Haha mbona walijua kumuonea mume wangu jamani mweeh. Naona akajifunza na "ujambawazi" kabisa, bora na yeye aibe
Yani nimewaza what if wanangu wakarithi roho mbaya from both parents, nimeishia kukemeaYaani nimecheka eti akawa anaiba hadi vile asivyo na kazi navyo anatupa, namuingiza rasmi kwa kamati ya roho mbaya.
Hahahahahahhaahaah nimecheka SanaNilifika shule usiku sana bweni lina harufu kali sijapata kuisikia vile kuna mwalimu alinipokea akaniambia asubuhi tu niende ofisini kufanya usajili.
Asubuhi mapema nikawahi ofisin kwenda kufanya usahili bwenini nikawaacha madogo kadhaa wa o level wanajiandaa kwenda madarasani.
Ofisini ile kulipa ada zao na kukamilisha usahili wakague vyeti na kukutana na wagen wengine wapya hapa na pale nikamaliza kila kitu saa nne.
Kurudi bwenini washavunja kufuli saa nyingi Dawa kubwa zile za mswaki, makatoni ya sabuni za kuogea na za unga, mafuta ya kupaka, kalamu na mazaga yote wale washamba wameiba wameniacha na counter book, nguo taulo na vitabu vichache
Roho iliniuma sana vile uzoefu wa maisha ya boarding nayajua nikahisi ni uzembe wangu jambo moja wahuni walikosa hela sikuweka kwenye sanduku la chuma.
Baada ya tukio sikureport popote nilienda kununua dawa ndogo ya mswaki, mswaki mmoja na sabuni ndogo ya kuoegea
vitu vingine vyote nikaanza kuiba kimya kimya niliiba bila huruma nilikua naiba ile mbaya mwaka mzima wezi wanatajwa hakuna anayenihisi vunja vunja makufuli wako darasani naiba vingine hata sina shida navyo natupa chooni iba iba mbaya sana.
Uchaguzi TYCS nachaguliwa kua katibu mkuu hakuna anayewaza mwizi ni mimi bwenini nakemea uwizi asubuhi jion na vunja.
Baadaye nikaamua kuacha mwenyewe. Nilisimulia marafiki kadhaa baada ya kumaliza shule miaka mingi ilivyopita. Mama alisema niwaombe msamaha. Sikuwahi kufanya hivyo.
Kwakweli tukemee kwa pamoja.Yani nimewaza what if wanangu wakarithi roho mbaya from both parents, nimeishia kukemea
Wakauchote wapi [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]Nakumbuka shule yetu ilikuwa na wanafunzi wengi walikuwa ni kutoka Kigoma,Tabora na Mwanza...washamba balaa...umeme ukikatika tunawapa ndoo wakachote umeme...yaani hata watu wazima walikuwa wanabeba ndoo kwenda kuchota umeme.....na tulikuwa tunawaambia wasiporudi na umeme wabaki huko huko....walipata taabu sana
Umenikumbusha kitu wallah ,unaenda zako na kanga na toilet paper,ukishatoka ndio unaenda kuvaa nguo la sivyo unanuka choo nguo zote,, hivi kwanini jamani vyoo vile vilikuwa na niniAlirudi kesho yake akafikia ofsini kwa walimu ndio wakamleta mabwenini... Shule za wavulana zina vituko sana..
Yani ilikua ukiingia chooni lazma uingie na chupi au uchi na ukitoka unakaa chini ya mti kama dakika tano la sivyo ukiingia na nguo harufu ya choo utaibeba nusu saa....
Wewe Martial hater kumbe umesoma kiliboys mkuu pale...Ile Kilamanjato Boys noma sana wenyewe tuliita "Kiliboys" hapa nakumbuka:-
1. Dogo mmoja form one ilikuwa siku ya ijumaa mchana ni makande hapa kunakuwa na vurugu sana bwaloni, yule dogo kawahi kajaza sahani akala kiasi kilichobaki akafungia kwenye mzinga(sanduku la chuma) ili jioni aendelee na makande yake asipange foleni ya ugali, wahuni wakamtaim ametoa wakageuza sanduku lile chini juu na kulitikisa sana kisha wakalirudisha kama lilivyokuwa. Pata picha alivyokuja kufungua sanduku baadae, ikumbukwe sanduku hili ndio lina kila kitu kuanzia uniform na vitu vingine.
2. Uzuri wa hii shule hakuna kukacha prepo ukajificha bwenini, mabweni yalikuwa na vibwengo sana hasa hasa bweni la horombo.
3. Shule ilikuwa mbali sana na wilayani, haina fensi huwezi hata kutoroka ni pori tupu na kuna tembo porini kutokea Kenya.
SIKU HIZI NASIKIA IMEPOA IMEKUWA SHULE YA WANAWAKE.
AsanteeMimi nimesoma bagamoyo secondary, shule pekee ukiwa ufukwen au baharin unaogelea unakua bado upo eneo la shule, kama advance hukusoma serikalin bas ww ni kilaza
Nipo tamisemi Dodoma, na ww wa shule binafsi unaendeleaje na private sector hapoAsantee
Haya wewe uliyesoma serikalini advance vp uko wizara gani sasa hv mkuu
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Khe khe [emoji1787] khe [emoji1787] khe [emoji1787] khe khe [emoji1787] khe [emoji1787] khe [emoji1787]Ilikuwa form V, baada ya orientation, tunes za kujuana. Wengi tulishapewa majina ya rafiki wa rafiki ambae anakuja shule ile.
