mh! mimi nililipoti baada ya siku kama tatu hivi likaibuka timbwili la kudai wali baada ya vijana kuchoshwa na ugali wengu, timbwili likiongozwa na makamanda wa form2, hasira zikichochewa zaidi baada ya timu ya mpira wa miguu ya shule niliyolipoti kutandikwa bao moja kwa sifuri na timu ya shule jirani na mkuu wa shule asubuhi alitutabilia kufungwa siku hiyo.
Form5 wengi tukiwa ni wagen madogo hawana huruma kwa mtu anaekaa nyumanyuma waliamuru form5 tuwe mstali wa mbele kuelekea kwa mkuu wa shule wao wako nyuma wakiimba kwa hasira TUNATAKA WALI TUNATAKA WALI.
Nyumba ya mkuu wa shule ilibomolewa vibaya na tayali ilikua usiku, mkuu alipona hali mbaya akatoa taarifa polisi ffu wakaja aisee kichopo kikaanza. form 2, 3, na six walikua wenyeji wanajua kila kona shida ikawa kwa form 1 na sisi form 5 hatujui tukimbilie wapi, ktk kimbiakimbia usiku ule baazi ya vijana walijikuta kwenye bonde ambalo juu kuna majani na matete mengi ila chini ni kina kirefu cha maji na ile giza ilikua ngum kujua dimbwi limeanzia wapi na linaishia wapi, hapo vijana kazaa wa form1 walipoteza maisha (RIP)
Baada ya usiku huo wa kadhia timbwili lilirudiwa tena asubuhi baada ya wanafunzi kujua kuwa kuna wenzetu waliopoteza maisha huko dimbwini hapo sasa ffu waliomba poo viongoz wa mkoa walikuja shule baada ya hali kua mbaya shule ilifungwa kwa muda usio julikana.