[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]Aisee itakuwa alikuwa anawaadithia baadhi ya marafiki zakee na kama ulikuwa unamsukumia motoo wenyewee ndo balaa...
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]Mtafute mzee baba mkumbushiee...Alivyoondoka ndo watu walijua hiko kisa [emoji1787] Wakati yupo watu walikuwa wanatuona kama washkaji tu.
[emoji2] [emoji2] [emoji2] pole sana sumbai jamani.
Wewe siku ya kwanza ulivyo riport hukukutaana na changamoto?[emoji2] [emoji2] [emoji2] pole sana sumbai jamani.
Missed you too!
Zilikuwepo ila si kubwa kivile,hlf shule ilikuwa ndio inaanza kwhy hakukuwa na wababe wengi.Wewe siku ya kwanza ulivyo riport hukukutaana na changamoto?
Nakumbuka shule yetu ilikuwa na wanafunzi wengi walikuwa ni kutoka Kigoma,Tabora na Mwanza...washamba balaa...umeme ukikatika tunawapa ndoo wakachote umeme...yaani hata watu wazima walikuwa wanabeba ndoo kwenda kuchota umeme.....na tulikuwa tunawaambia wasiporudi na umeme wabaki huko huko....walipata taabu sana
Hahahahahahah[emoji23] [emoji23] [emoji23] Nicheke kwanza kidogo.
Nilifika shule wenzangu wakiwa wameanza masomo, siku moja akaniita dada mmoja anaitwa Nuru alikuwa kidato cha 3 akaniuliza mbona wewe sijawahi kukuona hapa shuleni umetoka wapi? Nikamwambia nimetokea sehemu fulani akauliza wote mmetahiriwa au mna magovi. Nilikuwa na rafiki yangu mmoja anaitwa Thobias.
Nikamwangalia yule jamaa yangu maana alikuwa ni lile kabila lenye kukwepa tohara, nikasema ndiyo wote tumetahiriwa. Akauliza tena wote mmetahiriwa? Nikanyamaza.
Akaitwa jamaa mmoja mbambe aje kufanya uhakiki mbele ya yule dada (Nuru) ambaye nae alikuwa na mwenzake wa kike. Yule njema akafika na kumkamata Thobias na kuanza uhakiki jamaa kakutwa ana mkono wa sweta. Duh zamu yangu kufika nikalala mbele kwa mbio za Bolt sitaki ukaguzi kwenye dushe langu mbele ya KE.
Baada ya hapo nikaitwa timu ya shule kidogo nikapata ahuweni yale mateso niliyakwepa kwa mwamvuli wa soka.
Hahahahahahah!!!Kunaa Jamaa alikamatwa kijijini na ticha kuulizwa jina aksema anaitwa Bitozi Nyangema jumaatatu ticha Anaita assemble Bitozi Nyangema atoke mbele watu [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Okay. MkuuuZilikuwepo ila si kubwa kivile,hlf shule ilikuwa ndio inaanza kwhy hakukuwa na wababe wengi.
Zilikuwepo tu ishu za kuibiana nguo, mashuka, viti n.k
Kibahaa ninii..[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]Nilireport form 5 shule ya gov. Kwa mara ya kwanza. Njiani nilikua nina mawazo sana sijazoea maisjha ya kubanwa banwa. Uzuri ni kuwa shule ilikua free sana yan...
Sasa siku ya kwanza nimefika nikapokelewa na mtu simkumbakag had leo wakanisaidia trunk mpaka dorm la form 5... kimbembe ni usiku mpaka inafika saa 6 sion mtu anaekuja kulala mpaka nikauliza kwa mwana mmoja pemben kwamba wengi bado hawajareport? Akaniambia wako madarasani wanapiga msuli. Nilichokaaaaa. Na hata kuingia class ilikua bado yan
Duuh walifariki wangapi???mh! mimi nililipoti baada ya siku kama tatu hivi likaibuka timbwili la kudai wali baada ya vijana kuchoshwa na ugali wengu, timbwili likiongozwa na makamanda wa form2, hasira zikichochewa zaidi baada ya timu ya mpira wa miguu ya shule niliyolipoti kutandikwa bao moja kwa sifuri na timu ya shule jirani na mkuu wa shule asubuhi alitutabilia kufungwa siku hiyo.
Form5 wengi tukiwa ni wagen madogo hawana huruma kwa mtu anaekaa nyumanyuma waliamuru form5 tuwe mstali wa mbele kuelekea kwa mkuu wa shule wao wako nyuma wakiimba kwa hasira TUNATAKA WALI TUNATAKA WALI.
Nyumba ya mkuu wa shule ilibomolewa vibaya na tayali ilikua usiku, mkuu alipona hali mbaya akatoa taarifa polisi ffu wakaja aisee kichopo kikaanza. form 2, 3, na six walikua wenyeji wanajua kila kona shida ikawa kwa form 1 na sisi form 5 hatujui tukimbilie wapi, ktk kimbiakimbia usiku ule baazi ya vijana walijikuta kwenye bonde ambalo juu kuna majani na matete mengi ila chini ni kina kirefu cha maji na ile giza ilikua ngum kujua dimbwi limeanzia wapi na linaishia wapi, hapo vijana kazaa wa form1 walipoteza maisha (RIP)
Baada ya usiku huo wa kadhia timbwili lilirudiwa tena asubuhi baada ya wanafunzi kujua kuwa kuna wenzetu waliopoteza maisha huko dimbwini hapo sasa ffu waliomba poo viongoz wa mkoa walikuja shule baada ya hali kua mbaya shule ilifungwa kwa muda usio julikana.
watatu mkuuDuuh walifariki wangapi???