Siku nilipowashugulisha raia mtaani kwangu nilipokuwa mtoto

Siku nilipowashugulisha raia mtaani kwangu nilipokuwa mtoto

JEJUTz

Member
Joined
Aug 22, 2024
Posts
75
Reaction score
197
Hii siku haitokaa niisahau abadan!

Ilikuwa ni baada ya kushiba chakula changu cha mchana hapo home,huku nikifanya michezo ya hapa na pale.

Ghafla nikakutana na kiberiti cha gesi nikakifuata na kukichukua. Ile zima washa zima washa ikanivutia nikaamua kwenda nacho mtaani.

Kulikuwa na open space yenye nyasi ndefu kwenye eneo kubwa tu karibu na makazi ya watu, huku zikiwa zimekauka vizuri kwa jua kali.

Basi bhana nikajongea hapo na kiberiti changu cha gsi. Nikawa nawasha moto kisha nazima.Mara ghafla moto ukanizidi nguvu .

Nikaona isiwe taabu nikatimua mbio mpaka mtaa wa tatu huko.
Moto ukawa mkubwa vibaya mno, huku ukitishia usalama wa raia, mali pamoja makazi yao.

Hakika watu walipambana na kushughulika vya kutosha. Huku wasijue nani kasababisha janga lile. Bahati nzuri moto ulidhibitiwa na kuleta madhara kidogo tu.

Je! wewe ulifanya tukio gani ukiwa mtoto ambalo hutolisahau?
 
Nilikuwa mtaani kwetu ndiyo mkubwa kuliko watoto wote,ilikuwa kama kundi la watoto kumi, kila jmapili tulikuwa tunaambiwa tuende kanisani kusali misa ya jioni ya watoto, tulikuwa tukitoka tu nyumbani nakusanya sadaka zote, kipindi kile shilingi moja na sumuni zina thamani sana,hapo tutaenda kutembea na mimi ndiyo bosi nitawanunulia gubiti, bisi, kalanga n.k, tukimaliza,mda wa wenzetu kutoka kanisa na sisi tunaludi nyumbani,tukiulizwa mmesali tunasema ndiyo
 
Mie nilikuwa napita nyumba kwa nyumba nikiwa na pakti kubwa ya chumvi. OLE WAO nikute mboga jikoni. WANAJUTA SIKU HIYO
Siku moja nitakula kwa chumvi hadi Kisamfu cha kopo

USSR
 
Tukio nililofanya nikiwa Darasa la 4 limebaki historia mpaka leo. Nikipita mtaani wazee wananiambia we kijana ulitaka kulipua mtaa umeacha utundu.
 
Mim kipindi hicho nipo mdogo kuna dogo mmoja aliokota pesa nyingi inaweza fika kama millioni hivi akafukia pesa ndani ya pagara akaja kutuita tuende kufukia aisee pesa zilikuwa nyingi akawa anatugawia kila mmoja tulivyokuwa wajinga tukaanza kutangaza mtaa mzima mwishowe mwenye pesa akapatikana wakachukua pesa zote hili tukio nikikumbuka nacheka sana🤣🤣🤣🤣sijui inausiana na mada.
 
Tukio lengine tulikuwa tunajifanya mapolisi tunakamata waendesha matahiri pia tulikuwa tunatumia pagala kama sero hila utoto😂😂😂
 
Kuna mzee mmoja alikuwa anachunga mbuzi za wasomali, alikuwa anapendaga kukaa sehemu moja chini ya yale matanki ya maji machafu yaliyojengewa kwa sumeti, alikuwa na kichwa kama cha kipepe halafu hapa juu hana nywele yaani ana kipara
Siku hiyo nikamuona amekaa, nikabeba kokoto kubwa, nikatambaa mpaka nakiona kipara hiki hapa yaani niko juu yake, niliishusha ile kokoto kwa nguvu zote, mzee kustuka mimi mbio, si akaniungia kosa nililofanya na mimi nakimbilia nyumba, kufika nikapitiliza ndani na kwenda kujifungia chooni, wakabembeleza nifungue nimeuchuna sasa si unajua utoto nimeimisi michezo ya wenzangu inje nikatoka, wewe nilichezea kichapo na dingi sitokuja sahau
 
Me tukio ambalo sisahau kipind nkiwa mtoto nilikuwa nawapelekea sn moto kwenye ile michezo ya kimama na kibaba dah mungu anisamehe mana ss ivi n mtu mkubwa sn serikalini
 
Tukio ambalo sitolisahau ni mwaka 96 tunacheza maeneo ya karibu na home,nimeitwa nikalale siendi akatokea kichaa mmoja hv alikua anapiga sana watu,nilishtuka na nikashindwa hata kuinuka pale chini ni kama nilipooza ghafla na nikabaki namshangaa tu na aliishia kunitishia na akaondoka,
Asee niliogopa mno na nilienda kulala wakati huohuo
 
Enzi hizo nipo darasa la 5 huko kijijini.

