajuana na Mungu huko huko na ni Mungu ndiye anatoa thawabu sirini.
 
tukiwaambia mtu anayebeba mimba akiwa bado hajaolewa ana kasoro zake muwe mnaelewa, nyie mnawaita single mother
amewafanyia dharau wazazi wake , ndugu zake wa tumbo moja. amekuja amevurugana na aliyemzalisha, wewe ndo atakupa heshima.
Pole sana
[emoji16]
 
Siku zote ishi kwa kusaidia bila kutegemea malipo yeyote. Iwe ya shukrani ama chochote.

Kwa sababu hata shukrani isingekuongezea chochote.
Huyu bidada siyo chuma au jiwe ni binadamu lazima atamani na yeye kutambuliwa mchango wake kwa vile msaidiwa kaamua kuwataja wahisani wake naye alipaswa kumtaja.
Tusiweke unafiki hata wewe na sisi tungeumia.
Huoni mfano mabango ya KWA HISANI YA WALIPA KODI WA MAREKANI au JAPAN?
 
Huyo mdada ulimsaidia hela ambayo ingetosha matibabu yote kwa hiyo kukuandika hapo status ingezua taharuki kwa wale wengine waliochanga pesa ndogo ndogo .HAPO HAJAKUWEKA WW ILI KUJILINDA YEYE SIO KWAMBA AMEKUDHARAU .ILA AMESHINDWA KUKUPA TAARIFA NA PIA HANA AKILI NZURI MANA ANGEWEZA HATA KUKUWEKA STATUS UONE PEKE YAKO MUAMALA ULIO MTUMIA.
 
Dada Leejay49 nimeyavaa maumivu yako yamenishinda na mimi nimejikuta naumia kama vile yamwnikuta mimi .
Watu wema ila watu wabaya , njia nzuri jitahidi kusahau hayo , futq namba ya huyo mchawi , anza maisha mapya bila kukumbuka uliwahi kujuana na Shetani wa aina hiyo
Usimpe tena hata chance ya kupiga story na wewe mfute maishani mwako huyo sio rafiki , sio ndugu , sio mtu mwema hata kidogo .
Wahenga walisema tenda mema nenda zako ila haikuwa utende wema uende kama hivi ulivyoondoshwa dada Leejay49 samehe ila usimsahau .
Pole sana , nasikitika na wewe na pia naumia na wewe , karibu Chabruma tupige story
 
Tenda wema uende zako na pia shida zina tabia ya kuwarudisha watu kwa watu waliowakosea. Aombe sana huyo dada asipate shida itakayohitaji msaada wako maana atashindwa kukurudia kwa kuona aibu.
 
Back
Top Bottom