Siku ya kwanza kuingia shule ya bweni ya Serikali

Hahahh mate umenikumbusha mbali sana
Baada ya kutoka shule za private kuingia shule za serikali First day was a nightmare
Kuoga ndio ulikuwa mtihani mkubwa kwani watu walikuwa wanajimwaga kama walivyozaliwa kwa kadamnasi hahahhh huu mtihani ulikuwa mgumu kuukamilisha. Tuje kwenye mlo kuanzia breakfast mpaka supper hili lilikuwa zoezi gumu sana maharage daily samaki sato once a week (harufu ya hapo anajua Mungu) chai na mkate nusu una wadudu sijui nyenyele wale ilikuwa balaa (thank God ule uji wa kuongezea chumvi ili sukari ikolee haukuwepo pande hii) Sasa tuje kwa ubwabwa na nyama ya ling'ombe hahahh pilipili hoho tu ndio zilikuwa zinachangamsha mlo.
After few months tukazoea na kuwa hodari wa kununua mihogo na kuunga maharage tena (kujipikilisha)
*** All in all tulijifunza mengi
*** miss maisha ya shule
 
Unazungumzia milambo secondary?
 
Usisahau wizi wa pichu, yaani ukiifua unaanika chini ya godoro ukiiacha wazi ukiondoka wanabeba. Hasa pichu za Ulaya, mate yamepita yale maisha.
 
Aisee..1992?

Shikamoo Baba mdogo
Marahaba yna2 mbona hivyo unataka kuninyima nini tena? 1992 si juzi tu miaka 26 iliyopita na kama unavyojua vijijini tulipokulia unaanza la kwanza na miaka 10-12 form i unaanza na miaka 17-20 kwahiyo im bout to turn 47,bado hata sijafikisha umri wa kustaafu......Damu bado inachemka nimemzidi MO miaka mitatu tu ila yeye kanizidi MABILIONI ya hela....😀😀😀😀
 
Nilifika shule usiku sana bweni lina harufu kali sijapata kuisikia vile kuna mwalimu alinipokea akaniambia asubuhi tu niende ofisini kufanya usajili.

Asubuhi mapema nikawahi ofisin kwenda kufanya usahili bwenini nikawaacha madogo kadhaa wa o level wanajiandaa kwenda madarasani.

Ofisini ile kulipa ada zao na kukamilisha usahili wakague vyeti na kukutana na wagen wengine wapya hapa na pale nikamaliza kila kitu saa nne.

Kurudi bwenini washavunja kufuli saa nyingi Dawa kubwa zile za mswaki, makatoni ya sabuni za kuogea na za unga, mafuta ya kupaka, kalamu na mazaga yote wale washamba wameiba wameniacha na counter book, nguo taulo na vitabu vichache

Roho iliniuma sana vile uzoefu wa maisha ya boarding nayajua nikahisi ni uzembe wangu jambo moja wahuni walikosa hela sikuweka kwenye sanduku la chuma.

Baada ya tukio sikureport popote nilienda kununua dawa ndogo ya mswaki, mswaki mmoja na sabuni ndogo ya kuoegea

vitu vingine vyote nikaanza kuiba kimya kimya niliiba bila huruma nilikua naiba ile mbaya mwaka mzima wezi wanatajwa hakuna anayenihisi vunja vunja makufuli wako darasani naiba vingine hata sina shida navyo natupa chooni iba iba mbaya sana.

Uchaguzi TYCS nachaguliwa kua katibu mkuu hakuna anayewaza mwizi ni mimi bwenini nakemea uwizi asubuhi jion na vunja.

Baadaye nikaamua kuacha mwenyewe. Nilisimulia marafiki kadhaa baada ya kumaliza shule miaka mingi ilivyopita. Mama alisema niwaombe msamaha. Sikuwahi kufanya hivyo.
 
Nakumbuka naingia seminary siku ya kwanza nafika tu nimepokelewa mida ya mchana napokelewa na 'angelus' (malaika wa bwana) nikashangaa sana. Nifika jumamosi siku ya kazi nikapangiwa kwenda kufagia mabanda ya nguruwe asee unakutana na nguruwe ana jino kubwa kama ngiri alafu ana watoto ukisogea uzoe kinyesi linakoroma mpaka mkojo unatoka.

Hapo jamaa wazoefu wanakuambia fanya fasta kuna masifu saa 12:30 jioni. Yani nimetoka kwenye mabanda ya noah nanuka kama jalala la Tandale.

Kwenda kuoga kabla sijamaliza mara kengele imelia watu kurupushani kuwahi chapel kwenye masifu. Tuliochelewa pale tukaandikwa majina kesho yake adhabu ya kuhamisha mbolea ya ng'ombe kupeleka bustanini. Baada ya masifu kengele ikagongwa hao tukatimba messini kula msosi.

Hapo kwenye msosi ndio raha unakuta nyali imepikwa fresh nyama zakutosha alafu self service na matunda yapo.

Usiku kabla ya kulala nikasikia tena kengele nikaambiwa saizi ni compreto hata sielewi ni nini wakati huo. Asubuhi saa kumi na dakika 45 tayari tushaamka tushaoga kanisani na huko ndio kuna zamu za kuandaa ibada kila siku na kutumikia pamoja na kuongoza masifu na nyimbo. Asee mpaka nimekuja kuiva nilipata tabu sana ila nikaja kuwa mcharo alafu nikachaguliwa kuwa messi officer basi ikawa raha sana mimi na masela tunafaidi mambo ya store; nyama, maziwa, samaki, matunda, sukari, mikate kwa sana..

Ila life la seminary gumu sana ila tamu kama una wito. Nilikua nabubujika wito enzi hizo hadi nikirudi likizo mtaani wananiita 'paroko' (mpaka saaa hili jina lipo). Wito ulikuja kukata niliporudi likizo moja chaliangu mmoja nimesoma msingi nikaenda kufika nikakuta wazazi hawapo hapo ndani kuna machalii wahuni kibao ni moshi wa ganja nyumba nzima kama hujawahi kabisa kunusa hata moshi lazima uzimie. Nikalipua na mimi race bese ndio mwanzo wa wito kufa hapo.

Natamani maisha yale ya seminary yajirudie japo yalikua magumu ila mtu unajifunza discipline kwenye maisha.
 
Usingeona comment yake ungeomba wap hela mbona mnapenda kuonyesha njaa zenu mapema sana
Usingeona comment yangu ungeongea nini mbona mnapenda kuonyesha viranga vyenu mapema sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…