kante mp2025
JF-Expert Member
- Nov 11, 2022
- 631
- 1,192
Mimi ni mgonga ulimbo mwenye matumaini tele wakati wagonga ulimbo wenzangu wakiwa addicted na porn na betting.
Basi mimi niko addicted na page & website za sekretarieti ya ajira maana nina imani nao sana tu baada ya mgonga ulimbo mwenzangu kutoka kule Inyalikungu kulamba shavu kwenye moja ya taasisi nono tu bila connection yeyote zaidi ya Mungu wa mbinguni sasa hivi anajilia marupu rupu kama mpumbavu pale maabara kuu ya taifa NIMR.
Nikiwa kama mmoja ya wagonga ulimbo baada ya kuona website inasoma 0 job vacancy kiukweli nikama nimepigwa msumali wa kichwa naamini mambo yatanoga tena ili niendelee kurusha nyavu labda zitanasa.
Wakuu wa sekretarieti ya ajira washawahi nibutua risasi ya kichwa kwenye written interview moja nikalamba 38 kama mpumbavu nililia kama kichanga sikuwakatia tamaa nikarudi tena kupambania moja ya nafasi zao nikafanikiwa kufika oral
Sasa lile neno la selected for oral linalipa matumaini sana ila kimbembe ni kuwa kila nikifungua pdf za placement najikuta sipo, Hapa namwomba Bwana Wa Majeshi na Mizimu ya Makumbusho Inifanyie Muujiza nami niwe miongoni mwa hawa wanaopata placement.
Natanguliza Shukrani, Kutokea Mpimbwe DC
Basi mimi niko addicted na page & website za sekretarieti ya ajira maana nina imani nao sana tu baada ya mgonga ulimbo mwenzangu kutoka kule Inyalikungu kulamba shavu kwenye moja ya taasisi nono tu bila connection yeyote zaidi ya Mungu wa mbinguni sasa hivi anajilia marupu rupu kama mpumbavu pale maabara kuu ya taifa NIMR.
Nikiwa kama mmoja ya wagonga ulimbo baada ya kuona website inasoma 0 job vacancy kiukweli nikama nimepigwa msumali wa kichwa naamini mambo yatanoga tena ili niendelee kurusha nyavu labda zitanasa.
Wakuu wa sekretarieti ya ajira washawahi nibutua risasi ya kichwa kwenye written interview moja nikalamba 38 kama mpumbavu nililia kama kichanga sikuwakatia tamaa nikarudi tena kupambania moja ya nafasi zao nikafanikiwa kufika oral
Sasa lile neno la selected for oral linalipa matumaini sana ila kimbembe ni kuwa kila nikifungua pdf za placement najikuta sipo, Hapa namwomba Bwana Wa Majeshi na Mizimu ya Makumbusho Inifanyie Muujiza nami niwe miongoni mwa hawa wanaopata placement.
Natanguliza Shukrani, Kutokea Mpimbwe DC