Siku ya kwanza kuingia shule ya bweni ya Serikali

[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]Aisee itakuwa alikuwa anawaadithia baadhi ya marafiki zakee na kama ulikuwa unamsukumia motoo wenyewee ndo balaa...

Alivyoondoka ndo watu walijua hiko kisa 🤣 Wakati yupo watu walikuwa wanatuona kama washkaji tu.
 
Alivyoondoka ndo watu walijua hiko kisa [emoji1787] Wakati yupo watu walikuwa wanatuona kama washkaji tu.
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]Mtafute mzee baba mkumbushiee...
 
Nilireport form 5 shule ya gov. Kwa mara ya kwanza. Njiani nilikua nina mawazo sana sijazoea maisjha ya kubanwa banwa. Uzuri ni kuwa shule ilikua free sana yan...

Sasa siku ya kwanza nimefika nikapokelewa na mtu simkumbakag had leo wakanisaidia trunk mpaka dorm la form 5... kimbembe ni usiku mpaka inafika saa 6 sion mtu anaekuja kulala mpaka nikauliza kwa mwana mmoja pemben kwamba wengi bado hawajareport? Akaniambia wako madarasani wanapiga msuli. Nilichokaaaaa. Na hata kuingia class ilikua bado yan
 
Watu walikuwa wanadate mapadre.kuna mmoja ni mbunge siku hizi alipata mimba .akaenda kuzaa akaenda Shule ingine.
 
Hahaahahaahahaaaah
 
Hahahahahahah
 
Kibahaa ninii..[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Form one nimeingia nikaambiwa baada ya prepo saa nne nitasikia kengele niende assemble nikachukue machungwa [emoji16]
Nilienda nikajiona alone

Enzi hizo form five tunawaita chuwa

Unakaa ghorofani unampiga mtu water splash anaepita chini sometimes ya maji ya moto au mawe ila kama mbabe akigundua room anakuja kumwaga maji ya bafuni room nzima
 
Nimeenda form five first day naamka naona mtu anafungua locker lake ananipa maji nikapigie mswaki
Nikamuuliza yanapatikana wapi akaniambia pale dukani wanauza [emoji1373] means maji ya kupigia mswaki inabidi ununue au uchukue chai nyingi asubuhi usubiri ipoe upigie mswaki


Kuoga ilikuwa hadi weekend niende mjini niakaoge au unaoga by cooling system( ukishakula jioni unavua shati unabaki na boxer unapunga upepo kama nusu saa) then unaingia prepo
 
mh! mimi nililipoti baada ya siku kama tatu hivi likaibuka timbwili la kudai wali baada ya vijana kuchoshwa na ugali wengu, timbwili likiongozwa na makamanda wa form2, hasira zikichochewa zaidi baada ya timu ya mpira wa miguu ya shule niliyolipoti kutandikwa bao moja kwa sifuri na timu ya shule jirani na mkuu wa shule asubuhi alitutabilia kufungwa siku hiyo.

Form5 wengi tukiwa ni wagen madogo hawana huruma kwa mtu anaekaa nyumanyuma waliamuru form5 tuwe mstali wa mbele kuelekea kwa mkuu wa shule wao wako nyuma wakiimba kwa hasira TUNATAKA WALI TUNATAKA WALI.

Nyumba ya mkuu wa shule ilibomolewa vibaya na tayali ilikua usiku, mkuu alipona hali mbaya akatoa taarifa polisi ffu wakaja aisee kichopo kikaanza. form 2, 3, na six walikua wenyeji wanajua kila kona shida ikawa kwa form 1 na sisi form 5 hatujui tukimbilie wapi, ktk kimbiakimbia usiku ule baazi ya vijana walijikuta kwenye bonde ambalo juu kuna majani na matete mengi ila chini ni kina kirefu cha maji na ile giza ilikua ngum kujua dimbwi limeanzia wapi na linaishia wapi, hapo vijana kazaa wa form1 walipoteza maisha (RIP)
Baada ya usiku huo wa kadhia timbwili lilirudiwa tena asubuhi baada ya wanafunzi kujua kuwa kuna wenzetu waliopoteza maisha huko dimbwini hapo sasa ffu waliomba poo viongoz wa mkoa walikuja shule baada ya hali kua mbaya shule ilifungwa kwa muda usio julikana.
 
Duuh walifariki wangapi???
 
Dining siku ya kwanza mdada mmoja akimwaga magarage kisa alimkuta mende ndani ya bakuli. Kwakuwa bado tulikuwa na makula kula kuna waliomtengenezea orange squash na marie biscuits.

Baada ya miezi miwili pale shule, mdada alikuwa hodari wa kutoa mende kwa kijiko na kuendelea na menu.[/QUOTE]



Siku ya kwanza kuripoti boarding school ,kwakua nilifika usiku kesho yake alhamisi mchana, ilikuwa ni Siku ya wali .Ajabu nilikula kidogo nikaumwaga ule wali kutokana na kuzoea chakula cha nyumbani. Usiku nikakutana na viazi na maharage ,kwakuwa nilikuwa mtoto wa mama machozi yalinilenga kutokana na kukutana na maisha ambayo sikuwai kuishi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…