Siku ya kwanza baada ya kufungua kibanda umiza

Siku ya kwanza baada ya kufungua kibanda umiza

KUNA SEHEMU NILIKUTA VIJANA WA CHUO WAMENUNUA SMART TV KWAAJILI YA KUONESHA MPIRA KWENYE KIBANDA UMIZA.
ILI KUEPUKA GHARAMA ZA DSTV WAO WANACHOKIFANYA NI KUTAFUTA CHANEL INAYOONYESHA MPIRA MTANDAONI KUPITIA SIMU KISHA WANAWASHA BLUETOOTH YA SIMU NA TV HIVYO MPIRA UNAONEKANA VIZURI TU KWENYE TV.
HAPO HATA MVUA IKINYESHA ZILE KERO ZA DISH KUSCRATCH HAZIPO LABDA MTANDAO TU ULETE SHIDA.
Tatizo network huku mwisho kabisa 3G
 
Leo nimetoa ofa kama wadau mlivyonitonya ambapo kimsingi walikuja watu 21 nikatumia nafasi kuwaambia jmosi ni jero jero na saivi niko na wana hapa kama kumi tunacheki uefa free
Kaza buti mkuu siku zote uvumilivu Ni kitu mhim Sana,kwa hiyo wewe amini tu kadiri siku zinavyoenda na ndio mambo yatazidi kuwa mazuri na ujitahidi kuboresha mazingira...
 
Hauna mkono wa biashara, fanya kitu kingine, utashindwa! Biashara yaitaji mipango na uvumilivu, ni mapema sana!

Kama unataka biashara, tafuta namna nyingine ya kulipia hizo kwa miezi hata 3 then biashara itakaa sawa!

Biashara zote zinalipa, issue ni how long can you wait for that ili ikulipe? If u can wait utaifaidi.
Hauna mkono wa biashara!!!

Hili neno naomba ufafanyzi mkuu.
 
Komaa mwanzo mzuri kwa baadae weka na spika moja nje iwe inapiga sauti hua inaleta mzuka pia utaongeza na screen ukubwa angalau uwe na moja ya inch 49
 
Mleta mada umeanza vizuri biashara yako cha msingi ni kukomaa ili watu wapazoee mimi nilianza hii biashara mwaka 2013 maeneo ya Chanika pasipokuwa na umeme nilikuwa natumia Generator now mimi ndo top kama leo mechi ya Simba vs Kagera Sugar nimefunga na kiasi cha 48,000= bado Uefa cha msingi ni kukomaa
 
Hii kweli kule mbagara rang tatu kuna ukumbi unaitwa emirates ni wa kawaida tu lakini watu huenda pale kwa sababu ya ubishi kuna jamaa anaitwa Salum mshabiki wa Arsenal na Nando mahabiki wa Liverpool hawa watu mwenye ukumbi hawadai hela hasa huyo Salum maana ndo wanaleta amsha amsha sana wakiwepo hao ukumbi wote unakua kelele mwanzo mwisho....

Yule mmiliki wa huo ukumbi kwa sasa ana duka kubwa sana la jumla la kuuza bidhaa mbalimbali za vyakula na pia ana Costa kama sikosei 2 kwa biasharahiyo.
Watu wanapenda sana ukumbi uwe na amsha amsha pamoja na mashabiki wabishii
 
Mleta mada umeanza vizuri biashara yako cha msingi ni kukomaa ili watu wapazoee mimi nilianza hii biashara mwaka 2013 maeneo ya Chanika pasipokuwa na umeme nilikuwa natumia Generator now mimi ndo top kama leo mechi ya Simba vs Kagera Sugar nimefunga na kiasi cha 48,000= bado Uefa cha msingi ni kukomaa
Nataka nitumie jmos kama kipimo hio game y watani wa jadi
 
Unapanda mbegu Leo unataka uvune kesho?!! Biashara inaanza kupimwa ndani ya miezi 3 na kuendelea.

Biashara isiyo na hasara ni UTAPELI pekee
 
Shida ni kwamba sisi wa afrika tunaanzisha biashara na mtaji kiduchu sana,ndo maana tunakuwa tunafeli mapema sana,tujifunze kwa wenzetu wa asia ambao wao wameonyesha mafanikio makubwa ktk ujasiriamali,kwa kipindi hiki kifupi ulichoanzisha biashara hukupaswa kufikiria mambo ya vifurushi n.k ..usikute na kula napo unategemea hapohapo ..biashara ni kama mtoto unapaswa uilee hata kwa mwaka ndo ufunge mahesabu,la sivyo itakupa sana mawazo,itakuendesha badala ya wewe kuiendesha yenyewe
 
Back
Top Bottom