GuDume
JF-Expert Member
- Jan 18, 2015
- 6,651
- 14,337
Wadau wakati najikumbusha kitabu flan cha shule ya msingi miaka yetu si tunasoma enzi za Mr na Mrs Daudi( nadhan kwa sasa watakuwa wamezeeka sana nasikia baraka yule mtoto wao mdogo ameoa miaka 5 iliyopita) nikakumbuka ile hadithi ya siku ya GULIO KATERERO. nami nikapata wazo moja mujarabu.
katika kudumisha urafiki na mahusiano naomba nilete wazo kuwa siku ya 7/7 kutakuwa na banda la nyama choma ambalo litakuwa maalum kuwakutanisha wana jamiiforums. ukiweza njoo kabisa na bandiko katika nguo yako la ID unayotumia ila kama hutotaka tukufaham haina shida.
lakini ningependa kabisa warembo, wanaume,wavulana,wanawake,wasichana na wamama wasikosekane. njoo wewe njoo na mwenzio nimeshapata banda tayari na fundi wa kuchoma nyama ya kuku,ng'ombe na mbuzi atakuwepo. siku hiyo usije na mtu ambaye hayumo jamiiforum...njoo wewe kama wewe tu rafiki utampata huko huko. najua kuna wale ambao wamewatenda vibaya wenzao humu ndani watakuwa na pingamizi sana. nawaomba wanawake muwasamehe wanaume waliowagonganisha na kuwa hit na kurun wa humu ndani.
siku hiyo itakuwa siku ya kujenga mahusiano mapya na pia kusambaza upendo kati yetu. njoo wewe njoo peke yako usihofu partner wa kucheza naye music atapatikana huko huko. ni kula nyama choma kwa ndizi na kushushia vileeee vinywaji vyetu. akina dada amarula zinauzwa kwa nusu bei na wine pia zitakuwepo kwa bei rahisi. hiyo ni siku maalum ya gulio. 7/7
WADAU WA MIKOANI TUTAONANA SIKU YA WAKULIMA 8/8 tutagawa Makundi..huko huko kwenye mabanda ya maonesho ya kilimo msisahau kuja mmevaa vibwaya. Mliokuwa tu mnatusikia na kutuona kwenye TV tutakuja mtuone LIVE . akina dada jiwekeni vizuri muwe katika nyakati zenu nzuri.msije mkaja kulalamika wanaume wa Dar wanadharau.
katika kudumisha urafiki na mahusiano naomba nilete wazo kuwa siku ya 7/7 kutakuwa na banda la nyama choma ambalo litakuwa maalum kuwakutanisha wana jamiiforums. ukiweza njoo kabisa na bandiko katika nguo yako la ID unayotumia ila kama hutotaka tukufaham haina shida.
lakini ningependa kabisa warembo, wanaume,wavulana,wanawake,wasichana na wamama wasikosekane. njoo wewe njoo na mwenzio nimeshapata banda tayari na fundi wa kuchoma nyama ya kuku,ng'ombe na mbuzi atakuwepo. siku hiyo usije na mtu ambaye hayumo jamiiforum...njoo wewe kama wewe tu rafiki utampata huko huko. najua kuna wale ambao wamewatenda vibaya wenzao humu ndani watakuwa na pingamizi sana. nawaomba wanawake muwasamehe wanaume waliowagonganisha na kuwa hit na kurun wa humu ndani.
siku hiyo itakuwa siku ya kujenga mahusiano mapya na pia kusambaza upendo kati yetu. njoo wewe njoo peke yako usihofu partner wa kucheza naye music atapatikana huko huko. ni kula nyama choma kwa ndizi na kushushia vileeee vinywaji vyetu. akina dada amarula zinauzwa kwa nusu bei na wine pia zitakuwepo kwa bei rahisi. hiyo ni siku maalum ya gulio. 7/7
WADAU WA MIKOANI TUTAONANA SIKU YA WAKULIMA 8/8 tutagawa Makundi..huko huko kwenye mabanda ya maonesho ya kilimo msisahau kuja mmevaa vibwaya. Mliokuwa tu mnatusikia na kutuona kwenye TV tutakuja mtuone LIVE . akina dada jiwekeni vizuri muwe katika nyakati zenu nzuri.msije mkaja kulalamika wanaume wa Dar wanadharau.