Siku niliyotaka kuitiwa mwizi wakati nafanya mazoezi

Siku niliyotaka kuitiwa mwizi wakati nafanya mazoezi

Lycaon pictus

JF-Expert Member
Joined
Jan 31, 2021
Posts
9,189
Reaction score
16,128
Ni miaka mingi iliyopita wakati nachukua kozi ya unesi chuo cha Muhimbili. Hosteli zipo karibu na taasisi ya MoI. Sasa nyuma ya Hosteli kuna barabara ambayo nilikuwa naenda kukimbia muda wa jioni saa moja hivi. Na huko nyuma kuna sehemu watu wa MoI huweka mazaga yao kama vitanda vibovu nk.

Kumbe wezi kutoka Magomeni huwa wanavuka mto Msimbazi na kuruka ukuta wa Muhimbili kuja kuiba vitu hivyo. Hivyo MoI wakawa wanaweka walinzi hiyo sehemu.

Siku hiyo jioni saa moja nakimbia jogging, naenda na kurudi. Ghafla nashangaa walinzi wawili wananifukuza kwa kasi nyuma yangu kimyakimya. Ile kuwaona nikasimama kuwaangalia wanakimbilia nini. Nao wakasimama, nafikiri wanajiuliza mwizi gani anasimama kutusubiria. Wakaniuliza unaenda wapi, ndiyo kuwaambia napiga tizi ni mwanafunzi wa unesi. Ndiyo wakanisimulia wanavyoibiwaga.

Pengine nisingewaona ningekula mtama kutokea nyuma. Unawaletea mazeozi wabongo!!
 
Pana mtu alikua kawaida yake alfajiri anafanya mazoezi kabla ajaenda kazini,Pana siku yupo na bukta yake anakimbia kumbe mtaa huo huo alfajiri mida hio hio vibaka wamekurupushwa na wananchi jamaa aelewi hili anashangaa watu wanamuungia akasimama.

Kwenye mobb Huwa hakuna wa kukusikiliza watu Wana hasira ya mwizi.

Jamaa akaanza kushushiwa kipigo hadi akafa.
 
Muda mzuri wa mazoezi ni huo.... mm wakati mwingine napiga saa 10.30 alfajir lkn nakuwa full equipped gear zangu zote zipo full reflected na nina dimming running light yaani nakuwa na full tahadhari!
Iwe ndani. Nje ni hatari sana.
 
Hakikisha ukiwa unafanya mazoezi ya kukimbia barabaran hakikisha unapendeza yaani unavaa kama unatoka out truck kali , jezi kali soks na laba za kisasa ila ukivaa ovyo lazima watakuitia mwizi tu

Kwani kuna miaka wahuni walikuwa wanatuharibia wafanya mazoezi wa road work- yaani wanajifanya wafanya mazoezi Na wakiona mtu kazubaa na simu kituoni wanapita nayo
 
kila jambo na changamoto zake.

Nakumbuka kuna siku nafanya mazoezi asubuhi saa 11 nikakimbizwa na mbwa, utadhani walitumwa wanipime pumzi. Wale mbwa ni mbwa [emoji51][emoji51][emoji58] (nimewatusi kwa jina lao)

[emoji38][emoji38][emoji38]
Sasa ulkua unakimbia bila kukimbizwa, wakaamua kuku support, sasa ubaya uko wapi hapo[emoji23][emoji23]
 
Pana mtu alikua kawaida yake alfajiri anafanya mazoezi kabla ajaenda kazini,Pana siku yupo na bukta yake anakimbia kumbe mtaa huo huo alfajiri mida hio hio vibaka wamekurupushwa na wananchi jamaa aelewi hili anashangaa watu wanamuungia akasimama.

Kwenye mobb Huwa hakuna wa kukusikiliza watu Wana hasira ya mwizi.

Jamaa akaanza kushushiwa kipigo hadi akafa.
Ujinga wa mtanzania
 
Back
Top Bottom