Siku chache baada ya Trump kutishia kuongeza Tozo, Mexico na Canada wametii amri kudhibiti wahamiaji haramu

Siku chache baada ya Trump kutishia kuongeza Tozo, Mexico na Canada wametii amri kudhibiti wahamiaji haramu

G Tank

JF-Expert Member
Joined
Feb 9, 2023
Posts
2,297
Reaction score
8,760
Katika muhula wa Biden na Harris, wahamiaji haramu zaidi ya milioni 20 wameingia Marekani, wengi wakitumia mpaka wa Mexico na baadhi Canada, wahamiaji haramu wengi hasa wa wanaoingia kwa mpaka wa Mexico wakiwa ni wahalifu waliokimbia nchi zao ama wahanga wa kutumikishwa kihalifu kuanzia wauaji, wabakaji, punda wa kubeba madawa, watoto wanaovushwa kutumikishwa kingono (sex traffiking), n.k.

Rais wa Mexico na waziri mkuu wa Canada hawakufanya jitihada, waliichukulia poa sana serikali ya Biden / Harris

Ni jambo lililowakera sana Wamarekani na kupelekea wengi kumpigia kura Trump mwenye historia ya mafanikio makubwa ya kudhibiti wahamiaji haramu katika muhula wake wa 2016 - 2020.

Trump kachimba mkwara wa kuchapa ushuru wa 25%, matokeo yameonekana ndani ya siku chache sana

Tamko la Trump 25 - Novemba - 2024
1733071372083.png


Kama kila mtu anavyofahamu, wahamiaji haramu wengi wanamiminika kupitia Mexico na Canada, wakileta uhalifu na dawa za kulevya kwa viwango ambavyo havijawahi kuonekana hapo awali. Hivi sasa, msafara mkubwa kutoka Mexico, wenye maelfu ya watu, unaonekana kutoshikika katika jaribio lake la kuvuka mpaka wetu ulio wazi kwa sasa.

Kuanzia Januari 20, kama mojawapo ya Amri Zangu za Kwanza za Utendaji, nitasaini hati zote zinazohitajika kutoza ushuru wa asilimia 25 kwa BIDHAA ZOTE zinazoingia Marekani kutoka Mexico na Canada, pamoja na mipaka yao isiyo na udhibiti.

Ushuru huu utaendelea hadi pale Dawa za Kulevya, hususan Fentanyl, na Wahamiaji Haramu wote watakapoacha uvamizi huu wa Nchi Yetu! Mexico na Canada wanayo haki na uwezo kamili wa kutatua tatizo hili ambalo limechukua muda mrefu.

Tunadai rasmi kwamba watumie uwezo huu mara moja, na mpaka watakapofanya hivyo, ni wakati wa wao kulipa gharama kubwa sana!


28 - Novemba - 2024
1733071349373.png


Nimekuwa na mazungumzo mazuri sana na Rais wa Mexico, Claudia Sheinbaum Pardo.

Amekubali kusitisha uvukaji kupitia Mexico na kuingia Marekani (kinyemela), hatua inayofunga kabisa mpaka wetu wa Kusini.

Pia tumefanya mazungumzo kuhusu hatua za kusitisha wimbi kubwa la dawa za kulevya zinazoingia Marekani, pamoja na matumizi ya dawa hizi ndani ya Marekani. Mazungumzo haya yamekuwa yenye mafanikio makubwa!

30 - Novemba - 2024
1733071428392.png


Justin Trudeau, Waziri mkuu wa Canada kapanda Jet mpaka Marekani na kunyooka moja kwa moja Florida nyumbani kwa Trump kwajili la mazungumzo ya ana kwa ana
 
Trump kila anayeenda against naye tishio ni kuongeza tu ushuru,hivi bila kuuza Marekani uchumi wa nchi hauwezi kwenda?!

Latin Amerika, Afrika, Asia, Ulaya na Australlia huko hakuna masoko?!
 
Trump kila anayeenda against naye tishio ni kuongeza tu ushuru,hivi bila kuuza Marekani uchumi wa nchi hauwezi kwenda?!

Latin Amerika, Afrika, Asia, Ulaya na Australlia huko hakuna masoko?!
Marekani ndio soko la Dunia

CHINA na ujanja wake kwa TRUMP anakaa kisha CHINA anategemea soko la Marekani ,
URUSI ana natural resources nyingi otherwise angekuwa MCHINA 2

HAYA masoko uliyoyatata yananua kiasi kidogo na kwa bei ya chini
 
Trump kila anayeenda against naye tishio ni kuongeza tu ushuru,hivi bila kuuza Marekani uchumi wa nchi hauwezi kwenda?!

Latin Amerika, Afrika, Asia, Ulaya na Australlia huko hakuna masoko?!
viwanda vitahamia Marekani ili kukwepa rungu la ushuru
 
Inawezekana hujui maana ya neno "haramia" linavyotumika katika Kiswahili
 
Ni sahihi kabisa; piga ushuru wa kutosha ipatikane pesa ya kudili maharamia including kujenga jela za kutosha na kuyalisha huko.

Haifai chakula cha watoto kuwatupia mbwa. Wanaowazalisha wawahudumie vinginevyo wawadhibiti huko huko kwenye source.
 
Inawezekana hujui maana ya neno "haramia" linavyotumika katika Kiswahili
Naomba maelezo kidogo ya kina, ujazie nyama juu ya hoja yako ya neno "haramia" ili na sisi wengine tujifunze.
 
Marekani ndio soko la Dunia

CHINA na ujanja wake kwa TRUMP anakaa kisha CHINA anategemea soko la Marekani ,
URUSI ana natural resources nyingi otherwise angekuwa MCHINA 2

HAYA masoko uliyoyatata yananua kiasi kidogo na kwa bei ya chini
Wewe unaichuliaje China ?

Ni kama Tanzania?
 
Hakuna atakacho badilisha wahamiaji wataendelea kuingia marekani
 
Hakuna atakacho badilisha wahamiaji wataendelea kuingia marekani
fuatilia 2016 - 2020

Mexico walikubali kukamata maharamia wanaotumia ardhi yao kuvukia Marekani
 
Hahaaa sasa hivi rungu la US ni kuongeza ushuru tu
 
Marekani ndio soko la Dunia

CHINA na ujanja wake kwa TRUMP anakaa kisha CHINA anategemea soko la Marekani ,
URUSI ana natural resources nyingi otherwise angekuwa MCHINA 2

HAYA masoko uliyoyatata yananua kiasi kidogo na kwa bei ya chini
Pumba
 
Back
Top Bottom