Shuleni tulikuwa tunafuga ng'ombe,mbuzi na sungura. Sasa ikatokea mchungaji wa mbuzi na ng'ombe ameacha kazi. Ikapangwa ratiba ya mpito ya kuwapeleka wanyama malishoni hadi siku akipatikana mchungi mpya.

Katika ratiba nikajikuta nimechaguliwa siku ya jumatano kwenda kuchunga na wenzangu watatu,jumla tukawa wanne.

Sasa kwa sababu ya ujanja ujanja nikajikuta kwenye ile ratiba ya kuchunga mbuzi na ng'ombe naendelea tu,sibadilishwi. Kumbe behind the scene Mzee baba Nimeiba sufuria home,kiberiti,sukari na vikombe vinne Tena vile tulivyoambiwa vya wageni.

Tukifika machungani tunawakamua mbuzi wanaonyonyesha maziwa kisha tunachemsha kwenye vifaa vyangu milivyoiba home. Hapa wahuni wakashindwa kunitoa kwenye rotation ya kwenda malishoni,coz nilikuwa owner wa mazaga yote ya huko maChakani.

Tukafumania shamba la Mzee mmoja la ndizi zimekomaa sana,alooh!! Ukawa ni mwendo wa maziwa na ndizi full kufaidi.

Siku ya kufa nyani ikawadia,miti yote iliteleza.

Siku hiyo,nimetoka zangu home vizuri smart kabisa naenda shule kumbe kwenye mkoba Kuna nguo za kushindia home kama kawaida yangu. (kwenda nazo porini kuchunga). Nilikuwa sifiki shulen.Tunafika kwenye kituo tunaficha madaftari (mikoba) kwenye kichaka chetu maarufu,tunabadili nguo kisha tunamsubiri jamaa aliyeenda kuwafungulia wanyama shule kisha tuungane nae kuwapeleka huko mbali.

1.Siku hiyo moto wa kiangazi ukapita lile eneo la kichaka ukalamba madaftari,uniform na mikoba yote.

2. Narudi home jioni Huku naogopa coz Sina nguo za shule,zimeungua moto,naulizwa na Mzee "zimekuja taarifa za malalamiko hapa home kuwa una wiki mbili huendi shule,ukitoka hapa nyumbani unakwenda wapi na daftari ziko wapi,na mbona hauna nguo za shule?"

3. Kwenye like shamba la ndizi,yule Mzee alijuwa Mimi ndiye mkubwa wakikundi maana Kila alipoliona gang la wanaochunga,sura yangu ilikuwepo. akapeleka taarifa home kuwa Nina gang la kuiba mazao mashambani na tuna vifaa vyote vya kupikia huko,hivyo siendi shule ila naishia maporini kuchunga na kuiba.

4. Nikaulizwa kumbe humu ndani sufuria,vikombe na sukari vimepotea hadi tunasingizia majirani waliazima hawajarudisha kumbe wewe ndiyo umeiba? Aisee!!

5. Shuleni zikaja taarifa za kuwakamua maziwa mbuzi na kuwapitisha kwenye vichaka vya manyingu(dondora) ili wang'atwe. Ni kweli maana Kila siku mbuzi walikuwa wanarudi zizini wakiwa wamevimba balaa usawa wa tumbo. Ulikuwa mchezo wetu kuwapitiaha mbuzi wakorofi usawa wa viota vya manyingu ili wang'atwe maana walikuwa wanatukomoa kwenye kuwachunga. Wanazurura sana.

5. Shule nikapewa kesi ya Utoro uliokithiri na sifanyi homework. Kumbe hata daftari Sina wakati huo maana zimeshaungua moto.

Hiyo siku Nilipigwa kolabo ya kichapo ile siku kutoka kwa walimu na father hadi nilichakaa!!
 
Nakumbuka enz tunaenda bichi kidimbwi mto mbezi wa pale ubungo sasa ilikuwa kama mazoea kwenda kuogelea siku hiyo narudi nyumbani nimepauka na maji ya mtoni macho mekundu. Ishu ikawa naulizwa ulikuwa wapi mi kmya sisemi, wakaitwa wenzangu kuulizwa wakasema tulienda kuogelea siku hiyo nilichapwa na kupewa risala kwamba maji yanaua na kuna kichocho mtoni
 
Kuna siku moja kaka yangu alitengeneza manati, akamwambia dada yangu simama pale mbele ili nikilenge shabahaa kidole chako cha mkononi, naye akasimama akanyoosha mkono na kidole juu,bahati mbaya shabaha ilienda tofauti ikakutana na paji la uso,mziki wake sitakuja sahau
 
Kuna siku moja kaka yangu alitengeneza manati, akamwambia dada yangu simama pale mbele ili nikilenge shabahaa kidole chako cha mkononi, naye akasimama akanyoosha mkono na kidole juu,bahati mbaya shabaha ilienda tofauti ikakutana na paji la uso,mziki wake sitakuja sahau
Mbona hatari sana hii!!
 
Back
Top Bottom