Dining siku ya kwanza mdada mmoja alimwaga magarage kisa alimkuta mende ndani ya bakuli. Kwakuwa bado tulikuwa na makula kula kuna waliomtengenezea orange squash na marie biscuits.
Baada ya miezi miwili pale shule, mdada alikuwa hodari wa kutoa mende kwa kijiko na kuendelea na menu.
Pole sana mkuuSiku ya kwanza nilianza kula menu ya jioni ilikuwa ugali
Ugali ulikuwa wa unga uliokaa kwa muda mrefu hadi ukavundika ukawa na harufu fulani amaizing.
Nilikula matonge hayazidi matano nikaacha nikaenda kuumwaga, kesho yake njaa ililikamata maana sikula vizuri jana yake.
Ilipofika lunch ile harufi sikuiona tena(sikuijali) niliparamia menu bila kubakisha hata punje ya tonge. Kuanzia hapo nikazoea ugali moja kwa moja
Watu tulianzia kwenye shida za menu kabla ya kuanza na hayo ma quantumPole sana mkuu
Mi mzee wangu alikua ananipenda sana ... !!!
Shida nilizopitia ni yale ma quantum phyz
Aisee pole sanaForm 5 nilipangiwa na shosti angu tena comb moja..... Tukaenda wote tumevuuta hatari tumefika shule tunajikuta masista duu wajanja ndo sis asubuhi tunashangaa kuamka saa kumi na moja asubuhi hapo unapangiwa kufagia uwanja mkubwaa,afu umwagilie garden mpaka iwe tifu tifu baada ya hapo ukadeki choo afu saa moja sharp uwe parade ....aisee ikabid niulize hiz Kazi mpaka lini nikajibiwa ndo maisha ya kila siku niliangua kilio kisicho na mfano siku ya kwanza nikasema haya maisha siwez ,
Mda wa parade nipo na shati la tomato kidogo dogo na sketi ya kisista duu ya kiunoni nilikua nmeshashona home mwee mweee mwalimu kupita akatutoa mbele kwamba m shoga angu tumevaa kihuni tukapelekwa kwa Fundi wa shule tukashonewa mpaka shati kubwa kama la baba paroko kitamba kama cha shuka daa huku sket ya tumboni ndefu hatari
Nilienda na kikombe cha udongo kidogo dogo cheupe kama cha kahawa vile na kisahani changu kidogo kama kisosi maana o'level shule niliotoka full ubishoo ,doooh kufika SAA nne uji madai hatunywi tumbo litakua kubwa afu nashangaa watu wana majagi hahahaha..... Mwezi mrefu nikatafuta jagi langu na bakuli kubwa tu tena la plastic uji nikaunywa vizuri tuuuu na foleni ya ugali nikapanga
Shule ilikuwa kanda ya ziwa washamba washamba wengi tukaanza kuwacheka wahaya kwamba mjini wanajishauaga saana ila kumbe wana lafudhi mbovu inshort ni wakuja tuu tuliwacheka saana....
Nakumbuka siku ya kwanza tu nilipiga simu nyumban maisha magum siwez mzee akanimbia vumilia mpaka muhula uishe ndo utahama ,sasa muhula daah Kazi nying afu viongoz walikua wanaishi kwa raha saana hawafanyi kazi yeyote nikaona bora nikimbilie uongoz bahati mbaya viongoz wote form6 na uchaguz mpaka muhula wa pili ,siku ya kufunga niliondoka na kila kitu changu kufika nyumban shule nilizotaka kuhamia background ya result zao kwa comb yangu sio nzur tena wasichana ndo kabisa div3 , div4 na 0 maana nilikua pcm nikasema hapana bora nilipotoka comb yangu wanafaulu nikarudi baada ya miez miwili na tranka langu hahahaha nikakuta mwalimu wa zamu mnoko hatari akanipa adhabu ya kuvuta akanikatia shamba la kulima na kuchimba na kuzisombelea molam ndoo 25 ,shamba nikaajiri wanakijiji kimbembe molam anasimami nikabeba kufika ndoo ya 10 viungo vya mwili vikagoma havina ushirikiano kabisa naumwa kila sehemu nalia hatari nikarud Dom nikampigia mzee nikamwambia akasema nipe namba za mwalimu wako nikampa sijui waliongea nin baadae nashangaa naitwa sikwenda mwl akaja nipo kama nakaribia kufa akaniambia adhabu umesamehewa
Muhula wa pili baada ya mda ikafika kipind cha uchaguz nikasema hapa lazima niwe kiongoz kwa mikaz ya shule naweza kufeli bure nikachukua fomu bahati nzur kichwani nilikua vizuri nikachaguliwa academic
Baada ya kuwa kiongoz ndo maisha yakaanza sasa kwanza nikachagua room nayotaka ,ambazo nitofaut na wanafunz wa kawaida ndani mnakaa wawil tu chumba mapazia ,carpet hapo ndo nikaish kama nipo chuo mpaka namaliza .....
Nashukuru tu Mungu nilifaulu vzuri
Asante, nilishapoaAisee pole sana